Matamko ya Polepole yanawahusu watia nia wasiokuwa na fedha na vyeo kuhusu kuanza kampeni mapema na rushwa

Ngorika Nangomwa

New Member
May 28, 2020
2
0
Nimemsikiliza ndugu Polepole mara kadhaa kuhusu watia nia kuanza kampeni maapema pamoja na kutoa rushwa. Niseme hili ni zuri sana ila linawahusu hawa watia nia wasiokuwa na fedha. Kwa mfano juzi nilikuwa mkoa wa Ruvuma watia nia matajiri wanazunguka kuhonga bila woga Ruvuma na wale wenye vyeo vya ukurugenzi na udc nk. Hawaogopi na nilipouliza wenyeji wanasema jamaa wanatoa saana na hakuna anayeshughulika nao hili tayari changamoto kwa chama

Pia nilivyoenda Tunduru nimekutana na hali hiyo wenye pesa wanazunguka hakuna chombo chochote kinachochukua hatua yaani kimsingi kama huna fedha au madaraka basi vyombo utakutana navyo tu.

Mtwara ndio usiseme wanazurula hovyo watia nia wale matajiri yaani huko ndio utasema serikali jamaa wameitia mfukoni, niliuliza sehemu moja mtia nia anagawa sukari hapo Mtwara wengine wanagawa sementi wengine fedha yaani mkoa wa Mtwara vurugu ndio zimekuwa nyingi sasa.

Jana asbh nimeingia mjini kwangu hapa Dar waungwana hapa ni zaidi ya sehemu zote nimebaki kujiuliza hivi haya matamko ya Polepole hawayasikii au viburi vimewajaa tena huku wanatishiwa kabisa vijana waliotia nia na wenye fedha.

Wiki kadha zilizopita kule Tanga nako ilikuwa hatari mno wanagawa sana fedha kwa ufupi mchakato wa kura za maoni washindi watakuwa wenye fedha na umaarufu na wale wenye vyeo sasa hivi ma-RC,ma-DC na ma-DED wachache saana hawa wasio na kitu watakaotoboa kutokana na uhalisia wa siasa za Tanzania.

Nimwombe ndugu Polepole watumieni vizuri watu wa vyombo hali ni mbaya sana Rais ana nia nzuri na chama ila mikoani huko balaa tupu hata hivyo vyombo vinanunulika huko ni marafiki zao matajiri na wenye vyeo.
 
Mataga kuna hatari sana Safari hii kama wnanchi wamemkataa Spika sijui hali itakuaje, vita kubwa nikati ya mataga kwa mataga.
 
Nimemsikiliza ndugu Polepole mara kadhaa kuhusu watia nia kuanza kampeni maapema pamoja na kutoa rushwa. Niseme hili ni zuri sana ila linawahusu hawa watia nia wasiokuwa na fedha. Kwa mfano juzi nilikuwa mkoa wa Ruvuma watia nia matajiri wanazunguka kuhonga bila woga Ruvuma na wale wenye vyeo vya ukurugenzi na udc nk. Hawaogopi na nilipouliza wenyeji wanasema jamaa wanatoa saana na hakuna anayeshughulika nao hili tayari changamoto kwa chama

Pia nilivyoenda Tunduru nimekutana na hali hiyo wenye pesa wanazunguka hakuna chombo chochote kinachochukua hatua yaani kimsingi kama huna fedha au madaraka basi vyombo utakutana navyo tu.

Mtwara ndio usiseme wanazurula hovyo watia nia wale matajiri yaani huko ndio utasema serikali jamaa wameitia mfukoni, niliuliza sehemu moja mtia nia anagawa sukari hapo Mtwara wengine wanagawa sementi wengine fedha yaani mkoa wa Mtwara vurugu ndio zimekuwa nyingi sasa.

Jana asbh nimeingia mjini kwangu hapa Dar waungwana hapa ni zaidi ya sehemu zote nimebaki kujiuliza hivi haya matamko ya Polepole hawayasikii au viburi vimewajaa tena huku wanatishiwa kabisa vijana waliotia nia na wenye fedha.

