akilimtindi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2008
- 421
- 83
Ndugu zanguni Wana-JF, nawapeni pole sana kwa majanga yanayowaandama wapenda haki wa nchi hii na wale wote wanaofanya bidii kuuweka uovu wa nchi hii wazi mbele ya wale wasiojua kinachoendelea.
Binafsi napenda kutoa pole kwa familia ya Kibanda pamoja na familia za wengine wote waliowahi kuumizwa kwa namna moja au nyingine kwenye mfululizo huu wa matukio yenye utata, nalazimika kutoa pole kwa ujumla maana hiki ni kidonda kipya kabla vidonda vingi vya siku kadhaa zilizopita havijapona hata kidogo.
Niombe radhi kwa wanajukwaa maana nimepotea kwa muda hapa jukwaani, lengo langu la kwanza kuandika haya ya leo ni kujaribu kueleza na kusisitiza tena kwamba ukombozi sio lelemama na ni ukweli usiopingika kwamba hii keki ya Taifa hili iko mikononi mwa watu fulani, ambao tulishawaachia nafasi walikaujua utamu wake kwa muda mrefu.
Sio kazi rahisi hata kidogo kwa kuona keki hiyo inawaponyoka na kwenda kusikojulikana ama kwa maneno mengine kwenda wasikoweza kuifikia na kuitafuna kwa jinsi wanavyoweza wao na kwa wakati wanaotaka wao.
Hata hivyo ikiwa sio kazi rahisi wao kuona keki hiyo inawaponyoka, kwa uelewa wangu ni kazi rahisi sana sisi kuichukua keki hiyo na kuirudisha mikononi mwetu kama tutafanya uamuzi...naamini sio wakati sahihi sana kuliongelea hili kwa sasa maana naona kama vile kuna namna Wadanganyika wamechanganyikiwa.
Cha msingi hatutakiwi kulegea, tunapaswa kuangalia mbele na kuendeleza vita hii hadi tutakapofanikiwa kuirudisha keki hii mikononi mwetu sisi wanyonge.
Lengo langu la pili ambalo nadhani ndilo la muhimu zaidi kwa leo ni kuwapa tahadhari wale walio mstari wa mbele kwenye uwanja wetu wa mapambano kukaa mkao makini zaidi, namaanisha wazi kwamba hii ni vita isiyo rasmi lakini yenye kutafuna taratibu.
Tusichukulie matukio kama haya ni mzaha na kuendelea kukaa ki-milegezo, ni muhimu sana tena sana wapambanaji kujifunza mbinu muhimu za mapambano maana hawatafundishwa na yeyote wala haitatokea siku wakaambiwa rasmi wajifunze hayo.
Hakuna jambo la kushangaza, Mungu yu-pamoja nanyi lakini alisisitiza pia kwenye kutumia akili zenu. Simaanishi waliomvamia Kibanda walifanikiwa kwasababu Kibanda kalegea, hapana...namaanisha kuna umuhimu sasa wa kukaa mkao wa kujilinda zaidi ya Kibanda alivyojaribu kujilinda.
Mimi ni Mkristo kwahiyo naomba ninukuu Bibilia, tafakarini mstari usemao "...Jifunzeni kukaa na wana wa giza, iweni na akili kama wana wa giza".
Kama nimekosea wenye kuijua kuliko mimi wanisahihishe, naomba kwa leo niishie hapa na walioko mstari wa mbele wanaoelewa watayafanyia kazi vinginevyo kuna hatari ya kuukimbia uwanja wa mapambano.
Ukihitaji kuendelea na mapambano, moja ya mambo muhimu ni kuangalia kwa upya mbinu zako za mapambano ukilinganisha na mbinu za adui yako pia.
Binafsi napenda kutoa pole kwa familia ya Kibanda pamoja na familia za wengine wote waliowahi kuumizwa kwa namna moja au nyingine kwenye mfululizo huu wa matukio yenye utata, nalazimika kutoa pole kwa ujumla maana hiki ni kidonda kipya kabla vidonda vingi vya siku kadhaa zilizopita havijapona hata kidogo.
Niombe radhi kwa wanajukwaa maana nimepotea kwa muda hapa jukwaani, lengo langu la kwanza kuandika haya ya leo ni kujaribu kueleza na kusisitiza tena kwamba ukombozi sio lelemama na ni ukweli usiopingika kwamba hii keki ya Taifa hili iko mikononi mwa watu fulani, ambao tulishawaachia nafasi walikaujua utamu wake kwa muda mrefu.
Sio kazi rahisi hata kidogo kwa kuona keki hiyo inawaponyoka na kwenda kusikojulikana ama kwa maneno mengine kwenda wasikoweza kuifikia na kuitafuna kwa jinsi wanavyoweza wao na kwa wakati wanaotaka wao.
Hata hivyo ikiwa sio kazi rahisi wao kuona keki hiyo inawaponyoka, kwa uelewa wangu ni kazi rahisi sana sisi kuichukua keki hiyo na kuirudisha mikononi mwetu kama tutafanya uamuzi...naamini sio wakati sahihi sana kuliongelea hili kwa sasa maana naona kama vile kuna namna Wadanganyika wamechanganyikiwa.
Cha msingi hatutakiwi kulegea, tunapaswa kuangalia mbele na kuendeleza vita hii hadi tutakapofanikiwa kuirudisha keki hii mikononi mwetu sisi wanyonge.
Lengo langu la pili ambalo nadhani ndilo la muhimu zaidi kwa leo ni kuwapa tahadhari wale walio mstari wa mbele kwenye uwanja wetu wa mapambano kukaa mkao makini zaidi, namaanisha wazi kwamba hii ni vita isiyo rasmi lakini yenye kutafuna taratibu.
Tusichukulie matukio kama haya ni mzaha na kuendelea kukaa ki-milegezo, ni muhimu sana tena sana wapambanaji kujifunza mbinu muhimu za mapambano maana hawatafundishwa na yeyote wala haitatokea siku wakaambiwa rasmi wajifunze hayo.
Hakuna jambo la kushangaza, Mungu yu-pamoja nanyi lakini alisisitiza pia kwenye kutumia akili zenu. Simaanishi waliomvamia Kibanda walifanikiwa kwasababu Kibanda kalegea, hapana...namaanisha kuna umuhimu sasa wa kukaa mkao wa kujilinda zaidi ya Kibanda alivyojaribu kujilinda.
Mimi ni Mkristo kwahiyo naomba ninukuu Bibilia, tafakarini mstari usemao "...Jifunzeni kukaa na wana wa giza, iweni na akili kama wana wa giza".
Kama nimekosea wenye kuijua kuliko mimi wanisahihishe, naomba kwa leo niishie hapa na walioko mstari wa mbele wanaoelewa watayafanyia kazi vinginevyo kuna hatari ya kuukimbia uwanja wa mapambano.
Ukihitaji kuendelea na mapambano, moja ya mambo muhimu ni kuangalia kwa upya mbinu zako za mapambano ukilinganisha na mbinu za adui yako pia.