Matamshi ya Spika Sitta kuhusu Anna Makinda yaibua maswali magumu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Na Waandishi Wetu
Mwananchi

KITENDO cha Spika wa Bunge Samwel Sitta kumkataza Naibu Spika wake Anna Makinda kusimamia mijadala mizito inayohusu ubadhirifu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na ule wa utata kuhusu tenda iliyotolewa kwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond Development Limited kimeibua maswali kadhaa kutoka kwa baadhi ya wananchi, huku kukiwa na hoja kuwa Spika Sitta huenda ana jambo analolificha.

Sitta jana aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kifungu chochote kinachombana Naibu Spika kusimamia mijadala mizito lakini ni busara tu za ofisi yake kuona mambo makubwa yanabaki kusimamiwa na yeye kwa kuwa ndiye atakayehusishwa na mabaya au mazuri kuhusu mambo yote yanayofanyika Bungeni.

"Mimi ndiye ninayetukanwa kwa kila jambo linalotokea ndani ya Bunge. Hata Rais anapokuwa nje ya nchi Makamu wake hawezi kuamua mtu kunyongwa! Kuna mambo ambayo lazima yanisubiri na sio kama mnavyodhani kuwa kuna mgongano kati yetu," alisema Sitta na kuongeza kuwa;

"Hata muda nitakaokuwa nje bado hauwezi kuathiri hoja hizo kujadiliwa nikiwepo. Kwa taratibu zetu huwa tunaanza na miswada kwanza na bado ipo mingi. Hili jambo naona liko wazi tu na hakuna lolote linalofichwa," alisema.

Mhadhiri kutoka katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu Dar es Salaam Dk Sengondo Mvungi aliliambia gazeti hili kuwa, kilichofichika ndani ya maamuzi hayo ya Sitta huenda ikawa ni maangamizi kwa chama chake kufuatia kuwepo kwa uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiteto.

Dk Mvungi alisema, wakati spika Sitta anarejea kutoka hiyo ziara yake ya Marekani kwanza ndio kampeni zitakuwa zimeshika kasi katika jimbo la Kiteto, hivyo kwa yeye kuruhusu agenda hizo mbili kujadiliwa kipindi hicho ni wazi anakifunga goli chama chake bila kwa kujua ama kutokujua.

"Suala hilo kujadiliwa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Kiteto litatoa mwanya mkubwa wa wapinzani kukimaliza Chama cha Mapinduzi, maana zitatumika takwimu hizo hizo anazozilinda spika kuimaliza CCM kwa wananchi," alisema Dk. Mvungi.
 
"Sitta jana aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kifungu chochote kinachombana Naibu Spika kusimamia mijadala mizito lakini ni busara tu za ofisi yake kuona mambo makubwa yanabaki kusimamiwa na yeye kwa kuwa ndiye atakayehusishwa na mabaya au mazuri kuhusu mambo yote yanayofanyika Bungeni"

Tabia ya Six kuamini na kutumia mara kwa mara utashi na fikra zake binafsi badala ya kanuni na taratibu zinazoliongoza Bunge huwa inanifurahisha kwelix2
 
"Sitta jana aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kifungu chochote kinachombana Naibu Spika kusimamia mijadala mizito lakini ni busara tu za ofisi yake kuona mambo makubwa yanabaki kusimamiwa na yeye kwa kuwa ndiye atakayehusishwa na mabaya au mazuri kuhusu mambo yote yanayofanyika Bungeni"

Tabia ya Six kuamini na kutumia mara kwa mara utashi na fikra zake binafsi badala ya kanuni na taratibu zinazoliongoza Bunge huwa inanifurahisha kwelix2

Inasikitisha kuona "ETI" yeye ndiye mwenye "BUSARA" peke yake. Huku ni kuwadharirisha WATz na hasa wasaidizi wake. Sitta ni binadamu mwenye mapungufu kama binadamu wengine. Watanzania tusikie mahali kuacha bunge liendeshwe kwa "UTASHI" badala ya Kanuni, sheria na taratibu, vinginevyo tunajenga " Dhana ya Udikteta Bungeni" Kuzuia mijadala ya wabunge eti tu kwa sababu anashauriana na Serikali ni mapungufu makubwa ya Katiba yetu.
 
