Matokeo ya Kidato cha Sita kwa Mwaka 2019 yametangazwa rasmi leo

Kama mwaka huu akikosa chuo ..basi mwakani akiomba kwa usahihi atapata tu
Lakini cha kumshauri akiwa anaomba mwaka huu inabidi aombe kwa umakini mkubwa, asiombe cozi zenye ushindani wa hali ya juu

Dirisha la maombi ya vyuo vikuu linafunguliwa kuanzia tarehe 15/07/2019
Dah kasema ataomba udaktari tu et anataka afuate nyayo zangu !

Private lakini si uhakika ?
 
Anhaa , kwani mwaka jana kuna watu waliopata one ya nane kwa vyuo vya serikali walikosa ?

Wakuu wengine njoen mtoe mchango wenu hapa !

Kwa md ?
Mkuu kwanza mpe Hongera mdogo wako kwa kupata one ya 8, ila kwa miaka ya sasa one ya 8 ni kawaida maana kuna madogo ni mbwa wanakung"uta banda kama hawana akili nzuri.

kwa hiyo one labda ajaribu vyuo vya private tofouti na hapo akasomee unesi...
 
Advance mara zote wapo smart
kismir ina wanafunzi wachache sana mkuu ,ingawa ipo top ten embu angalia mziki st Mary gorret,Marian girls na Boys na hata kibosho girils ,zote hizo zimeipita kwa mbali idadi ya wanafunzi waliopata division one mkuu ,NACTE iache kulinganisha shule zenye wanafunzi wachache na wale walio wengi ili kuweza kipata picha halisi ya ushindani ,zile zenye wanafunzi chini ya mia moja zilinganishwe kivyake mkuu
 
HaYa Matokeo ya kisiasa haya...

Haiwezekani ma Division One yakawa kama mboga...

Sioni wasio na wani kupata vyuo..
 
Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) nchini Tanzania leo Alhamisi Julai 11, 2019 limetangaza matokeo ya kidato cha sita ya mwaka 2019

Katika matokeo hayo yaliyotangazwa na Katibu Mtendaji wa Necta mjini Unguja Zanzibar, Dk Charles Msonde amesema ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 97.58 mwaka 2018 hadi kufikia asilimia 98.32 mwaka 2019 ikiwa ni sawa na asilimia 0.74.
Dk Msonde amesema mtihani huo uliofanyika kati ya Mei 6 hadi 23 mwaka 2019, watahiniwa 91,298 walisajiliwa wakiwamo wasichana 37,948 sawa na asilimia 41.56 na wavulana 53,350 sawa na asilimia 58.44.

Amesema kati ya watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 80,216 na watahiniwa wa kujitegemea walikuwa ni 11, 082.

Katibu mtendaji huyo amesema kati ya watahiniwa 91,298 waliosajiliwa kufanya mtihani , watahiniwa 90,001 sawa na asilimia 98.58 walifanya mtihani na watahiniwa 1,297 sawa na asilimia 1.42 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za ugonjwa na utoro.

Dk Msonde amesema watahiniwa wa shule, kati ya watahiniwa 80,216 waliosajiliwa, watahiniwa 79,770 sawa na asilimia 99,44 walifanya mtihani ambapo wasichana walikuwa 33,883 sawa na asilimia 99.57 na wavulana 45,887 sawa asilimia 99.35. Watahiniwa 446 sawa na asilimia 0.56 hawakufanya mtihani.

Amesema watahiniwa wa kujitegemea kati ya11,082 waliosajiliwa, 10,231 sawa na asilimia 92.32 walifanya mtihani na watahiniwa 851 sawa na asilimia 7.68 hawakufanya.

“Jumla ya watahiniwa 88,069 sawa na asilimia 98.32 ya watahiniwa waliofanya mtihani wamefaulu,” amesema Msonde

Watahiniwa Kumi bora Kitaifa kwa masomo ya Sayansi kuanzia namba moja hadi kumi ni

1. Faith Nicholous Matee (St. Marry’s Mazinde Juu-PCB)
2. Herman Pauline Kamugisha (Kisimiri-PCM)
3. Levina Calist Chami (St. Marry Goretti-PCM)
4. Benius Eustace (Mzumbe-PCB)
5. Augostino Issaya Omari (Ilboru-PCB)
6. Satrumin Arbogast Shirima (Temeke-PCB)
7. Khalid Hussein Abdallah (Feza Boys-PCM)
8. Assad Y. Msangi (Feza Boys-PCM)
9. Peter Jovenal Riima (Kibaha-PCM)
10. Augustine J. Kamba (Feza Boys-PCM)

