Matatizo ya wabunge wa kuteuliwa!

Mugishagwe

JF-Expert Member
Apr 28, 2006
300
58
Jamani salaam tena na leo narudi kutaka kujifunza. Nimeona mjadala wa mgombea binafsi unapamba moto na nikaanza kujiuliza kama Mtikila ama Mzee Es anaweza naye kwenda kuomba kufata Wabunge wa Kuteuliwa ama Viti maalam.

Sasa ninavyoona ni kwamba hawana maana wakati majimbo yote ya Tanzania yana wawakilishi Bungeni na ni gharama kubwa kwa Taifa ikifika wameshaulamba ukuu.

Nchi ya Tanzania ni ya Vyama vingi na haki ya kuchagua vongozi wamepewa Watanzania kwa nini tuwe na watu wa maalum ambao ni mzigo wa walipa kodi. Wanamwakilisha nani na wana nguvu gani ukiachilia mbali kuwa ni Wabunge? Rais kuwa na wake 10 na Vyama vya upinzani kupewa kutoa Wabunge wa cheee je ni sahihi?

Mtanisamehe maana hata mwalimu aliwahi kusema Mugishagwe una kichwa kigumu kuelewa nikamuuliza kwa nini akasema huwa unangoja linatokea baada ya muda ndipo unazuka na maswali. Sasa nakuja kwenu nipeni msaada wa maoni yenu nione kama naweza kutinga Mahakamani kupingana na watu hawa ambao nadhani hawana haja kwa kuwa majimbo yote yana Wabunge wa kupigiwa kura na tena kuwapa upendeleo ni Ubaguzi kwa mujibu wa Katiba maana makundi mengine hayajawakilishwa Bungeni pia.
 
Heshima Mkuu,

Wabunge wa kuteuliwa na rais, nia na madhumuni ilikuwa kuwapa nafasi professionals ambao hawawezi kugombea ubunge kuwa mawaziri, yaani kumpa rais nafasi ya kuchagua mawaziri nje ya wabunge,

Ni sheria iliyopitishwa na bunge la jamhuri, wakiwemo wabunge wa upinzani, na wawakilishi wa CUF,

Leo ZNZB, kuna wabunge kumi wa kuteuliwa na rais na kati yao kuna mpaka wa upinzani, na Bara ni hivyo hivyo.

Nia nyngine ya hii sheria ya bunge ilikuwa ni kuwapatia nafasi vilema na wasiojiweza,

Now with all that said, sina tatizo na nia na madhumuni ya hii sheria kwani viongozi kama Asha Rose wasingeweza kuwapo kwenye cabinet, na ni mmoja wa kina mama ambao wameonyesha uwezo mkubwa kikazi, that hakuna mtu yoyote atakayesema kuwa ni hawara ya kiongozi NO!

Now on the other side of the coin, ni yale yale ya viongozi wetu wabovu, wameitumia kuimarisha utetezi wao bungeni, that is wrong! Wameitumia kuwarubuni viongozi wa upinzani kujitoa vyama vyao that is wrong!

Kwenda mahakamani against hii sheria, good luck kwani utapambana na CCM na Upinzani pia, Je mahakama zetu zina uwezo kisheria kutengua sheria zilizopitishwa na bunge la Jamhuri?? Nafikiri mzee mugyyi unahitaji research ya nguvu!
 
Mzee Es,

Nadhani Mzee Muggy ana point hapo, hebu soma katikati ya mistari, hilo la wataalamu hata mimi naunga mkono. Ni lazima Rais apewe nafasi ya upendeleo ili apate wataalamu.

Ila hili la viti maalum kutoka vijana, wakina mama, wasomi, wazazi, vilema..etc naona ni kutumia vibaya pesa za walipa kodi, kama ni hivyo basi kama alivyosema Mzee Muggy itabidi kuwe na wawakilishi wa kila kundi, bunge itaishia kuwa na wabunge 1000!!

Naomba mnisaidie mimi huwa fikira zangu naziona ni DUNI sana hata kuelewa nachelewa mnooo! Mzee Es ni mbunge gani wa upinzani ktk bunge la serikali ya jamhuri ya Tanzania aliyeteuliwa na rais katika nafasi zake za upendeleo?

FD
 
Suala zima la wabunge wa kuteuliwa halina msingi wowote wa kidemokrasia na halina uhalali wowote wa kimantiki! Ni masalio ya utamaduni na siasa ya kikoloni. Tangu zamani, wafalme au watawala wa kigeni walikuwa wakiteua watu kuwawakilisha katika maeneo fulani ya kitawala. Watu hao lengo lao kubwa si kutumikia wananchi walio chini yao bali kuhakikisha kuwa maslahi ya Kiongozi Mkuu (Rais, Mfalme, Gavana n.k) yanalindwa.

Lengo kubwa la utaratibu huu ni chama tawala kuwa na kura za ziada kutokana na wabunge wanaopatikana kwa kuteuliwa au kuingia kutokana na hali fulani fulani. Hakuna sababu ya watu kuingia kwenye Baraza la Kutunga Sheria bila ya kuchaguliwa na wananchi. Period. Tunauwezo wa kufikiri na kuona ni jinsi gani makundi hayo yanaweza kuwakilishwa. Zaidi ya yote utaratibu huu wa Rais kuteua wabunge kama unavyofanyika hivi sasa, unaendeleza hisani na shukurani. Unatolewa kama zawadi na fadhila.

Haya ni mapendekezo yangu.
a. Ili kuhakikisha kuwa wanawake wanachaguliwa Bungeni, basi utaratibu uwekwe kuhakikisha kuwa Bunge linakuwa 50/50 kwa wabunge wa kuchaguliwa na wananchi.

b. Hakuna sababu ya kuwa na wabunge wa makundi fulani fulani ya Kijamii. Kwanini tuna wabunge wa walemavu, wanawake, vijana. etc Hivi wabunge wa majimbo hawawakilishi watu wa makundi hayo wanaoishi kwenye majimbo yao? Kama kila kundi linaona linastahili kuwa na wabunge, kwanini basi tusiwe na Wabunge wa makabila madogo k.m Wahazebi n.k?

Kama ni kweli tunataka kuendelea nao, miye naona wabunge wote wanaoteuliwa na Rais wasiwe na haki ya kupiga kura. Then that will be fair.
 
Here we are again, bunge letu lina wabunge kama 315 kati yao hao 90% ni wa CCM, je rais wa CCM anahitaji wabunge kumi kupitisha mambo yake?

Tanzania tumeamua kwa kupitisha sheria kuwa mawaziri watakuwa wabunge tu, hapa kweli tumepoteza viongozi wengi shupavu wa taifa ambao hawana uwezo wa kutumia shillingi millioni 300, kupata ubunge!

Is it ok jinsi hii sheria inavyokuwa manipulated na marais wa CCM na kuwaingiza kina Kingunge, ili wakawa-bully wabunge wa CCM bungeni? Hell NO! sikubaliani kabisaaa, je dawa ni kuifuta? hapana kwa sababu kesho Tanzania tunaweza kupata rais mstaarabu ambaye ataitumia kama ilivyokusudiwa kwa faida ya taifa letu,

Je tutabadili sheria ngapi, maana ukianza na moja ni lazima upitie zote which leads to a bigger picture and question hapa, Je Tanzania kuna umuhimu wa ku-reform katiba yetu? We can debate about that!

Kuwakilishwa bungeni 50/50, kati ya wanaume na wanawake, mimi sikubaliani kabisa na hiyo hoja ya ku-mandate uwakilishwaji, kwani tukianza hapo baadaye tutahitaji ku-mandate kila sector NO! we do not need that! Kilakitu kwenye maisha kinakuja na wakati wake, kama leo hatuna wanawake wengi bungeni ina maana wakati bado haujafika!

Na kwa mzee FD, toka hiyo sheria ipitishwe marais wa CCM wamekuwa wakiwachagua wapinzani waliolala ndio maana hujawasikia, mara mwisho alikuwa ni mzanzibari kwa jina la Rashid siui kama umewahi kumsikia, isipokuwa safari hii rais amechagua wabunge 7 so far hajamaliza na wote ni CCM!
 
Heshima mbele wakuu.....

Nimekuwa nikijiuliza kuhusu waBunge wa kuteuliwa na raisi huwa inatumika vigezo gani?? Lakini nimeshindwa sababu ukiangalia the personalities kwa kweli zinapishana sana....

Hebu bofya hapo uone waBunge wetu walioteuliwa na Mtukufu Rais!!

http://www.parliament.go.tz/bunge/MP_Comp.asp?fpkey=APP

Naomba wanaJambo wenzangu mnisaidie kama kuna mtu ameweza kupata trend ys uteuzi huu wa waBunge wetu manake inakuwa kaazi kweli kweli!!
 
Hakuna Kigezo chochote isipokuwa kile kinachompa sifa ya kuweza kuchaguliwa ubunge pia. Mtanzania, miaka 18, akili timamu na asiyewahi kufungwa zaidi ya miezi mitatu kwa kosa la kihalifu. Vingine ni uamuzi tu wa Rais.
 
