Matawi ya vyama vya siasa nje ya nchi, nini sifa za uanachama?

Kaduguda

JF-Expert Member
Aug 1, 2008
724
641
Heshima mbele wadau wote!

Nimekuwa nikitatizwa sana haswa ninapoona huu utitiri wa matawi ya vyama vya Siasa haswa vya Tanzania kufungua matawi nje ya nchi na haswa nchi za magharibi na India. Kwani sijasikia Labour, Republicans wala Democrats kufungua matawi nje ya nchi zao.

Hivi nini haswa sifa ya mtu kuwa mwanachama huko ughaibuni? Je ni kwa mtu aliye mtanzania tu au hata aliyeukana uraia wake anaruhusiwa? Kama mtu ameukana uraia wa TZ na kujibandika wa USA au UK nadhani si mtanzania tena huyo na hivyo moja kwa moja anapoteza stahili yake.

Hofu yangu ni kuwa na wanachama wa vya vyama vyetu vya siasa ambao si wa-Tanzania na hivyo kupoteza ile maana halisi ya vyama vyetu. Hii ni kusema kwamba yeyote yule pasipo kujali uraia wake anaweza kujiunga na chama chetu au kuanzisha tawi popote pale duniani apendapo. Kitu hiki hakiniingii akilini kabisa.

Mods kama hii imeshajadiliwa sehemu waweza ihamishie huko!

Nawakilisha
 
Last edited:
zaidi ya CCM ambao wanajitangaza rasmi, Je kuna vyama vingine venye kufanya hivyo?
 
Heshima mbele wadau wote!


Hofu yangu ni kuwa na wanachama wa vya vyama vyetu vya siasa ambao si wa-Tanzania na hivyo kupoteza ile maana halisi ya vyama vyetu. Hii ni kusema kwamba yeyote yule pasipo kujali uraia wake anaweza kujiunga na chama chetu au kuanzisha tawi popote pale duniani apendapo. Kitu hiki hakiniingii akilini kabisa.


....akili yako ni sifuri maana zero ina afadhari!
 
Ni kutafuta ulaji tu.

Sifa ni kuwa na ulafi uliokubuhu kiasi cha kushindwa kutambua tofauti kati ya utu na unyama. Hawana tofauti na vibaka wanaokimbilia eneo la ajali si kuwasaidia waliopata maafa bali kuwaibia bila huruma yoyote. Waache tu wajiunge, inatusaidia kuwatambua mapema the "fisadis-to-be" na hivyo kuwa rahisi kuwatosa wakati muafaka ukifika.
 
Sifa ni kuwa na ulafi uliokubuhu kiasi cha kushindwa kutambua tofauti kati ya utu na unyama. Hawana tofauti na vibaka wanaokimbilia eneo la ajali si kuwasaidia waliopata maafa bali kuwaibia bila huruma yoyote. Waache tu wajiunge, inatusaidia kuwatambua mapema the "fisadis-to-be" na hivyo kuwa rahisi kuwatosa wakati muafaka ukifika.
Kwa maneno mengine wanaojiunga na vyama vya siasa ni mafisadi to be, na mafisadi ni wale ambao sasa ni wanasiasa katika vyama mbalimbali vya siasa?
 
Kwa maneno mengine wanaojiunga na vyama vya siasa ni mafisadi to be, na mafisadi ni wale ambao sasa ni wanasiasa katika vyama mbalimbali vya siasa?

Ukweli ni kuwa tunapoongelea matawi ya vyama vya sasa nje ya nchi tunaongelea CCM. Sasa swali lililo mbele yetu ni nini sifa za uanachama kwenye matawi ya vyama vya siasa nje ya nchi ? Inawezekana vyama vingine vikawa na wapenzi nje ya nchi, lakini ni CCM tu inaweza kuwa na jeuri ya kuwabagua Watanzania nje ya nchi kwa kufungua matawi. Hili kwangu ni sera ya kifisadi na kama una mawazo tofauti, naomba uwasilishe na ushahidi - mimi ninao.

Labda ningeandika hivi - Kwa maneno mengine wanaojiunga na CCM nje ya nchi ni mafisadi to be, na mafisadi ni wale ambao sasa ni wanasiasa katika CCM? Je, hapa tunakubaliana ?
 
- Mimi ni mwanachama wa CCM, lakini ya kuanzisha matawi ya CCM Ulaya ni a little too much kwa wahusika.

- Nijuavyo huko majuu ni kwamba wananchi wanyonge huwatanguliza watoto wa vigogo wa CCM, mbele huku wao wakijficha nyuma yao halafu baadaye hujipenyeza ili wasonge mbele, ndivyo mbunge mmoja Nyami alivyofanya kule Minnesota, akajificha nyuma ya mtoto wa Mkapa na kumuingia mama yake, sasa ni mheshimiwa mbunge.

