Upinzani wa kweli hakuna Tanzania. Vyama vingi vya upinzani ni matawi ya CCM ama kuna watu wa CCM wamepandwa ndani yake. Ukombozi wa Mtanzania uko mbali sana. Angalieni upuuzi wa msomi na mwanasheria aliyebobea.
2009-01-19
DK MVUNGI AYEYUSHA RAI YA KUMSHITAKI MKAPA
Written by James Magai
MHADHIRI maarufu wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengondo Mvungi, amesema hakuna sheria inayoweza kutumika kumshitaki Rais mstaafu Benjamin Mkapa, kwa mambo anayotuhumiwa.
Kauli hiyo ya Dk Mvungi, inakuja wakati kukiwa na shinikizo kutoka kwa baadhi ya wanasiana na wanaharakati, kutaka kiongozi huyo aondolewe kinga ili ashitakiwe kwa tuhuma za kufanya biashara akiwa Ikulu.
Wanasiasa hao ni pamoja na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Wilbroad Slaa. Dk Slaa pia ni Mbunge wa Karatu
Hivi karibuni, Mohamed ambaye pia ni msemaji wa kambi ya upinzani bungeni, alielezea azma yake ya kutaka kuwasilisha hoja binafsi bungeni, kumtaka Mkapa aondoelewe kinga na hatimaye ashitakiwe.
Kwa upande wake, Dk.Slaa amekuwa akidai kuwa Mkapa anaweza kushitakiwa hata bila kuondolewa Kinga.
Lakini akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu kuhusu uwezekano wa kumfungulia mashatka Mkapa kwa uthuma hizo, Dk. Mvungi ambaye ni mtaalamu wa Sheria na Katiba, alisisitiza kuwa hakuna sheria yoyote inayoweza kumtia hatia Mkapa.
Dk. Mvungi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, aliliambia Mwananchi kuwa watu wanaomjadili Mkapa wanajadili kwa hoja nyepesi tu ambazo hazina nguvu za kisheria.
"Hakuna sheria inayoweza kushitaki Mkapa kwa tuhuma za kufanya biashara akiwa Ikulu.Wale wote wanaojadili hoja hiyo wanajadili kwa hoja nyepesi tu na wanasukumwa na emotions (maono) zao tu na si kwa misingi ya kisheria," alisema Dk. Mvungi.
Alisema ingawa Mkapa wakati wa utawala wake aliwaminya na kuwakandamiza wapinzani, lakini kwa hili yeye kama mtaalamu wa sheria hawezi kutumia kigezo hicho cha uhasama wa kisiasa,wala taaluma yake kama silaha kushinikiza kumwangamiza na kwamba anazungumza kisheria.
Ingawa alikiri kuwa kitendo cha Mkapa kufanya biashara akiwa rais wa nchi hakifai, lakini alisema kisheria rais kufanya biashara si kosa na kwamba hakuna sheria inayomzuia kufanya biashara.
"Hata kwenda kukopa pesa benki, siyo kosa, ila tu inaweza kuonekana kuwa umepewa kipaumbele kwa sababu ya nafasi yako, lakini bado hakuna sheria inayomzuia kiongozi yeyote wa seriakali wala hata awe rais kuomba mkopo benki," alisema Dk. Mvungi.
Alisema yeye akiwa mwalimu wa sheria, anazungumza kitaalamu na kwa ushahidi wa kisheria,na kwamba kwa tuhuma hizo dhidi ya Mkapa haoni kosa la kisheria.
"Kama wanasema ni kosa basi wanieleze hapa kosa ni lipi na wanioneshe ni sheria gani inayomshitaki,"alisisitiza Dk.Mvungi.
Alisema wanaojadili suala la Mkapa kabla ya kwenda mahakamani kumfungulia mashitaka kwa kufanya biashara Ikulu inabidi kwanza waangalie Katiba ya nchi, Sheria ya Mambo ya Urais (Presidential Affairs Act) na Sheria ya Huduma za Jamii (Public Service Act).
