Matatizo ya VodaCom

Idimi

JF-Expert Member
Mar 18, 2007
14,888
10,371
Samahani wana JF, nimekuwa nikipata sana shida kupiga simu katika mtandao wa Vodacom nyumbani (niko nje ya nchi), sijajua shida iko wapi! Kuna wakati huwa nikipiga simu inaita kama kawaida ila huwa haipokewi na nikituma ujumbe mtu niliyekuwa nikimpigia anasema simu haijaita wala nini, sasa hii huwa inanipa wakati mgumu sana! Mara nyingine huwa nikipiga, simu inakuwa inatafuta line muda wote tu bila majibu, sasa huwa nakereka sana! Nikituma Ujumbe unaenda kama kawaida! Nilidhani ni mtu mmoja tu mwenye shida hii, lakini nikaja kugundua kuwa ni line zote za vodacom zina shida ya namna hii nikipiga toka huku nje niliko. Kama kuna maelezo yoyote ya kutatua kadhia hii kutoka kwa wahusika (Vodacom) nitafurahi sana. Nilishakutana na mtu akilalamikia shida ya namna hii katika blogu fulani maarufu! Naomba kusaidiwa shida hii!
 
It happen to me often. But not only vodacom, even celtel and tigo.
Sometimes when i make call, before the other hand receive it, connection is terminated at the same time they charge it as if the call was successful
 
Sasa Hivi Hapa Kuna Tatizo La Celtel Ukiingiza Vocha Za Simu Hazifanyi Kazi Ukipiga Simu Celtel Huduma Kwa Wateja Hakuna Jibu Lolote Unalopata Yaani Kama Vile Hawahusiki Na Tatizo Hili
 
Sasa Hivi Hapa Kuna Tatizo La Celtel Ukiingiza Vocha Za Simu Hazifanyi Kazi Ukipiga Simu Celtel Huduma Kwa Wateja Hakuna Jibu Lolote Unalopata Yaani Kama Vile Hawahusiki Na Tatizo Hili
Vodacom=Celtel??
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom