Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,371
Kwa ninavyofahamu,mtumishi wa umma akisimamishwa kazi analipwa mshahara nusu na baadae akija kuonekana hana makosa/hatia basi hurejeshwa kazini na kulipwa sehemu mishahara yake yote iliyobaki.
Si hivyo tu,hats mtumishi wa umma akifukuzwa kazi na mtumishi huyo kwenda mahakamani na baadae mahakama ikaamuru mtumishi huyo arejeshwe kazini,bila shaka mwajiri(serikali) itawajibika kumlipa mtumishi huyo mishahara ya miezi yote ambayo mtumishi husika hakulipwa kutokana na yeye kufukuzwa kazi kimakosa.
Sasa najiuliza iwapo wabunge wa CUF waliofukuzwa uanachama na kuvuliwa ubunge itathibitika mahakamani kuwa walifukuzwa kimakosa,hawatakuwa na haki ya kudai mishahara yao?
Kama watakuwa na haki hiyo, atakaepaswa kuwalipa ni nani?
Ni chama kilichowavua uanachama na kusababisha wao kupoteza ubunge au serikali inayowalipa mishahara?
Au ni chama ndio kitapaswa kuwalipa fidia?
Mikopo waliochukuwa wabunge hawa(kama ipo) nani atapaswa kuilipa kwa sasa wakati mshahara hawapati?
Kama kuna bima,je, mbunge anapofukuzwa uanachama na hivyo kupoteza ubunge wake,bima hapa inahusika?
Wabunge hawa waliokula kiapo leo hii na kuwa wabunge kamili,si wanastahili mikopo kwa mujibu wa sheria?
Kesho na keshokutwa mahakama ikawavua ubunge wabunge hawa walioapidhwa leo huku wameshachukua mikopo(iwapo watachukua) watairejesha kwa vipato gani?
Au wabunge mikopo yao hawairejeshi kupitia wao kukatwa mishahara?
Kwa mujibu wa sheria/taratibu,serikali hulipa sehemu ya mikopo hii wanayochukua wabunge, sasa ikitokea mahakama imewavua hawa ubunge,kisheria na hivyo wao kuwa si wabunge tena,sheria itaruhusu serikali kulipia mkopo wa mtu ambae si mbunge tena?
Baada ya wabunge hawa wa viti maalumu kuapishwa leo hii na mamlaka husika kuridhia wabunge waliovuliwa uanachama si wabunge halali,serikali inaendelea kulipia sehemu ya mikopo yao?
Au ndio watakatwa mafao yao?
Kwasababu wametumika Bunge kwa muda mfupi tu,mafao hayo yatatosha?
Hapa ndipo napoona hasara ya mahakama kutotoa zuio la wabunge hawa kuapishwa na pia kutoruhusu wabunge wa sasa kuendelea na ubunge wao mpaka pale kesi ya msingi itakapotolewa uamuzi.
Si hivyo tu,hats mtumishi wa umma akifukuzwa kazi na mtumishi huyo kwenda mahakamani na baadae mahakama ikaamuru mtumishi huyo arejeshwe kazini,bila shaka mwajiri(serikali) itawajibika kumlipa mtumishi huyo mishahara ya miezi yote ambayo mtumishi husika hakulipwa kutokana na yeye kufukuzwa kazi kimakosa.
Sasa najiuliza iwapo wabunge wa CUF waliofukuzwa uanachama na kuvuliwa ubunge itathibitika mahakamani kuwa walifukuzwa kimakosa,hawatakuwa na haki ya kudai mishahara yao?
Kama watakuwa na haki hiyo, atakaepaswa kuwalipa ni nani?
Ni chama kilichowavua uanachama na kusababisha wao kupoteza ubunge au serikali inayowalipa mishahara?
Au ni chama ndio kitapaswa kuwalipa fidia?
Mikopo waliochukuwa wabunge hawa(kama ipo) nani atapaswa kuilipa kwa sasa wakati mshahara hawapati?
Kama kuna bima,je, mbunge anapofukuzwa uanachama na hivyo kupoteza ubunge wake,bima hapa inahusika?
Wabunge hawa waliokula kiapo leo hii na kuwa wabunge kamili,si wanastahili mikopo kwa mujibu wa sheria?
Kesho na keshokutwa mahakama ikawavua ubunge wabunge hawa walioapidhwa leo huku wameshachukua mikopo(iwapo watachukua) watairejesha kwa vipato gani?
Au wabunge mikopo yao hawairejeshi kupitia wao kukatwa mishahara?
Kwa mujibu wa sheria/taratibu,serikali hulipa sehemu ya mikopo hii wanayochukua wabunge, sasa ikitokea mahakama imewavua hawa ubunge,kisheria na hivyo wao kuwa si wabunge tena,sheria itaruhusu serikali kulipia mkopo wa mtu ambae si mbunge tena?
Baada ya wabunge hawa wa viti maalumu kuapishwa leo hii na mamlaka husika kuridhia wabunge waliovuliwa uanachama si wabunge halali,serikali inaendelea kulipia sehemu ya mikopo yao?
Au ndio watakatwa mafao yao?
Kwasababu wametumika Bunge kwa muda mfupi tu,mafao hayo yatatosha?
Hapa ndipo napoona hasara ya mahakama kutotoa zuio la wabunge hawa kuapishwa na pia kutoruhusu wabunge wa sasa kuendelea na ubunge wao mpaka pale kesi ya msingi itakapotolewa uamuzi.