Matokeo Kidato cha Nne 2020: Siku hizi hakuna 'penati' za Civics na Basic Mathematics?

Yaani mtu anasoma sayansi hesabu anapata F msiba huu
Ina staajabisha kwa kweli, huwezi kufauru Physics ngumu then uje ufeli Hesabu rahisi. physics inahitaji Maths knowledge kuweza kufauru.
 
Elimu imekuwa rahisi Sana

St Francis wako 90 waliopata one za 7 wako 79

Mtu aliyekuwa anakuwa wa mwisho darasani Ana one ya 9 daaah!!!

Ina maana siku hizi Mambo simple eeeeh!!!au hao watoto wanafundishwa kujibu paper

So mchezo!!!
 
Siku hizi hawapigi penalty ya kurudisha divion/daraja nyuma. Kwa sasa kinachofanyika kama mwanafunzi ana F ya hesabu hachaguliwi kusoma tahasusi/combination za sayansi hata kama masomo mengine amefaulu vizuri.

Inamaana huyo dogo licha ya kuwa amefaulu vizuri masomo mengine ya sayansi atapigwa penalty ya kwenda kusoma tahasusi ya sanaa/art kwa sababu ya kupata F kwenye hesabu
 
Hata hivyo mleta mada hajui asaidie kitu gani, maelezo yake hayajakamilika. Arudie
Nini hapo hakijakamika? Mada ipo vizuri ni kwamba nyie watoto wa juzi hamuelewi kitu.
Yaani mim niumize kichwa kwa mada za kikuda,, sasa Unataka nimpe dondoo makini ili amshushe daraja mtoto wa watu?

Nyie ndo walewale mliowaponza ajira za ualimu kwa ukudaukuda wenu.

Huwaga najiuliza mkishakosoa ndo mnapata mkate wa siku au laah!

Pamoja na kukosoa kwenu wahusika wanabaki madarakani palepale na ndugu yako au family yako ndio inayoumia.
Either wewe ni mshamba au huna akili. Kama huelewi mada bora usichangie, nasoma comments zako una mihemko isiyokuwa na mantiki.
 
Nini hapo hakijakamika? Mada ipo vizuri ni kwamba nyie watoto wa juzi hamuelewi kitu.
Either wewe ni mshamba au huna akili. Kama huelewi mada bora usichangie, nasoma comments zako una mihemko isiyokuwa na mantiki.
Kabisa,hata mimi nimeona anapuyanga tu!Hapa suala ni jepesi,ilitakiwa mtu anayefahamu kama utaratibu umebadilika basi atueleze!
 
Mimi pia nakataa. Haiwezekani upate physics C, chemistry B, na biology B halafu mathematics upate F... haiwezekani ubahatishe masomo magumu kwa grade nzuri halafu somo jepesi usifike hata D
Nahisi kuna makosa... mtu upate physics C, chemistry B, biology B halafu somo jepesi kuliko hayo mathematics apate F.. yaani hata D aikose?
Kumbe B/Maths ni nyepesi?
Why wanafeli?
 
Elimu imekuwa rahisi Sana

St Francis wako 90 waliopata one za 7 wako 79

Mtu aliyekuwa anakuwa wa mwisho darasani Ana one ya 9 daaah!!!

Ina maana siku hizi Mambo simple eeeeh!!!au hao watoto wanafundishwa kujibu paper

So mchezo!!!
Hahaha, mkuu kwenye kila jambo ukipanga ufaulu lazima kuwe na mtu wa mwisho ila huyo wa mwisho kuna sehemu ukimpeleka atakuwa wa Kwanza, kuna shule zingine unakuta zina wastani wa 70, mwanafunzi asipofikisha huo wastani inatakiwa arudie darasa, sasa fikilia mtoto aanze tangu form one hadi form four anatembea na wastani wa 70 unategemea atapata ufaulu gani?

