Matatizo ya Maradhi na magonjwa ya kawaida

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,315
33,111
Matatizo na magonjwa ya kawaida

Katika sehemu hii, utajifunza kuhusu magonjwa na matatizo ya kawaida ya meno. Baadhi iya matatizo haya huenda yatakuathiri hata kama unatunza meno yako vizuri. Ingawa unaweza ukayazuia baadhi kwa kusugua meno na kuondoa chakula iliyokwama kwenye meno kwa kutumia uzi spesheli mara mbili kwa siku; kumwona daktari wa meno mara kwa mara, kutovuta sigara na kula vizuri

Alama ya uchafu/madoadoa kwenye meno

Tumbaku, baadhi ya vyakula na vinyaji vyaweza kufanya meno yetu kuwa na alama ya uchafu na madoadoa kadri tunavyozidi kuzeeka. Alama hizi za uchafu au madoadoa hayasabibishi tatizo lolote la afya. Lakini watu wengi wanatamani kuwa na meno meupe.

Ni nini husababisha alama za uchafu au madoadoa kwenye meno
Baadhi ya vitu vinavyosababisha hali hii ni pamoja na:

  • Uvutaji wa sigara au biri na kutafuna tumbaku. Matumizi ya aina yoyote ya tumbaku yanaweza kuleta ugonjwa wa kansa, ikiwemo kansa ya kinywa. Uchungu ukizidi kwa muda wa siku mbili na zaidi, muone daktari wa meno, labda una jino lililovunjika
  • Vinyaji kama vile chai, kahawa, mkola na mvinyo wenye rangi nyekundu husababisha kuwepo na madoadoa kwenye meno. Chai na mvinyo nyekundu ni nzuri au bora kwa afya yako, lakini hakikisha kuwa umesugua meno baada ya kuvinywa.
  • Matunda kama vile beriberi ni nzuri pia, lakini huchafua meno. Sugua meno yako baada ya kuyala.

Unatibu vipi?
Ikiwa meno yako yana madoadoa au uchaafu, jaribu dawa ya meno itakayofanya yawe meupe. Unaweza kwenda kwa daktari wa meno akaya pausha ingawa ni bei ghali sana. Dawa ya meno husaidia sana ingawa hufanya kazi polepole.

Mashimo

Mashimo ni nini?

Mashimo ni uwazi ulio kwenye meno yako na hutokana na meno kuoza. Ingawa ni rahisi sana kuzuia mashimo, ni watu wengi huwa na mashimo. Daktari wako wa meno anaweza akakutibu mapengo ila ni vyema sana kuyatibu kabla hayajazidi au kuwa makubwa au kusabisha maumivu ya meno, ufizi kufura au uchungu wowote ule.

Njia zitakazokuwezesha kuzuia mashimo:

  • Sugua meno yako, kisha uondoe chakula iliyo kwenye meno kwa kutumia uzi spesheli na umuone daktari wa meno mara kwa mara
  • Usile peremende kwa wingi na vyakula vitamu au vinywaji vingi vilivyo baridi na vinywaji vitamu. Jizoeshe kunywa kinywaji kimoja baridi kwa siku au peremende kidogo.
  • Kula matunda na mboga (itakayosafisha meno yako) ama jibini na mtindi (ambazo ni nzuri kwa meno na ufizi wako) kama kumbwe
  • Ili kutengeneza mate, tafuna sandarusi isiyo na sukari baada ya vyakula. Mate huwa na kemikali inayozuia meno kuoza.
  • Hakikisha kuwa unatumia dawa ya meno iliyo na floraidi. Floraidi hufanya meno yako kuwa na nguvu.
  • Dalili au ishara huwa zipi
  • Ukiona doa nyeusi au hudhurungi (kahawia) kwenye meno au wasikia maumivu ya meno ambayo haishi muone daktari wa meno haraka iwezekanavyo. Usipoende kupata matibabu ya meno, uozo uliopo kwenye meno huenda ikasababisha matatizo mengine kama vile kufura kwa ufizi, maumivu kwenye taya na kichwa kuuma.
  • Unatibu vipi?
  • Safisha/sugua meno yako vizuri, kula vyakula bora na upate uchunguzi wa meno mara kwa mara ili kuzuia matatizo haya.

Picha za baadhi ya maradhi ya meno
phototake_rm_photo_of_tooth_illustration.jpg
Tooth Enamel

whitmore_rm_photo_of_teeth_damaged_by_bruxism.jpg
Bruxism: Effects of Teeth Grinding


mckay_rf_photo_of_overview_of_bulimic_teeth.jpg
Bulimia: Impact on Oral Health


mckay_rm_photo_of_bulima_teeth.jpg
Teeth Damaged by Bulimia
 
Maumivu ya meno

Je, maumivu ya meno ni nini?Jino likikuuma, hali hii hutokana na uchungu uliopo kwenye taya ya jino au meno mbili. Uchungu wa meno husababishwa na kitu kukwama katikati ya meno, pengo ama jino linalomea au lililovunjika kutokana na kuuma vitu vigumu sana.

Unaitibu vipi?