Wanafunzi 10 bora waliofanya vizuri kwa masomo ya Lugha na Sanaa ni

1. Victor G. Mtui (Feza Boys-EGM)
2. Paula Nelson Lujwangana (St. Marry’s Mazinde Juu-HKL)
3. Blandina Kessy Nyage (St.Marry’s Mazinde Juu-HGL)
4. Eva J. Shitindi (Machame Girls-HKL)
5. Ruhinda Benedicto Machimu (Geita Adventist-HKL)
6. Anita Zacharia Massawe (St.Marry Mazinde Juu-HKL)
7. Karimu Kassimu Muhibu (Nyangao-HKL)
8. Anold Andrea Msuya (Manyara-HKL)
9. Latifa Mohamed Mrosso (Ahmes-HKL)
10. Eliibariki Desidery Baliyanga (Lukole-HKL)

Waliofanya vizuri Kitaifa kwa masomo ya Biashara ni

1. Astone Stevin Ngaeje (Kibaha-ECA)
2. Gift M. Mwakikusi (Tusiime-ECA)
3. Emmanuel P. Chila (Alpha-ECA)
4. Athumani Magadula William (Umbwe-ECA)
5. Stephano Y. Dismas (Kibaha-ECA)
6. Robert John Tano (Scolastika-ECA)
7. Shabani H. Shabani (Kibaha-ECA)
8. Dotee A. Zuberi (Galonos-ECA)
9. Ernest P. Game (Kibaha-ECA)
10. Deogratias Ladislaus Msilinga (Kibaha-ECA)

Katika matokeo hayo Shule Kumi bora zilizoongoza Kitaifa ni

1. Kisimiri (Arusha)
2. Feza Boys (Dar es Salaam)
3. Ahmes (Pwani)
4. Mwandet (Arusha)
5. Tabora Boys (Tabora)
6. Kibaha (Pwani)
7. Feza Girls (Dar es Salaam)
8. St. Marry’s Mazinde Juu (Tanga)
9. Canossa (Dar es Salaam)
10. Kemebos (Kagera)

Shule Kumi zilizofanya vibaya Kitaifa ni

1. Nyamunga (Mara)
2. Haile Salassie (Mjini Magharibi)
3. Tumekuja (Mjini Magharibi)
4. Bumaangi (Mara)
5. Butuli (Mara)
6. Mpendae (Mjini Magharibi)
7. Eckernford (Tanga)
8. Msimbo (Katavi)
9. Mondo (Dodoma)
10. Kiembe Samaki A (Mjini Magharibi)
Hivi mnajua Kisimiri - Arusha ni shule ya Kata!! Nafikiri inafaa kutumika kama case study kwa shule nyingine za kata nchini walimu wakajifunze mbinu pale Kisimiri.
 
Shul
kismir ina wanafunzi wachache sana mkuu ,ingawa ipo top ten embu angalia mziki st Mary gorret,Marian girls na Boys na hata kibosho girils ,zote hizo zimeipita kwa mbali idadi ya wanafunzi waliopata division one mkuu ,NACTE iache kulinganisha shule zenye wanafunzi wachache na wale walio wengi ili kuweza kipata picha halisi ya ushindani ,zile zenye wanafunzi chini ya mia moja zilinganishwe kivyake mkuu
Performance ya shule zinakuwa ranked based % performance ambayo ni fair assessment
 
Hivi mnajua Kisimiri - Arusha ni shule ya Kata!! Nafikiri inafaa kutumika kama case study kwa shule nyingine za kata nchini walimu wakajifunze mbinu pale Kisimiri.
Labda Mbinu za Kuvujisha mtihani..
 
Mkuu kwanza mpe Hongera mdogo wako kwa kupata one ya 8, ila kwa miaka ya sasa one ya 8 ni kawaida maana kuna madogo ni mbwa wanakung"uta banda kama hawana akili nzuri.

kwa hiyo one labda ajaribu vyuo vya private tofouti na hapo akasomee unesi...
Kun mtu kanambia udom au ile campus ya mbeya ya udsm anaweza kupata !
 
Matokeo ya f6 yanatangazwa hivi punde. Tayari Necta wameweka tangazo


Shule ya Sekondari ya Nyamunga ya mkoani Mara imeshika namba moja kati ya shule 10 zilizofanya vibaya kitaifa katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2018.

Matokeo hayo yametangazwa leo Alhamisi Julai 11, 2019 na katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde.

Katika orodha hiyo kuna shule nne za Mjini Magharibi visiwani Zanzibar ambazo ni Kiembesamaki A Islamic, Mpendae, Tumekuja na Haile Selassie.

==>>Hizi ni Shule 10 za Mwisho Kitaifa
1. Nyamunga, Mara.

2. Haile Salassie Mjini Maghari.

3. Tumekuja,mjini Magharib

4. Bumaangi,mara

5. Butuli,mara

6. Mpendae, Mjini Magharib

7. Eckernford, Tanga.

8. Msimbo, Katavi.

9. Mondo, Dodoma.

10. Kiembe Samaki A Mjini Magharib
 
Ngoja ije
Hapa ni wanafunz kumi bora
Mhaya ni mmoja tu lkn Chagas ni 2 na mpare mmoja kilimanjaro ni ngome ya wasomi karne na karne
@instanbul
Screenshot_20190711-202349.jpeg
 
Back
Top Bottom