Mnyanyembe wa Mboka
JF-Expert Member
- Feb 10, 2017
- 2,347
- 3,033
Mkuu Mayalla ... kwa ufafanuzi wako na kwa sababu wewe ni msomi wa sheria naweza kukubaliana na wewe ila nina swali juu ya maelezo yako ili nijiweke salama katika kukubaliana na weweMkuu Pulchra Animo , asante kwa hoja zako, na kubwa zaidi ni jinsi ulivyomaliza hoja hii kwa maneno haya "Kazi ya kutafisiri sheria ni ngumu. Ukiishia kwenye literal meaning ya neno linalosomeka kwenye sheria husika, mara nyingi, utachemsha!". Naomba kuchangia ifuatavyo in points format
Kwa maoni yangu, this is wrong!. Lengo la mtunga katiba kutaka wabunge waape kwenye kikao cha Bunge, yaani, parliament in session, yenye mamlaka ya kibunge kwasababu wabunge ni watunga sheria, viapo vyao lazima viwe na mamlaka, ili kuwapa mamlaka ya kutunga sheria.
- Kitu cha kwanza kinachozingatiwa kwenye kuitafsiri sheria, ni kuangalia mtunga katiba alidhamiria nini kwa kifungu husika?.
- Mfumo wetu wa utawala una mihimili 3 inayojitegemea, Serikali, Bunge na Mahakama, hivyo wakuu wa mihimili hiyo, Rais, Spika na Jaji Mkuu ndio waapishaji wakuu, waapishaji wengine wote ni kwa niaba yao!.
- Kuna viapo ambavyo anatajwa muapishaji bila katiba kuweka mahali, mfano viapo vyote vya Rais, au Jaji Mkuu, katiba haukusema rais ataaoishia Ikulu au Jaji Mkuu ataapishia mahakamani, hii maana yake rais anaweza kuapishiwa popote na kuapishia popote, sambamba na CJ anaweza kuapishia popote.
- Lakini kwa kiapo cha Mbunge, Mtunga Katiba amesema wazi, Mbunge ataapa mbele ya Spika, Bungeni!.
- Neno Bungeni halimaaninishi jengo la Bunge, bali limemaanisha Mamlaka ya Bunge!.
- Jengo la Bunge na Mamlaka ya Bunge ni vitu viwili tofauti, kama ilivyo kwa neno Mahakama na Chumba cha Mahakama.
- Jengo la Bunge ni eneo lolote ambalo Bunge linaweza kuendeshewa, na sio lazima ule ukumbi wa Bunge, linaweza kuendeshewa popote. Lakini ili liwe ni Bunge, lazima liwe na Mamlaka ya Kibunge, session.
- Vivyo hivyo kwa Mahakama na chumba cha mahakama, Mahakama ni ile session, eneo lolote linaweza kuwa chumba cha mahakama lakini ili iwe ni mahakama lazima iwe na mamlaka, court session.
- Hivyo mtunga katiba aliposema Mbunge ataapishwa mbele ya Spika Bungeni akimaanisha Mbunge ataapa kwenye kikao cha Bunge, Session yenye mamlaka ya kibunge na sio eneo la Bunge.
- Watunga Kanuni wakadhani Mtunga katiba alimaanisha eneo la Bunge, hivyo wakakasimu madaraka kwa Spika, kuapishia eneo lolote!. Kwa lugha nyingine, kanuni imempa Spika mamlaka ya yeye Spika kujingeuza ni mamlaka ya kibunge na kuapishia wabunge eneo lolote.
NB. Pamoja na kanuni hiyo kwenda kinyume cha katiba, lakini kitendo alichokifanya Spika kuwaapisha wabunge nje ya kikao, ni kitendo halali kwa mujibu wa kanuni. Kama Bunge limetunga kanuni batili kwa kwenda kinyume cha katiba, kanuni hiyo itakuwa ni halali mpaka pale itakapo batilishwa, hivyo Spika Mhe. Job Ndugai is right kufanya anachokifanya kwasababu ndivyo kanuni inavyosema!.
Hata ikitokea, mtuhumiwa akahukumiwa kunyongwa kwa makosa, na mnyongaji akamnyonga kwa kutekeleza hakumu ya mahakama. Baada ya kunyongwa ikathibitika alihukumiwa kwa makosa, mwenye kosa ni aliyehukumu, huyo mnyongwaji atakuwa amenyongwa kwa makosa, lakini mnyongaji did the right thing, kazi yake ni kunyonga, akiletewa mtu wa kunyongwa, kazi yake ni kunyonga tuu na sio kujua amekosa nini.
Kwa muktadha huo, Spika Mhe. Job Ndugai ametimiza wajibu wake kwa mujibu wa kanuni halali ya Bunge, kama kuna makosa, yamefanywa na mtunga kanuni.
P.
Kabisa bila ya shaka nakubaliana kuwa jengo la Bunge na eneo la Bunge ni vitu viwili tofauti kwani jengo litabaki kuwa jengo tu lililojengwa kama majengo mengine
Hivyo Bunge inaweza kuwa eneo lolote lile lililo chaguliwa kuwa hapo ni Bungeni whether ni uwanja tu au kuwe kumefungwa maturubai au pana kibanda tu cha makuti au hata pawe na jengo la ghorofa 70
Sasa swali ili eneo hilo lililo chaguliwa liwe ni eneo la Bungeni kwa mujibu wa katiba kunapaswa kuwe na vigezo gani kukamilisha maana hiyo ya Bunge katika eneo lolote lililocahaguliwa ... ?
1. Je, kuna sehemu yeyote katika katiba au kanuni inayoelezea ili eneo lolote liwe Bungeni panapaswa kukamilisha vigezo gani ili eneo hilo liwe eneo la Bunge ... ?
2. Je, ile SIWA ina tafsiri yeyeote inayoendana au kushikamana na eneo ambalo linatumiwa kama Bunge ...?
3. Je, kuwepo kwa SIWA katika Bunge kuna kunahusiana au kuna ulazima ili kukamilisha tafsiri ya Bunge katika eneo lolote lile ...?