"Kama kuna kifungu cha sheria kinachozuia rais kufanya biashara wakilete tukijadilina kama hakuna basi tuache kupiga kelele, vinginevyo turudi na tuangalie sheria zetu,kwa kuwa zina mapungufu".
Akitetea hoja zake Dk. Mvungi alisema yako mambo mengi tu ambayo hayafai kufanywa na na kiongozi au raia yeyote kimaadili, lakini si kinyume cha sheria na hivyo mtu hawezi kushitakiwa kwa kuwa hakuna sheria inayovunjwa.
"Mkapa anaweza kuitwa kwenye Tume ya Maadili ya viongozi na kuhojiwa kama kweli alifanya biashara ndani ya Ikulu,na hata kama akikiri bado hatuwezi kumfungulia mashitaka" ,alisema Dk Mvungi.
Aliongeza kuwa ikiwa Mkapa atakiri mbele ya tume hiyo, itakuwa nafasi ya kurekebisha sheria za nchi kwa ajili ya kukabiliana na rais ajaye na si kurudi nyuma hata kwa yule aliyefanya mambo kama hayo kabla ya marekebisho ya sheria hiyo.
Dk. Mvungi anakuwa ni mwanasiasa wa kwanza kumtetea Mkapa kwa hoja za kitaalam, tangu tuhuma dhidi yake zilipoibuliwa na wanasiasa kuanza kujadiliwa kwa mtizamo wa kutaka kumshitaki.
Watu wengi ambao wamekuwa wakimtetea Mkapa dhidi ya tuhuma hizo,wakiwemo wabunge,wanaharakati viongozi wa kidini na wananchi wa kawaida wamekuwa wakimtetea Mkapa kwa hoja za kiutendaji wake tu kuwa amelileta taifa heshima na si kwa misingi ya kisheria.
Mkapa anatuhumiwa akiwa madarakani alianzisha kampuni ya Kiwira Coal Mine ambayo ilinunua mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira akishirikiana na aliyekuwa Waziri wake wa Nishati na Madini Daniel Yona.
Comments Add New Search
Write comment
Name:
Email: do not notifynotify
Title:
Powered by !JoomlaComment 3.23
3.23 Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Next >
[ Back ]
2009-01-19
DK MVUNGI AYEYUSHA RAI YA KUMSHITAKI MKAPA
Written by James Magai
MHADHIRI maarufu wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengondo Mvungi, amesema hakuna sheria inayoweza kutumika kumshitaki Rais mstaafu Benjamin Mkapa, kwa mambo anayotuhumiwa.
Kauli hiyo ya Dk Mvungi, inakuja wakati kukiwa na shinikizo kutoka kwa baadhi ya wanasiana na wanaharakati, kutaka kiongozi huyo aondolewe kinga ili ashitakiwe kwa tuhuma za kufanya biashara akiwa Ikulu.
Wanasiasa hao ni pamoja na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Wilbroad Slaa. Dk Slaa pia ni Mbunge wa Karatu
Hivi karibuni, Mohamed ambaye pia ni msemaji wa kambi ya upinzani bungeni, alielezea azma yake ya kutaka kuwasilisha hoja binafsi bungeni, kumtaka Mkapa aondoelewe kinga na hatimaye ashitakiwe.
Kwa upande wake, Dk.Slaa amekuwa akidai kuwa Mkapa anaweza kushitakiwa hata bila kuondolewa Kinga.
Lakini akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu kuhusu uwezekano wa kumfungulia mashatka Mkapa kwa uthuma hizo, Dk. Mvungi ambaye ni mtaalamu wa Sheria na Katiba, alisisitiza kuwa hakuna sheria yoyote inayoweza kumtia hatia Mkapa.
Dk. Mvungi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, aliliambia Mwananchi kuwa watu wanaomjadili Mkapa wanajadili kwa hoja nyepesi tu ambazo hazina nguvu za kisheria.
"Hakuna sheria inayoweza kushitaki Mkapa kwa tuhuma za kufanya biashara akiwa Ikulu.Wale wote wanaojadili hoja hiyo wanajadili kwa hoja nyepesi tu na wanasukumwa na emotions (maono) zao tu na si kwa misingi ya kisheria," alisema Dk. Mvungi.