Wiki kadha zilizopita kule Tanga nako ilikuwa hatari mno wanagawa sana fedha kwa ufupi mchakato wa kura za maoni washindi watakuwa wenye fedha na umaarufu na wale wenye vyeo sasa hivi ma-RC,ma-DC na ma-DED wachache saana hawa wasio na kitu watakaotoboa kutokana na uhalisia wa siasa za Tanzania.

Nimwombe ndugu Polepole watumieni vizuri watu wa vyombo hali ni mbaya sana Rais ana nia nzuri na chama ila mikoani huko balaa tupu hata hivyo vyombo vinanunulika huko ni marafiki zao matajiri na wenye vyeo.
Ushahidi wa madai hayo ni muhimu sana kuhalalisha usemacho,vinginevyo ni porojo tu.
Hata hivyo nikutoe shaka wote wanaojipitisha na kutoa hongo au kujinadi chama kipo makini sana na wasishangae wanaowapa hongo ndio wakusanya ushahidi kuja kuwamaliza wahongaji majimboni ,chama kimejipanga haswa
 
Cha kushangaza hayo madudu PCCB Wanayaona lakini hawasemi chochote kwaajili ya kutunza heshima ya mamlaka ya uteuzi. Lakini wanahangaika na CDM ambayo ina hati safi ya CAG, na hizi double standards ndyo znazoliangamiza taifa letu
 
Nimemsikiliza ndugu Polepole mara kadhaa kuhusu watia nia kuanza kampeni maapema pamoja na kutoa rushwa. Niseme hili ni zuri sana ila linawahusu hawa watia nia wasiokuwa na fedha. Kwa mfano juzi nilikuwa mkoa wa Ruvuma watia nia matajiri wanazunguka kuhonga bila woga Ruvuma na wale wenye vyeo vya ukurugenzi na udc nk. Hawaogopi na nilipouliza wenyeji wanasema jamaa wanatoa saana na hakuna anayeshughulika nao hili tayari changamoto kwa chama

Pia nilivyoenda Tunduru nimekutana na hali hiyo wenye pesa wanazunguka hakuna chombo chochote kinachochukua hatua yaani kimsingi kama huna fedha au madaraka basi vyombo utakutana navyo tu.

Mtwara ndio usiseme wanazurula hovyo watia nia wale matajiri yaani huko ndio utasema serikali jamaa wameitia mfukoni, niliuliza sehemu moja mtia nia anagawa sukari hapo Mtwara wengine wanagawa sementi wengine fedha yaani mkoa wa Mtwara vurugu ndio zimekuwa nyingi sasa.

Jana asbh nimeingia mjini kwangu hapa Dar waungwana hapa ni zaidi ya sehemu zote nimebaki kujiuliza hivi haya matamko ya Polepole hawayasikii au viburi vimewajaa tena huku wanatishiwa kabisa vijana waliotia nia na wenye fedha.

Wiki kadha zilizopita kule Tanga nako ilikuwa hatari mno wanagawa sana fedha kwa ufupi mchakato wa kura za maoni washindi watakuwa wenye fedha na umaarufu na wale wenye vyeo sasa hivi ma-RC,ma-DC na ma-DED wachache saana hawa wasio na kitu watakaotoboa kutokana na uhalisia wa siasa za Tanzania.

Nimwombe ndugu Polepole watumieni vizuri watu wa vyombo hali ni mbaya sana Rais ana nia nzuri na chama ila mikoani huko balaa tupu hata hivyo vyombo vinanunulika huko ni marafiki zao matajiri na wenye vyeo.
Hivi unazan toka lini wagombea ccm wakapita bila Rushwa? Hayo matamko ya Polepole yapo toka enzi za Nyerere na still watu kama hao wapo tena wengi tu pale. Haijawai kutokea wakawa siriaz na jambo la Rushwa hata Mara moja kama unabisha niambie ni mgombea gani kawahi kufungwa kwa kosa la Rushwa ya uchaguzi au labda Bia yetu anasemaje kwani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi mtu mwenye pesa yake ya kutosha atupe pesa yake huku akijua bunge la Ndugai na serikali ya Magufuli haipendezewi na vipato vya wabunge?Kama ni kutafuta uwaziri mtaishia kutumbuliwa?
 
Back
Top Bottom