Matisho toka kwa viongozi wa CCM kwa Wapinzani

Sema Kweli

Member
Apr 12, 2013
53
20
Ndugu wana jamvi nasikitika sana kwa jinsi demokrasia ya nchi hii inavyo haribiwa na watu wachache,kwa wale walio sikia umafya ulio fanywa makuyuni jinsi watanzania wenzetu walivyo umizwa bila sababu ni kwa kutaka tu kuwalazimisha watanzaa kile ambacho mtu mmoja anataka yeye.

Hizi ni siasa chafu na ambazo ambazo zinaratibiwa na wanasiasa wengi sana huwezi kuamini kuwa baada ya tukio hilo makuyuni leo katika baa ya seven up mbunge mmoja nae anajisifia kwa kusema bado simanjiro,kwa maana hiyo ni jinsi gani utaona kuwa huu ni mpango wa watu wanao ngangania madaraka na kwa kuwa wameona kuwa kwa sasa hawakubaliki wameona njia pekee ni kuwatisha watanzania na ikiwezekana kutengeneza makundi ambayo yatakuwa yanawafanyia wapinzani wa watu hao fujo na ikiwezekana kuwapiga.

Ni tumie nafasi hii kuiambia serikali kuwa kama hawako tayari kuwa na mfumo wa vyama vingi ni vyema wakavifuta mpaka watakapo kuwa tayari kuliko hali hii ikiachwa badhi ya watu kujitengenezea majeshi yao ambayo yameanza kuwaumiza watanznia wenye haki ya kukishabikia au kuksaidia chama wanacho dhania kuwa ndio mkombozi wao.

Pia nichukue nafasi hii kuwapa taarifa hii wanasiasa wote wa simanjiro kuwa mkakati wa kuwaumiza pindi mtakapo kuwa kwenye shughuli za kisiasa katika wilaya yenu ya simanjiro umeanza kuratibiwa na mbunge wa wilaya hiyo,na hili alikuwa akizungumza mwenyewe bila ya kujua kuwa walioko pale kuna ambao wanajua lugha ya aliyo kuwa akituia ya kimasai,nimeona niwajulishe ili kwenye shughuli zenu za kisiasa mjue kuwa kuna mkakati huo ambao ushapangwa.

Labda kwa wale walio karibu na sendeka wamuulize kwa kushabikia nasary kuumizwa kwamba ni kwa nini alienda huko je yeye alipo kuwa meru wakati wa uchaguzi wa nasary pale kulikuwa simanjiro?juzi alikuwa Arusha,mbulu je hapo kulikuwa simanjiro?anataka kuwaambia nini watanzania wengine pale ambapo mwanasiasa yeyote atakae kuwa anafanya siasa wilaya ambayo sio yao haya yaliyo mpata nasary ndio sawa?

Ni vyema sana polisi wakawa wanawahudumia watanzania wote kwa sio sawa kwa sasa kuwaona polisi wanakuwa washabiki wa chama tawala badala ya kuwa walinzi wa wote.

Mwisho watanzania tukumbuke kuwa tanzania ni yetu sote na sio nchi ya kikundi fulani.


 
Wekeni hizo kumbukumbu mana hizo ndo zitakazitumiwa kwenye mahakama ya The Hague, Wamuulize Uhuru na Ruto kwa nini wako kule kwa sasa. Mungu atajibu Muda si mrefu. Hata afya za hao ni mgogoro tu hata kama watatumia mbinuchafu namna gani lakini siku zao ndo hizo zinahesabiwa. Sasa Watanzania ndo wajue kuwa atakayeleta vita na machafuko ya ukweli nchi hii ni CCM ya Mafisadi Papa wenye kutuibia kwenye miradi michafu kama ile ya RichMonduli, nk.

Wao nafsi zao sasa hazina roho wa Mungu wanachoona mbele ni madaraka tu ili watuibie raslimali zetu. Tunawaomba M4C na CHADEMA kwa jumla kuansisha kampeni babu kubwa, tuwaelimishe watu wajue uovu huu mkuu.
 
Back
Top Bottom