Alisema ingawa Mkapa wakati wa utawala wake aliwaminya na kuwakandamiza wapinzani, lakini kwa hili yeye kama mtaalamu wa sheria hawezi kutumia kigezo hicho cha uhasama wa kisiasa,wala taaluma yake kama silaha kushinikiza kumwangamiza na kwamba anazungumza kisheria.
Ingawa alikiri kuwa kitendo cha Mkapa kufanya biashara akiwa rais wa nchi hakifai, lakini alisema kisheria rais kufanya biashara si kosa na kwamba hakuna sheria inayomzuia kufanya biashara.
"Hata kwenda kukopa pesa benki, siyo kosa, ila tu inaweza kuonekana kuwa umepewa kipaumbele kwa sababu ya nafasi yako, lakini bado hakuna sheria inayomzuia kiongozi yeyote wa seriakali wala hata awe rais kuomba mkopo benki," alisema Dk. Mvungi.
Alisema yeye akiwa mwalimu wa sheria, anazungumza kitaalamu na kwa ushahidi wa kisheria,na kwamba kwa tuhuma hizo dhidi ya Mkapa haoni kosa la kisheria.
"Kama wanasema ni kosa basi wanieleze hapa kosa ni lipi na wanioneshe ni sheria gani inayomshitaki,"alisisitiza Dk.Mvungi.
Alisema wanaojadili suala la Mkapa kabla ya kwenda mahakamani kumfungulia mashitaka kwa kufanya biashara Ikulu inabidi kwanza waangalie Katiba ya nchi, Sheria ya Mambo ya Urais (Presidential Affairs Act) na Sheria ya Huduma za Jamii (Public Service Act).
"Kama kuna kifungu cha sheria kinachozuia rais kufanya biashara wakilete tukijadilina kama hakuna basi tuache kupiga kelele, vinginevyo turudi na tuangalie sheria zetu,kwa kuwa zina mapungufu".
Akitetea hoja zake Dk. Mvungi alisema yako mambo mengi tu ambayo hayafai kufanywa na na kiongozi au raia yeyote kimaadili, lakini si kinyume cha sheria na hivyo mtu hawezi kushitakiwa kwa kuwa hakuna sheria inayovunjwa.
"Mkapa anaweza kuitwa kwenye Tume ya Maadili ya viongozi na kuhojiwa kama kweli alifanya biashara ndani ya Ikulu,na hata kama akikiri bado hatuwezi kumfungulia mashitaka" ,alisema Dk Mvungi.
Aliongeza kuwa ikiwa Mkapa atakiri mbele ya tume hiyo, itakuwa nafasi ya kurekebisha sheria za nchi kwa ajili ya kukabiliana na rais ajaye na si kurudi nyuma hata kwa yule aliyefanya mambo kama hayo kabla ya marekebisho ya sheria hiyo.
Dk. Mvungi anakuwa ni mwanasiasa wa kwanza kumtetea Mkapa kwa hoja za kitaalam, tangu tuhuma dhidi yake zilipoibuliwa na wanasiasa kuanza kujadiliwa kwa mtizamo wa kutaka kumshitaki.
Watu wengi ambao wamekuwa wakimtetea Mkapa dhidi ya tuhuma hizo,wakiwemo wabunge,wanaharakati viongozi wa kidini na wananchi wa kawaida wamekuwa wakimtetea Mkapa kwa hoja za kiutendaji wake tu kuwa amelileta taifa heshima na si kwa misingi ya kisheria.
Mkapa anatuhumiwa akiwa madarakani alianzisha kampuni ya Kiwira Coal Mine ambayo ilinunua mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira akishirikiana na aliyekuwa Waziri wake wa Nishati na Madini Daniel Yona.
Comments Add New Search
Write comment
Name:
Email: do not notifynotify
Title:
Powered by !JoomlaComment 3.23
3.23 Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."
Next >
[ Back ]