Mbona hajamchagua Lunyungu ? No ni ushikaji unatumika nanadhani we should get rid of this wabunge wa kuteuliwa ni mzigo kwa Taifa linalo liwa kila siku kwa kasi .
 
hivi bunge limeanza au bado,au litaanza lini maana ni kimya tu,tupeni nyepesi nyepesi kama zipo na tarehe ya kuanza vikao vya bunge
 
Mbona hajamchagua Lunyungu ? No ni ushikaji unatumika nanadhani we should get rid of this wabunge wa kuteuliwa ni mzigo kwa Taifa linalo liwa kila siku kwa kasi .

Lunyungu,

Wabunge kumi naona sio wengi. Hii inaweza kumpa rais nafasi ya kuteua watu wachache ambao anaona anawahitaji ili kumsaidia kazi.

Labda tu tuombe iwe kama Kenya ili nafasi zitokane na uwingi wa kura bungeni.

Hakuna kitu kibaya kama kubadili katiba kwasababu tu rais wa CCM hajaitumia vizuri. Hii sheria huenda ni nzuri kwenye ufanisi wa serikali. Unless kuna sababu zingine nyingi kuonyesha huo utaratibu haufai, vinginevyo naona madhara yake sio makubwa.
 
Wabunge hawa ndiyo wanatuletea viongozi mabomu kama kina Kikwete na Meghji (wote waliingia bungeni mara ya kwanza kama wabunge wa kuteuliwa).Watu wote magoigoi wasioweza kushindana katika jukwaa la siasa huwa wanapewa nafasi kwa kuwa wabunge wa kuteuliwa kwanza halafu baada ya miaka mitano au zaidi wanapewa majimbo kushindania.

Ingefaa kuondoa hizi nafasi, sana sana wanazidisha bajeti tu hata maswali wengi wao hawaulizi.
 
Nakubaliana nawe kwamba Wabunge 10 si wengi Mtanzania lakini mtu kama Meghji kiwa waziri wa namna ile na ni wa kuteuliwa inakuwa balaa .
 
Nakubaliana nawe kwamba Wabunge 10 si wengi Mtanzania lakini mtu kama Meghji kiwa waziri wa namna ile na ni wa kuteuliwa inakuwa balaa .

Lunyungu,

Nakubaliana na wewe kwamba kwa jinsi hizo nafasi zinavyotumika sasa, kweli hata mimi nashawishika kusema ziondolewe, maana serikali ni kama wana abuse hiyo sheria. Wanatoa hizo nafasi kwa watu ambao either wameshindwa kwa wananchi au hawana uwezo wa maana.

Lakini pia naona lengo lake ni zuri ila linategemea tuna rais gani, hizo nafasi zingetumika ku promote watu wapya ambao wana uwezo lakini labda bado hawana mizizi ya kutosha, hasa kwa wale ambao wanaweza kuwa mawaziri wazuri.

Meghji ana uwezo wa kugombea ubunge kama anataka kuwa mwanasiasa lakini akaamua kutokugombea, sasa kumpa hiyo nafasi nafikiri ni makosa. Hivyo hivyo kwa Kingunge na hata Mwang'onda ambaye alishindwa kule Mbeya.
 
mbunge ama wabunge ni wawakilishi wa wananchi. Sasa hawa wabunge wa kuteuliwa wanamwakilisha nani?.

Kwanini walipwe mshahara na malupulupu mengine na sisi wakati si wawakilishi wetu?. Huu ni mzigo tunaobebeshwa bila ya kujitakia. Mambo kama haya ndiyo yanafaa tuyapigie kelele na yabadilishwe mara moja.
 
Nilikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kupendekeza kuwa CCM imzawadie Ubunge Bw. Makamba nikiamini kuwa ndugu yetu huyo atakuwa ni mtetezi wa wananchi kama alivyofanya miaka ile ya Ukuu wa Wilaya na hatimaye ukuu wa mkoa. Niliamini kuwa ni mtu ambaye hamuonei haya mtu yeyote. Hivyo, wakati Rais Kikwete anamteua kuwa Mbunge niliamini kabisa kuwa ulikuwa ni uamuzi sahihi kwa sababu nilitarajia mchango mkubwa wa mheshimiwa huyo.

Hata hivyo, naomba nikiri kuwa nilikosea. Nilichokigundua ni kuwa Mhe. Makamba ameweka Ukatibu Mkuu mbele na Ubunge wake pembeni kiasi kwamba sikumbuki mara ya mwisho lini alihudhuria mkutano wa Bunge, lini alitoa mawazo Bungeni, na ni lini alifanya kazi kama Mbunge na si Katibu wa Chama. Ninafahamu amekuwapo Bungeni hususan wakati wa sakata la kina Lowassa lakini alitumia cheo chake cha Ukatibu Mkuu zaidi kuliko nafasi yake kama Mbunge.

