kajekudya
JF-Expert Member
- Sep 24, 2015
- 2,469
- 4,902
Ukiangalia siasa za mwaka ni dhahiri kuna wanaume wawili wanumiza nyasi, yaani JPM wa CCM na ENL wa CDM/UKAWA. Wanaume hawa wamekuja na staili mpya, staili ya kutengeneza mafuriko lengo likiwa ni kuuaminisha umma wa Tanzania na dunia kwa ujumla kwamba wanakubalika, pamoja na njia zingine nyingi zinazotumika mojawapo ni kuwaleta watu wa maeneo au mikoa jirani kwenda kutengeneza mafuriko eneo mkutano unapofanyika, kweli wanafanikiwa maana watu wanajaa mpaka wengine wanakufaa au kuzimia kwa kukosa hewa au kukanyagana. Lkn kuna kitu hapa hawakiangalii, tareh 25 watu hataweza kutoka eneo moja kwenda lingine kupiga kura, yaani kama una wafuasi 50 katelelo halaf siku ya mkutano wako pale ulileta watu 300 ili utengeneze mafuriko kumbuka tareh 25 ni watu 50 tu watakupigia kura pale katelelo. ninachosema ni kuwa mwaka huu yanaweza yakatokea maajabu kwa either kati ya hawa wawili mmoja kushindwa vibaya, na hakutakuwa na visingizio maana kura zimehesabiwa kila kituo, ingekuwa tofauti kama mfumo wa zamani ungetumika maana amabaye atashindwa angesingizia wizi wa kura wkt wa kusafirisha masanduku na watu wangemuamini maana wakt wa kampeni alipata watu wengi bila kujali wametoka wap, lkn kwa mtindo huu, itakuwa ngumu maana mafuriko hayatakuwa na nafasi ck ya uchaguz ndo maana nasema si CCM wala UKAWA WANASTAHILI KUFURAHIA maana maana wote wanatumia mtindo mmoja, lakin tare 25 itaweka wazi kama kweli haya mafuriko ni ya kweli au feki.