- Sasa the question ni kama mbunge au kiongozi yoyote wa kuingia kwenye system kwa njia hii kweli anaweza kutusaidia wananchi wanyonge at large, kuliko waliomfikisha huko juu?
 
- Mimi ni mwanachama wa CCM, lakini ya kuanzisha matawi ya CCM Ulaya ni a little too much kwa wahusika.

- Nijuavyo huko majuu ni kwamba wananchi wanyonge huwatanguliza watoto wa vigogo wa CCM, mbele huku wao wakijficha nyuma yao halafu baadaye hujipenyeza ili wasonge mbele, ndivyo mbunge mmoja Nyami alivyofanya kule Minnesota, akajificha nyuma ya mtoto wa Mkapa na kumuingia mama yake, sasa ni mheshimiwa mbunge.

- Sasa the question ni kama mbunge au kiongozi yoyote wa kuingia kwenye system kwa njia hii kweli anaweza kutusaidia wananchi wanyonge at large, kuliko waliomfikisha huko juu?

On this tuko pamoja
 
Mkuu FMES siku zote husema ukweli hata kama unahusu mambo ambayo hukubaliani nayo yanayofanywa na chama chako, hapo nakuvulia kofia Mkuu!! laiti kama CCM ingekuwa na watu hasa ngazi za juu ambao siku zote wanatetea ukweli kama ufanyavyo wewe basi wengi wetu labda tungeiona CCM tofauti na tunavyoiona sasa, kwamba ni chama cha mafisadi. Hongera kwa hili Mkuu.
 
Jamii ya watanzania inahitaji mabadiliko na kusonga mbele. Kitendo cha baadhi ya watanzania waishio nje ya Tanzania kwa utashi wao walipoamua kushiriki siasa za nyumbani kwa kuanzisha matawi ya ya CCM inaonesha ni jinsi mahitaji yanavyokuwa katika jamii. Wakati ni ukuta ukipigana nao utaumia mwenyewe. Tunaweza kupinga mabadiliko lakini hatuwezi kuyazuia yasitokee. Kiashirio cha kuonesha jamii inabadilika ni pamoja na kutokea mambo mapya au tofauti na yale yaliyozoeleka.
Zaidi ya hapo kuishi nje ya mpaka watanzania katika ulimwengu huu ambao umepunguzwa kwa kiwango cha kuonekana kijiji kimoja kama sio mtaa mmoja, ni rahisi kushiriki jambo lolote hata kama si siasa (mathalani sasa hivi ninawasilana na watanzania kutoka kila kona ya dunia) kutokea popote pali ulipo ili mradi tu una nyenzo muafaka.
Ninashauri ndugu zangu watanzania tutumie fursa tulizonazo au zilizopo sasa hivi kufanya lolote lile ambalo tunadhani linaweza kuvunja barriers za kuwa mnyonge. Kama unataka kufanya biashara na huwezi basi unakuwa mnyonge, kama unataka kucheza soka na huna facilities, then unakuwa mnyonge, halikadhalika kama unataka kushiriki siasa na huna pa kushiriki basi utakuwa mnyonge. Tutumie fursa zilizopo kuondoa unyonge miongoni mwetu.
I support wale watanzania wenye common interest kukaa pamoja na kujadili yale wanayoona yana manufaa kwao.
 
Mkuu nipo na wewe kwenye hayo uliyoongea. Issue inakuja pale wale waliodiriki kwa utashi wao kuukana uraia wa TZ na kuchukua makaratasi kisha sasa kurudi tena kuwa wanachama wa nchi nyingine. Kwa maana halisi hawa si wa-Tanzania japo asili yao ni Tanzania.

Binafsi nipo EU lakini sioni kama ni halali kufungua tawi la CCM kwenye nchi ya watu ambako hakuendani na makusudi ya maana ya chama cha siasa (Kushika hatamu za uongozi wa nchi au serikali). CCM kushika hatamu za uongozi USA, yawezekana hiyo??

Sikatai vyama vya kushirikiana/vya kijamii, kishule nk, ni muhimu sana nami nimo miongoni mwao, lakini inapokuja siasa naona tunavuka mipaka. Unless niambiwe leo kwamba hao members wana uraia halali wa Tanzania, na wapo huko kwa sababu maalumu then watarudi nyumbani, japo haihalalishi kuwa na tawi. ANC, SWAPO na vinginevyo viliwahi kuwa na members wao TZ lakini kwa makusudi ya kujipanga kutetea na kupigania uhuru wa nchi zao, sasa CCM wanampigania nani UK, USA na India?

Nachelea kusema kwamba iko siku utaundwa mkoa wa kisiasa wa ULAYA, na wao watadai uwakilishi NEC na kwingineko!!!!!!tusubiri tuone kwa speed hii.
 
Hizi ni njaa za zilizohamia vichwani kutoka mifukoni, these guyz are disparately hopeless!! wanatafuta cheap popularity na kuna hata wengine hapa UK hawana legal document za kuishi hapa, wako mbele mbele na CCM yao!! Tawi la CCM UK walitumiwa USD 10,000 eti za kuendeshea chama nasikia, wacha waanze kugombana hata kuwekana utamu hahahah....