Huyo wa mwisho kwenye shule kama hiyo ndio unakuta ana wastani wa 72, pia hizo shule zina walimu bora kwenye kila somo mazingira mazuri ya kusomea, watoto wako form 3 ila wamemaliza topic za form four, likizo mtoto anapewa maswali kama 500 kwenye kila somo akirudi akusanye kumbuka hawaruhusiwi kusoma tuition kwakuwa mtaani kuna bora walimu na sio walimu bora hivo ni rahisi mtoto kulishwa matango pori
 
Hata hivyo mleta mada hajui asaidie kitu gani, maelezo yake hayajakamilika. Arudie

Maelezo ya Petro E. Mselewa yamejitosheleza, inaweza ikawa haujasoma viruzi ukamwelewa anachotaka kujua.

Zamani ilikua ukipsta alama za daraja la kwanza lakini ukapata ufaulu wa 'F' baadhi ya masomo, haupewi daraja la kwanza, unapigwa oenalt na kupewa daraja la tatu licha ya kuwa na ufaulu wa point za daraja la kwanza.

Miongoni mwa hayo masomo ilikua hesabu, civics, english na kiswahili ( sina uhakika).

Shule niliyosoma ilikua ni ya ufundi, hivyo masomo ya penati ilikua civics na english, ukifeli hesabu hata hauna pa kwenda kwa sababu ilikua lazima ukasome PCM au uende FTC.
 
Nahisi kuna makosa... mtu upate physics C, chemistry B, biology B halafu somo jepesi kuliko hayo mathematics apate F.. yaani hata D aikose?
Mimi pia nakataa. Haiwezekani upate physics C, chemistry B, na biology B halafu mathematics upate F... haiwezekani ubahatishe masomo magumu kwa grade nzuri halafu somo jepesi usifike hata D
Mkuu kwakweli hii awamu inarudisha sana elimu yetu nyuma kwa kutaka sifa za kuonekana ufaulu umepanda, kuna watoto wengine wanatuhusu kabisa kwenye familia zetu na kwa wao tunajua na unakuta mshajua huyu hawezi kutoboa necta ila cha ajabu matokeo yanatoka kafaulu ata muhusika mwenywe haelewi imekuaje, mfano kuna madogo hawajui kusoma ila mtihani wa darasa la saba wamefaulu kwa wastani wa C, na hapo shule imefaulisha wanafunzi wote

Awamu hii mtoto akifeli basi ujue alikuwa hajiwezi totally na inabidi atafutiwe kitu kingine cha kufanya maana kusoma atapoteza muda, kufaulu imekuwa rahisi sana na imekuwa ni sehemu ya siasa, mitihani ishapoteza dhana ya kuwa kipimo cha uelewa wa watoto wetu tena, tumepiga hatua 10000 kurudi nyuma kwenye elimu
 
Matokeo ya huyu Dogo vipi anaweza kuchukuliwa HKL?

Division 3 pointi 25 CIV-D, HIST-D, GEO-D, KISW-C, ENGL-C, PHY-F, CHEM-D, BIO-D, MATH-F
 
Hiyo kitu haina mashiko tena! Ulikuwa uonevu tu! Siku hizi hakuna cha penalty wala mjombake! Hiyo ilikuwa miaka yetu yaani hapo angeshushwa mpaka div. 3 pamoja na points zake hizo 16. Ila ulikuwa uonevu tu!
Mimi ni miongoni mwa walioshushwaga Kwa kupata F ya hisabati form four nikiwa na point 18 it was unfair
IMG20210117134153.jpg
 
Wakuu, nawasalimu!
Naomba nisaidiwe kuhusu suala la hapo juu. Nimeyaona matokeo fulani ya mwanafunzi ambaye amepata alama 'F' kwenye Basic Mathematics lakini amepata daraja la kwanza la alama 16.
S............​
F​
16​
I​
CIV - 'B' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'B' ENGL - 'B' FREN - 'D' PHY - 'C' CHEM - 'B' BIO - 'B' B/MATH - 'F'​
Ulikuwa ni uonevu mkubwa Mimi ni mhanga wa hayo mambo . Kama ingekuepo kuna uwezekano wangeturekebishia na Sisi tulioonewaga
IMG20210117134153.jpg
 
Back
Top Bottom