Mugo"The Great";134335 said:
Inasikitisha kuona "ETI" yeye ndiye mwenye "BUSARA" peke yake. Huku ni kuwadharirisha WATz na hasa wasaidizi wake. Sitta ni binadamu mwenye mapungufu kama binadamu wengine. Watanzania tusikie mahali kuacha bunge liendeshwe kwa "UTASHI" badala ya Kanuni, sheria na taratibu, vinginevyo tunajenga " Dhana ya Udikteta Bungeni" Kuzuia mijadala ya wabunge eti tu kwa sababu anashauriana na Serikali ni mapungufu makubwa ya Katiba yetu.

Mugo,
Huyu Six na wabunge wa ccm wanaturejesha kwenye enzi za "Zidumu fikra za six na bunge la mafisadi" Kwa kutopinga, wabunge wanamaanisha kujibu "zimedumu, zinaendela kudumu"

Kweli tunahitaji kufanya mabadiliko. Na haya hayawezi kuanzia ndani ya bunge lisilo na uwakilishi wenye uwiano unaleta upinzani wa kweli kwa maendeleo na wala lisilo na demokrasia ya vitendo. Vile vile hayawezi kuanzia ndani ya serikali ambayo imejaa vizazi vinne vya (Babu, Baba, Mtoto na Mjukuu) ufisadi. Kama alivyokwisha dhihirisha Dr. Slaa, mkakati sahihi ni kupeleka mashtaka kwa Wadanganyika. Tuunge mkono vuguvugu la elimu ya uzalendo na kuwapinga mafisadi kwa vitendo.
 
Where is the rule of law? Mtu mmoja na mawazo yake anaweza kukataza mjadala bungeni? Ina maana hamuamini naibu wake?

Kama huu si mfano wa kulindana na mfumodume ni nini sasa?
 
Lakini hebu. Hivi naibu spika ana kiapo cha utii kwa spika? Anawajibika kwa spika? Analazimika kufuata amri za spika? Kivipi ilhali wote wamechaguliwa na wabunge? Naelewa kuwa rais na makamu wake ni tofauti, kwani hata uchaguzi wao ni tofauti, makamu anachagulika automatically kutoka hatua ya mgombea mwenza pale mgombea urais anaposhinda kiti hicho, na nadhani majukumu yao yamewekwa wazi kikatiba. Sasa huyu Spika anaweza kumuamuru naibu wake kuwa hili lisijadiliwe hadi nirudi? Na je wabunge wakiamua kuleta hoja kwamba hilo suala lijadiliwe wakati Sitta hayupo, akarudi na kukuta bunge limeshatoa uamuzi, anaweza kumchukulia hatua gani naibu wake? Kama kanuni hazimbani naibu kufuata agizo hilo la Spika, nitamshangaa sana kama atalifuata. Nitaelewa kuwa wanashirikiana katika ufisadi, kwa hiyo wanalindana. Shime Mama Makinda, jitoe kwenye kundi hilo, simama katika nafasi yako na utimize wajibu wako uliopewa kikatiba, usitishike na mfa maji anaetapatapa, kama kuna suala la kujadiliwa, alimradi hujavunja kanuni, liweke mezani akirudi akute uamuzi! Asidhani yeye Sitta ndiye bunge! Kama utatii hii amri(batili) ya Sitta, Mama Makinda nitaamini sasa kuwa syndicate ya ufisadi ni kubwa nawe pia umo!
 
Nafikiri kosa hapa liko kwa Spika aliyehodhi madaraka kwa kila kitu ilhali akielewa kwamba ile ni Ofisi na Naibu wake huwa ni Spika yeye anapokuwa hayupo. Hakuna sababu ya kuwa na naibu iwapo anapewa masharti ya kipi ashughulikie na kipi aache. Mimi nafikiri wenye mamlaka ya nani ashughulikie kipi ni wabunge. Kama wao kwa busara zao wataona kwamba hoja fulani inahitaji kuwepo kwa substantive speaker watasema na kuomba kusitishwa kwa mjadala. Mimi nafikiri alichofanya spika ni kumdhalilisha naibu na utashi na uwezo wake na hata kudhalilisha busara za wabunge kumchagua huyu mama kuwa Naibu wa Spika. kwa ujumla hii ni ile hulka yake ya kuwafanye wengine ni watoto na hawajui chochote isipokuwa yeye.
 
