kindikwili
JF-Expert Member
- Oct 5, 2016
- 1,862
- 2,871
Wakuu amani iwe kwenu,
Bila shaka wengi wetu wameona kauli mbiu hizi kwenye mabango ya wagombea mbali mbali hasa wa chama cha mapinduzi (CCM). Mgombea wa Urais Zanzibar kwenye bango lake kuna maneno "Zanzibar mpya", Mgombea wa Ubunge kigamboni kuna neno "Kigamboni Mpya" kwingine kuna Tanzania mpya" kwa ufupi wagombea wengi wa chama tawala wana hii kaulimbiu.
Wagombea ubunge wengi wanaosema sijui kigamboni mpya au ...mpya wamekuwa kwenye nafasi zao za ubunge kwa muda wa miaka 5, wengine kwa miaka10 na wengine kwa zaidi ya hiyo miaka. Hivi inaingia akilini kwamba hii kaulimbiu ni muafaka kwao kutumia? miaka 5 au 10 umekuwa mbunge au Rais halafu unatuambia tukuchague ili kigambani au serengeti iwe mpya? Kwanza mpya kiaje? nadhani wangekuwa waungwana wangetuambia kwanini kwa muda tuliowapa walishindwa kufanya hayo maeneo kuwa mapya, bila kupepesa wangesema wazi safa za hiyo inayoitwa mpya na zamani (mfano ndugu Ndugulile ungesema sifa ya kigamboni ya zamani uliyokuwa mbunge wake huko nyuma na kigamboni mpya unayotaka kwasasa?. Hili suali liko kwenye nafasi zote za udiwani, ubunge na urais bila kujali jimbo au chama.
Kwa chama cha mapinduzi nini maana ya kauli mbiu hii kwenye mabango yenu ya urais maana toka uhuru nyie ndiyo mnatuongoza na kututawala? Zipi zilikuwa sifa ya Tanzania ya zamani chini ya ccm na zipi zitakuwa sifa ya Tanzania mpya chini ya ccm baada ya uchaguzi?
Kuuliza si ujinga ni kutaka kujua
CCM Mpya!
Tanzania Mpya
Bila shaka wengi wetu wameona kauli mbiu hizi kwenye mabango ya wagombea mbali mbali hasa wa chama cha mapinduzi (CCM). Mgombea wa Urais Zanzibar kwenye bango lake kuna maneno "Zanzibar mpya", Mgombea wa Ubunge kigamboni kuna neno "Kigamboni Mpya" kwingine kuna Tanzania mpya" kwa ufupi wagombea wengi wa chama tawala wana hii kaulimbiu.
Wagombea ubunge wengi wanaosema sijui kigamboni mpya au ...mpya wamekuwa kwenye nafasi zao za ubunge kwa muda wa miaka 5, wengine kwa miaka10 na wengine kwa zaidi ya hiyo miaka. Hivi inaingia akilini kwamba hii kaulimbiu ni muafaka kwao kutumia? miaka 5 au 10 umekuwa mbunge au Rais halafu unatuambia tukuchague ili kigambani au serengeti iwe mpya? Kwanza mpya kiaje? nadhani wangekuwa waungwana wangetuambia kwanini kwa muda tuliowapa walishindwa kufanya hayo maeneo kuwa mapya, bila kupepesa wangesema wazi safa za hiyo inayoitwa mpya na zamani (mfano ndugu Ndugulile ungesema sifa ya kigamboni ya zamani uliyokuwa mbunge wake huko nyuma na kigamboni mpya unayotaka kwasasa?. Hili suali liko kwenye nafasi zote za udiwani, ubunge na urais bila kujali jimbo au chama.
Kwa chama cha mapinduzi nini maana ya kauli mbiu hii kwenye mabango yenu ya urais maana toka uhuru nyie ndiyo mnatuongoza na kututawala? Zipi zilikuwa sifa ya Tanzania ya zamani chini ya ccm na zipi zitakuwa sifa ya Tanzania mpya chini ya ccm baada ya uchaguzi?
Kuuliza si ujinga ni kutaka kujua
CCM Mpya!
Tanzania Mpya