  • Suuza kinywa chako na maji vuguvugu kisha tumia uzi spesheli kuondoa chakula kilichokwama katikati ya meno. Ukiwa hauwezi kukiondoa kwa kutumia uzi spesheli, nenda ukamwone daktari wa meno.
  • Meza dawa za kupunguza uchungu
  • Tia barafu kwenye taulo kisha weka kwenye shavu lako kwa muda mfupi. Ikiwa shavu lako limefura; jaribu kutumia njegeve. Itakalibu uso wako kwa urahisi.
  • Uchungu ukiendelea baada ya siku mbili, muone daktari. Yaenda una shimo au jino limevunjika.

Meno iliyong’oka

Ukianguka au ugongwe kwenye mdomo kisha meno yako ing’oke, waweza ukarekebisha hali hii ukishughulikia haraka iwezekanavyo. Tunza jino hilo na uende kwa daktari wako wa meno ama chumba cha dharura haraka iwezekanavyo.

Fanya yafuatayo ikiwa jino lako limeng’oka au limelegea

  • Hakikisha kuwa u mzima. Ikiwa hauna fahamu ama una majeraha mabaya mtume mtu yeyote aitishe gari la wagonjwa
  • Ikiwa jino lako halijang’oka kabisa, linalegea tu, wacha mahali hapo ilipo kisha umwone daktari wa meno
  • Ikiwa jino lako limeng’oka kabisa, shikilia na enameli. Kumbuka kwamba haipaswi kushika mizizi iliyo kwenye ufizi
  • Suuza meno yako na maji. Usisugue
  • Jaribu kulitia polepole jino hilo katika shimo. Ikiwa halingii kwa urahisi, weka chini ya ulimi au katikati ya ufizi na shavu. Ikiwa utameza basi litie kwenye glasi ya maziwa, usiliwache likauke
  • Weka shashi au pamba kwenye shimo ikiwa latoa damu kisha shikilia na meno ya juu au chini
  • Nenda kwa daktari wa meno au chumba cha dharura haraka iwezekanavyo



​
Meno matego/isiyonyooka na vifaa vya kukazia meno

Watu wengi huwa na meno yenye matege yaani isionyooka. Wakati mwingine, hali hii huweza kusababisha uchungu wakati ambapo utafura kitu au unapoongea/unapozungumza. Daktari wako anaweza kurekebisha hali hii kwa kuondoa meno iliyosongamana mahali pamoja.
Daktari wako wa meno anaweza kukuelekeza kwa daktari aliye na ujuzi katika kusawazisha meno. Meno yako yaweza kusawazishwa kwa kutumia kifaa maalum cha kukazia meno katika umri wowote ule.
Vifaa hivi vya kukazia meno huwa vya plastiki au metali ambavyo hunatishwa kwenye meno yako na kuunganishwa na waya ambayo inaweza kukazwa. Vifaa hivi husawazisha meno yako polepole. Watu huvaa vifaa hivi kwa muda wa miaka mbili na hugharimu kiasi fulani cha fedha. Zungumza na daktari wako wa meno kuhusu uamuzi wako.


 
Ugonjwa wa ufizi

Ugonjwa wa ufizi huathiri ufizi na huweza kusambaa kwenye mifupa inayoshikilia meno. Hii ni mojawapo ya sababu ambazo hufanya watu kupoteza meno. Ugnjwa huwa katika hatua mbili lakini inapokuathiri waweza kutibu kabla ya kusababisha madhara

Ni nini baadhi ya dalili au ishara
Hatua ya kwanza ya ugonjwa huu wa ufizi huitwa ‘gingivitis’
Baadhi ya dalili/ishara ni pamoja na:

  • Ufizi nyekundu na iliyofura
  • Ufizi unaotoa damu unaposugua meno
  • Ufizi uliong’oka kutoka kwenye meno
  • Harufu mbaya isiyoisha

Wanawake wajawazito kwa kawaida huathiriwa na ‘gingivitis’. Ukiwa mjamzito tunza afya yako ni vizuri ikiwemo meno.

Hatua ya pili ya ugonjwa wa ufizi huwa hatari sana.

Waweza kuwa na ishara/dalili zilizotajwa hapo juu

  • Usaha unaotoka kwenye meno na ufizi
  • Meno iliyolegea
  • Nafasi kubwa katikati ya meno mahali ambapo ufizi inapaswa kuwa
  • Kutokuwepo na tofauti katika mpangilio wa meno ukiyauma chini.

Unaitibu vipi?
Ukiwa na dalili zozote za hatua ya kwanza, sugua meno na utumie uzi spesheli kutoa chakula katika meno mara kwa mara na umuone daktari wa meno. Ukiitibu tatizi hili basi utazuia ugonjwa wa ufizi.

Ukiwa na dalili zozote za hatua ya pili, mwone daktari haraka iwezekanavyo. Meno yako yaweza kung’oka au kung’olewa na daktari wa meno ikiwa hutatibiwa mara moja. Ugonjwa huu ukiwa mbaya sana daktari wako wa meno anaweza kukuelekeza kwa daktari wa meno aliye na ujuzi wa ugonjwa wa ufizi.
 
Back
Top Bottom