Ujinga na uhayawani wanatafuta njia rahisi kujiingiza chamani...wakija viongozi wa juu ni balaa kila mtu katinga bendera ya CCM na shati hahahah Tshirt na jeans wanasahau, acheni unafiki fanyeni kilichowaleta mrudi mkatumikie nchi

Masa wa Nilo
 
Mkuu nipo na wewe kwenye hayo uliyoongea. Issue inakuja pale wale waliodiriki kwa utashi wao kuukana uraia wa TZ na kuchukua makaratasi kisha sasa kurudi tena kuwa wanachama wa nchi nyingine. Kwa maana halisi hawa si wa-Tanzania japo asili yao ni Tanzania.

Binafsi nipo EU lakini sioni kama ni halali kufungua tawi la CCM kwenye nchi ya watu ambako hakuendani na makusudi ya maana ya chama cha siasa (Kushika hatamu za uongozi wa nchi au serikali). CCM kushika hatamu za uongozi USA, yawezekana hiyo??

Sikatai vyama vya kushirikiana/vya kijamii, kishule nk, ni muhimu sana nami nimo miongoni mwao, lakini inapokuja siasa naona tunavuka mipaka. Unless niambiwe leo kwamba hao members wana uraia halali wa Tanzania, na wapo huko kwa sababu maalumu then watarudi nyumbani, japo haihalalishi kuwa na tawi. ANC, SWAPO na vinginevyo viliwahi kuwa na members wao TZ lakini kwa makusudi ya kujipanga kutetea na kupigania uhuru wa nchi zao, sasa CCM wanampigania nani UK, USA na India?

Nachelea kusema kwamba iko siku utaundwa mkoa wa kisiasa wa ULAYA, na wao watadai uwakilishi NEC na kwingineko!!!!!!tusubiri tuone kwa speed hii.

Mkuu,
Mimi nadhani usiogope changes kwani changes ndiyo wote tunazipigia kelele hapa. Tuanze sisi kuwa mabadiliko badala ya kuyangojea.

Matawi ya CCM nje ya Tanzania hayana athari yeyote kwa watanzania au nchi husika. Ukitaka kuanzisha tawi la chama chochote EU unataruhusiwa kwani itabidi ulisajili katika local authorities za huko na utaelezea madhumuni yako. Hawa jamaa wenye ngozi nyeupe walishavuka huku sisi ambapo bado tunasuasua.
Be open minded person na kuamini kwa dhati kabisa kwa kile unachoona ni kizuri na kina manufaa kwako au jamii.

Usingoje mabadiliko, kuwa mabadiliko!
 
Kuhusu hili inatupasa tujiulize na tujitafiti sana. Vipaumbele vya watz waliopo ughaibuni ni nini? Kuona nchi inaenda katika mwelekeo sahihi, kwa kuwaondolea watz umaskini uliotopea na kuheshimu utawala bora au kulilinda tabaka la kifisadi? Hapo ndipo tunapopoteza mwelekeo, inavyoonyesha ubinafsi unaotafuna nchi kwa watu kujilimbikizia mali kwa kuifanya jamii yote masikini ndivyo wanavyojisikia walio nje ya nchi kwamba walau wanaweza kupata mlo wao, basi inatosha waliopo nyumbani walie, na tena bora kuambatana na wezi, mafisadi ili nao wafahamike kama wanapenda UFISADI, kwa sababu inaonyesha maisha yanakuwa guaranteed kwa kuwa mwanachama wa CCM. Hata hivyo sijui kama elimu imetukomboa au vipi? Elimu gani inayokufanya uwe mtumwa wa fikra za kifisadi?
 
Hizi ni njaa za zilizohamia vichwani kutoka mifukoni, these guyz are disparately hopeless!! wanatafuta cheap popularity na kuna hata wengine hapa UK hawana legal document za kuishi hapa, wako mbele mbele na CCM yao!! Tawi la CCM UK walitumiwa USD 10,000 eti za kuendeshea chama nasikia, wacha waanze kugombana hata kuwekana utamu hahahah....

Ujinga na uhayawani wanatafuta njia rahisi kujiingiza chamani...wakija viongozi wa juu ni balaa kila mtu katinga bendera ya CCM na shati hahahah Tshirt na jeans wanasahau, acheni unafiki fanyeni kilichowaleta mrudi mkatumikie nchi

Masa wa Nilo

Mambo mengine hayaiingii akilini. Ingeeeleweka kama wao si ndiyo walitakiwa watume dola ya kuendeshea chama chao.
 
swala sio hilo tu kuna tetesi kwamba viongozi wengi wa ccm nje ya nchi wamejipiga, na wanakaratasi which raise a question to their intergrity na kikatiba wanakuwa hawa qualify
 
Back
Top Bottom