Nafikiri kosa hapa liko kwa Spika aliyehodhi madaraka kwa kila kitu ilhali akielewa kwamba ile ni Ofisi na Naibu wake huwa ni Spika yeye anapokuwa hayupo. Hakuna sababu ya kuwa na naibu iwapo anapewa masharti ya kipi ashughulikie na kipi aache. Mimi nafikiri wenye mamlaka ya nani ashughulikie kipi ni wabunge. Kama wao kwa busara zao wataona kwamba hoja fulani inahitaji kuwepo kwa substantive speaker watasema na kuomba kusitishwa kwa mjadala. Mimi nafikiri alichofanya spika ni kumdhalilisha naibu na utashi na uwezo wake na hata kudhalilisha busara za wabunge kumchagua huyu mama kuwa Naibu wa Spika. kwa ujumla hii ni ile hulka yake ya kuwafanye wengine ni watoto na hawajui chochote isipokuwa yeye.
Very well said Mbopo sina la kuongeza.
Lakini swali hapa . How do we break the jinx ?
 
Hizi ndio dizaini za "MABABA" ambao wakisafiri nyumbani hakuna kula nyama mpaka "BABA" arudi. This is so selfish..

This is unbelievable!!!! Is he the wisest person in the country? What if he dies tonight... Inamaanisha ndio utakua ndio mwisho wa bunge? This is so primitive!!!

A wise President would get rid of leaders of his mentality..
 
Posted Date::2/2/2008
Matamshi ya Spika Sitta kuhusu Anna Makinda yaibua maswali magumu
Na Waandishi Wetu
Mwananchi

KITENDO cha Spika wa Bunge Samwel Sitta kumkataza Naibu Spika wake Anna Makinda kusimamia mijadala mizito inayohusu ubadhirifu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na ule wa utata kuhusu tenda iliyotolewa kwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond Development Limited kimeibua maswali kadhaa kutoka kwa baadhi ya wananchi, huku kukiwa na hoja kuwa Spika Sitta huenda ana jambo analolificha.

Sitta jana aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kifungu chochote kinachombana Naibu Spika kusimamia mijadala mizito lakini ni busara tu za ofisi yake kuona mambo makubwa yanabaki kusimamiwa na yeye kwa kuwa ndiye atakayehusishwa na mabaya au mazuri kuhusu mambo yote yanayofanyika Bungeni.

"Mimi ndiye ninayetukanwa kwa kila jambo linalotokea ndani ya Bunge. Hata Rais anapokuwa nje ya nchi Makamu wake hawezi kuamua mtu kunyongwa! Kuna mambo ambayo lazima yanisubiri na sio kama mnavyodhani kuwa kuna mgongano kati yetu," alisema Sitta na kuongeza kuwa;

"Hata muda nitakaokuwa nje bado hauwezi kuathiri hoja hizo kujadiliwa nikiwepo. Kwa taratibu zetu huwa tunaanza na miswada kwanza na bado ipo mingi. Hili jambo naona liko wazi tu na hakuna lolote linalofichwa," alisema.

Mhadhiri kutoka katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu Dar es Salaam Dk Sengondo Mvungi aliliambia gazeti hili kuwa, kilichofichika ndani ya maamuzi hayo ya Sitta huenda ikawa ni maangamizi kwa chama chake kufuatia kuwepo kwa uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiteto.

Dk Mvungi alisema, wakati spika Sitta anarejea kutoka hiyo ziara yake ya Marekani kwanza ndio kampeni zitakuwa zimeshika kasi katika jimbo la Kiteto, hivyo kwa yeye kuruhusu agenda hizo mbili kujadiliwa kipindi hicho ni wazi anakifunga goli chama chake bila kwa kujua ama kutokujua.

Suala hilo kujadiliwa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Kiteto litatoa mwanya mkubwa wa wapinzani kukimaliza Chama cha Mapinduzi, maana zitatumika takwimu hizo hizo anazozilinda spika kuimaliza CCM kwa wananchi,� alisema Dk. Mvungi.

Hii thread na mengine mengi yatakayowekwa hapa JF muda mfupi ujao ndiyo yamepelekea Spika kuahirisha safari yake. Hongera JF, wenye wivu wakome sasa na kujinyonga kwani the game ndio tu sasa imeanza.
 
Spika Sitta ambaye anaondoka leo kwenda Marekani, alimkataza Naibu Spika, Anna Makinda kuruhusu mjadala unaohusu BoT na Richmond mpaka atakaporudi Alhamisi wiki hii kwa kuwa ni masuala nyeti ambayo lazima yajadiliwe akiwepo.