552.jpg


Pichani Mhe. Makamba siku ya pili baada ya kuapishwa kuwa Mbunge

Je kuna faida gani mtu kuteuliwa kuwa Mbunge halafu huchangii Bungeni? Kuna faida gani kuwa mtunga sheria wakati wenzako wako kwenye mkutano wa Bunge wewe unakesha kupiga kampeni na kuliacha Bunge? Je, kuna ulazima bado wa kuwa na wabunge wa kuteuliwa kama kina Makamba? na kwa wale waliokuwa Bungeni ni kitu gani ambacho Makamba amekisema Bungeni kinachoonesha yeye ni mwakilishi wa watu? swali gani aliuliza au hoja gani alichangia?
 
Nilikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kupendekeza kuwa CCM imzawadie Ubunge Bw. Makamba nikiamini kuwa ndugu yetu huyo atakuwa ni mtetezi wa wananchi kama alivyofanya miaka ile ya Ukuu wa Wilaya na hatimaye ukuu wa mkoa. Niliamini kuwa ni mtu ambaye hamuonei haya mtu yeyote. Hivyo, wakati Rais Kikwete anamteua kuwa Mbunge niliamini kabisa kuwa ulikuwa ni uamuzi sahihi kwa sababu nilitarajia mchango mkubwa wa mheshimiwa huyo.

Hata hivyo, naomba nikiri kuwa nilikosea. Nilichokigundua ni kuwa Mhe. Makamba ameweka Ukatibu Mkuu mbele na Ubunge wake pembeni kiasi kwamba sikumbuki mara ya mwisho lini alihudhuria mkutano wa Bunge, lini alitoa mawazo Bungeni, na ni lini alifanya kazi kama Mbunge na si Katibu wa Chama. Ninafahamu amekuwapo Bungeni hususan wakati wa sakata la kina Lowassa lakini alitumia cheo chake cha Ukatibu Mkuu zaidi kuliko nafasi yake kama Mbunge.

552.jpg


Pichani Mhe. Makamba siku ya pili baada ya kuapishwa kuwa Mbunge

Je kuna faida gani mtu kuteuliwa kuwa Mbunge halafu huchangii Bungeni? Kuna faida gani kuwa mtunga sheria wakati wenzako wako kwenye mkutano wa Bunge wewe unakesha kupiga kampeni na kuliacha Bunge? Je, kuna ulazima bado wa kuwa na wabunge wa kuteuliwa kama kina Makamba? na kwa wale waliokuwa Bungeni ni kitu gani ambacho Makamba amekisema Bungeni kinachoonesha yeye ni mwakilishi wa watu? swali gani aliuliza au hoja gani alichangia?

Ahsante sana kwa hili, nafikiri itakuwa vizuri kuanzia kikao cha bunge kinachokuja, JF ikaweka kumbukumbu za Wabunge wote wa CCM na upinzani ambao wanaingia bungeni kuchapa usingizi tu bila mchango wowote. Hii itasaidia kuwafunua macho wapiga kura katika uchaguzi wa 2010. Hatuihitaji wabunge ambao hawachangii lolote Bungeni bali husubiri wakati wa kampeni za uchaguzi ili waanze kugawa pilau, pesa na pombe ili wachaguliwe tena.
 
Kiranja wa Bunge ni nani hasa? au hiyo ni nafasi tupu... naona kuna mtu ameamua kuitafuta kazi hiyo...
 
Mzee Kingunge alipewa Ubunge wa kuteuliwa ili apewe Uwaziri. Na ndivyo ilivyokuwa kwa Zakia Meghji. Sasa wote si Mawaziri tena, wamebaki kuwa wabunge wa kuteuliwa. Wanatusaidia nini bungeni sasa?

Wanamwakilisha nani? Je Rais anazo nguvu za Kikatiba za kutengua uteuzi wao?

Kwa mtazamo wangu, lengo la kuweka nafasi 10 za wabunge wa kuteuliwa na Rais lilikuwa zuri sana. Hii ni kwa sababu Rais anaweza kuona kuna watu wanaofaa sana katika baraza lake la Mawaziri ambao sio wabunge, akawateua na kisha kuwafanya Mawaziri.

Kwa bahati mbaya sana, naona kama vile inatumika vibaya kwa kuteua watu wa minaajili ya kuwalipa fadhila badala ya kuteua watu kutokana na ubora wa utendaji wao wa kazi. Kuna wasomi wengi wanaoweza kuongeza Wizara nyeti za serikali yetu lakini hawataki kugombea ubunge kwa sababu zinazofahamika, rushwa, majungu na kadhalika. Hao ndio walistahili hizo nafasi ili wamsaidie Rais.
 
Back
Top Bottom