Matendo ya Sabaya: Ukweli ni kwamba tulipaswa kupata Serikali Mpya ila tatizo Katiba haisemi hivyo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,991
144,327
Ukifikiri kwa makini, wote waliokuwa mabosi wa Sabaya chini ya Magufuli na wakuu wote wa vgombo vya ulinzi na usalama hawakupaswa kuendelea kuwa madarakani leo hii ila katiba ndio tatizo kwani haitoa hata fursa ya kufanya uchaguzi tupate viongozi wengine ambao bila shaka wangekuja na watendaji tofauti na hawa tulionao leo hii.

Je, Mama, Waziri Mkuu, IGP na Mkuu wa TISSS pamoja na waliowahi kuwa mawaziri wa mambo ya ndani bila kusahau RPC wa Kilimanjaro,OCD na wengineo hawakujua yaliyokuwa yanafanywa na Sabaya?

Kama walijua na wakaendelea kubaki Serikalini, leo hii wanastahili kuwa madarakani au baadhi yao wanastahili wawajibike kwa makosa ya Sabaya aliokuwa chini yao?

Labda Mkuu wa TISS na wasaidizi wake wanaweza kuwa na la kujitetea iwapo walitimiza wajibu wao ila hawa watendaji wengine ama walipaswa kujiuzulu kupinga matendo ya Sabaya au kuchukua hatua.

Kama watu wakitaka tu kuandamana serikali kupitia Jeshi la Polisi wanachukua hatua. Vipi kwa Sabaya kutenda yote haya na serikali ilikuwepo? Intelijensia ya Polisi inayotambua hatari ya maandamano ya wapinzani ilikuwa wapi kubaini matendo haya ya Sabaya?

Nawaza tu tutasikia mambo gani ikitokea kesi ya waliotaka kumua Lissu kwa risasi inatinga mahakamani kama tumesikia haya kwa Sabaya aliedai kutekeleza maagizo kutoka juu?
 
Sabaya ni shujaa anakaa level moja na Mandela.

Sabaya atatoka na kuwa kiongozi tena
 
Ndani ya mfumo uliooza huwezi kumpata kiongozi mzuri, kwa hatua waliyofikia sasa anaangaliwa mwenye nafuu tu.
 
Heheheh chadema mashetani sana. Wanataka serikali yote ijiuzuru ili wao waingie madarakani kiulaini. Chadematafuteni namna ya kuingua ikulu ila sio kwa njia hiyo.
 
Ukifikiri kwa makini, wote waliokuwa mabosi wa Sabaya chini ya Magufuli na wakuu wote wa vgombo vya ulinzi na usalama hawakupaswa kuendelea kuwa madarakani leo hii ila katiba ndio tatizo kwani haitoa hata fursa ya kufanya uchaguzi tupate viongozi wengine ambao bila shaka wangekuja na watendaji tofauti na hawa tulionayo leo hii.

Je, Mama,Waziri Mkuu, IGP na Mkuu wa TISSS pamoja na waliowahi kuwa mawaziri wa mambo ya ndani bila kusahau RPC wa Kilimanjaro,OCD na wengineo hawakujua yaliyokuwa yanafanywa na Sabaya?

Kama walijua na wakaendelea kubaki serikalini, leo hii wanastahili kuwa madarakani au wawajibike kwa makosa ya Sabaya aliokuwa chini yao?

Labda Mkuu wa TISS na wasaidizi wake wanaweza kuwa na la kujitetea iwapo walitimiza wajibu wao ila hawa watendaji wengine ama walipaswa kujiuzulu kupinga matendo ya Sabaya au kuchukua hatua.

Kama watu wakitaka tu kuandamana serikali kupitia Jeshi la Polisi wanachukua hatua. Vipi kwa Sabaya kutenda yote haya na serikali ilikuwepo? Intelijensia ya Polisi inayotambua hatari ya maandamano ya wapinzani ilikuwa wapi kubaini matendo haya ya Sabaya?

Nawaza tu tutasikia mambo gani ikitokea kesi ya waliotaka kumua Lissu kwa risasi inatinga mahakamani kama tumesikia haya kwa Sabaya aliedai kutekeleza maagizo kutoka juu?
Ndiyo maana wana lumumba ukiwaambia habari za katiba mpya wanakuona msaliti.
 
tena tulipaswa tuwe na serikali inayo undwa na genge la kihalifu likiingozwa na Gaidi namba 1.
 
Ukifikiri kwa makini, wote waliokuwa mabosi wa Sabaya chini ya Magufuli na wakuu wote wa vgombo vya ulinzi na usalama hawakupaswa kuendelea kuwa madarakani leo hii ila katiba ndio tatizo kwani haitoa hata fursa ya kufanya uchaguzi tupate viongozi wengine ambao bila shaka wangekuja na watendaji tofauti na hawa tulionayo leo hii.

Je, Mama,Waziri Mkuu, IGP na Mkuu wa TISSS pamoja na waliowahi kuwa mawaziri wa mambo ya ndani bila kusahau RPC wa Kilimanjaro,OCD na wengineo hawakujua yaliyokuwa yanafanywa na Sabaya?

Kama walijua na wakaendelea kubaki serikalini, leo hii wanastahili kuwa madarakani au wawajibike kwa makosa ya Sabaya aliokuwa chini yao?

Labda Mkuu wa TISS na wasaidizi wake wanaweza kuwa na la kujitetea iwapo walitimiza wajibu wao ila hawa watendaji wengine ama walipaswa kujiuzulu kupinga matendo ya Sabaya au kuchukua hatua.

Kama watu wakitaka tu kuandamana serikali kupitia Jeshi la Polisi wanachukua hatua. Vipi kwa Sabaya kutenda yote haya na serikali ilikuwepo? Intelijensia ya Polisi inayotambua hatari ya maandamano ya wapinzani ilikuwa wapi kubaini matendo haya ya Sabaya?

Nawaza tu tutasikia mambo gani ikitokea kesi ya waliotaka kumua Lissu kwa risasi inatinga mahakamani kama tumesikia haya kwa Sabaya aliedai kutekeleza maagizo kutoka juu?
IGP alipewa taarifa mapema sana za uchafu wa OCD Mpina aliyeshirikiana na Sabaya hata kwenye Ubakaji lakini akapuuza , kiukweli Sirro amelifanya jeshi la polisi lidharaulike sana .
 
Bora tuongozwe na ccm milele kuliko genge la kihuni.
Chadema imechafuka sana kutokana na tuhuma za Ugaidi za Mbowe, pia imevitia doa vyama vya upinzani.
alikitumia chama kama mwamvuli kutekeleza uhalifu!! hafai!! amekichafua sana chama.
Kabla ya hapo kweli chadema ilikuwa ni chama mbadala cha upinzani chenye hoja madhubuti, kipindi cha Dr. Slaa lkn badae chadema kilipoteza mwelekeo.
ona sasa viongozi wa chadema, eti Mnyika!!
Benson!! n.k hamna kitu kabisaa!
 
Back
Top Bottom