Hii inaonyesha dharau kubwa ya spika kwa Anna Makinda yaani kifupi ina maana huyu mama hana uwezo wa deal na issue nzito pamoja na kwamba ni naibu wake..Damn!
 
Posted Date::2/2/2008
Matamshi ya Spika Sitta kuhusu Anna Makinda yaibua maswali magumu
Na Waandishi Wetu
Mwananchi

KITENDO cha Spika wa Bunge Samwel Sitta kumkataza Naibu Spika wake Anna Makinda kusimamia mijadala mizito inayohusu ubadhirifu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na ule wa utata kuhusu tenda iliyotolewa kwa kampuni ya kufua umeme ya Richmond Development Limited kimeibua maswali kadhaa kutoka kwa baadhi ya wananchi, huku kukiwa na hoja kuwa Spika Sitta huenda ana jambo analolificha.

Sitta jana aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kifungu chochote kinachombana Naibu Spika kusimamia mijadala mizito lakini ni busara tu za ofisi yake kuona mambo makubwa yanabaki kusimamiwa na yeye kwa kuwa ndiye atakayehusishwa na mabaya au mazuri kuhusu mambo yote yanayofanyika Bungeni.

"Mimi ndiye ninayetukanwa kwa kila jambo linalotokea ndani ya Bunge. Hata Rais anapokuwa nje ya nchi Makamu wake hawezi kuamua mtu kunyongwa! Kuna mambo ambayo lazima yanisubiri na sio kama mnavyodhani kuwa kuna mgongano kati yetu," alisema Sitta na kuongeza kuwa;
"Hata muda nitakaokuwa nje bado hauwezi kuathiri hoja hizo kujadiliwa nikiwepo. Kwa taratibu zetu huwa tunaanza na miswada kwanza na bado ipo mingi. Hili jambo naona liko wazi tu na hakuna lolote linalofichwa," alisema.

Mhadhiri kutoka katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu Dar es Salaam Dk Sengondo Mvungi aliliambia gazeti hili kuwa, kilichofichika ndani ya maamuzi hayo ya Sitta huenda ikawa ni maangamizi kwa chama chake kufuatia kuwepo kwa uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiteto.

Dk Mvungi alisema, wakati spika Sitta anarejea kutoka hiyo ziara yake ya Marekani kwanza ndio kampeni zitakuwa zimeshika kasi katika jimbo la Kiteto, hivyo kwa yeye kuruhusu agenda hizo mbili kujadiliwa kipindi hicho ni wazi anakifunga goli chama chake bila kwa kujua ama kutokujua.

Suala hilo kujadiliwa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Kiteto litatoa mwanya mkubwa wa wapinzani kukimaliza Chama cha Mapinduzi, maana zitatumika takwimu hizo hizo anazozilinda spika kuimaliza CCM kwa wananchi,� alisema Dk. Mvungi.

Hii ni hoja dhaifu sana kwa mtu aliyekwenda shule. Aliwahi kudai Zitto ni mwanasiasa mabaye hajakomaa,kwa mtazamo wangu hii nafasi ya Spika haimfai kabisa Sitta kutokana na kushindwa kuwa na msimamo ndani ya mbunge na mbunge kupoteza heshima yake. Sitta ovyooooooooooooooooooooooooo
 
Shukurani,
Kweli bob huyu Sitta naona mpuuzi kweli kweli maanake katumia mifano ya hukumu ya mtu kunyongwa kama vile kuna mtu Bungeni anatafuta sahihi yake kumnyonga mhusika ambaye tayari hukumu imesha pita.

Alichoshindwa kuelewa ni kwamba Mhalifu yeyote hupitia mahakama kwanza kabla ya hiyo sahihi ya rais ambayo hutakiwa baada ya hukumu ya korti... Sii rais anayetoa hukumu ya kifo cha mhalifu.

Sasa swala hili halijapata kufikishwa korti na hakuna sheria inayosema Bunge haliwezi kuzungumzia baadhi ya maswala bila spika mteuliwa...
 
Huyu Six anaonekana hajui maana ya kudelegate na isitoshe Anne ni Naibu Spika cheo kinachompa uwezo wa kutenda kazi za spika bila matatizo yoyote.

Mimi nadhani kila kitu kinachofanyiwa maamuzi bungeni ni sensitive sasa kama kuna classes za issues then huyu jamaa ana matatizo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom