Poleni sana na kazi za kila siku za kuhakikisha kuwa sisi watanzania wenzenu tunapata ajira.
Mimi ni mtanzania ninaeishi mkoa wa Mara, ninapenda kuuliza maswali yafuatayo:
Hivi huwa mnajisikiaje kuita watu kwenye usaili kuja Dar es salaam huku mkitambua kwa hakika usumbufu na umasikini tuliyonayo sisi watanzania?
kwani hamjui kuwa:
-watafuta kazi walio wengi tunaishi mikoani vijijini kwetu kwa hiyo wengi hatuna ndugu huko Dar es salaam?
-Hiyo pesa ya kunikalisha huko Dar es salaam kwa siku zote za usaili nitatoa wapi?
-Je nyie hamtambui kuwa jiji la Dar es salaam kwa sasa lina idadi kubwa sana ya watu inayotokana na kulundikana kwa taasisi zinazotoa huduma muhimu kama hii ya kwenu?
-Nyie kama taasisi ya watanzania na siyo taasisi yawana Dar es salaam mna mikakati gani ya kuhakikisha kwamba katika mchakato wa kutoa ajira kwa watanzania unakuwa ni wa haki ukizingatia kwamba watafuta kazi wengi sana wanashindwa kuhudhuria usaili kutokana na sababu nilizozitaja hapo juu?
-kama mnashindwa kugawa vitengo vyenu kikanda kutokana na baadhi ya watendaji mlionao kukataa au kugoma kwenda mikoani mbona wapo watanzania ambao siyo wa Dar es salaam lakini bado wanasifa na wanaweza wakafanya kazi nzuri huenda kuliko hata hao?
MWISHO- je ni sahihi kwamba mtu yeyote anayetafuta kazi ni lazima atafute mahali pa kujishikiza Dar es salaam au awe na ndugu ama pesa zitakazo muwezesha kuhudhuria usaili unaofanyikia huko? Hamuoni kwamba mwishoni mtajikuta kwamba mnaajiri tu watu wa Dar es salaam kutokana na sisi wa mikoani kushindwa kuja huko kwa sababu ya michosho ya mchakato mzima katika mchakato wa ajira?
Mimi ni mtanzania ninaeishi mkoa wa Mara, ninapenda kuuliza maswali yafuatayo:
Hivi huwa mnajisikiaje kuita watu kwenye usaili kuja Dar es salaam huku mkitambua kwa hakika usumbufu na umasikini tuliyonayo sisi watanzania?
kwani hamjui kuwa:
-watafuta kazi walio wengi tunaishi mikoani vijijini kwetu kwa hiyo wengi hatuna ndugu huko Dar es salaam?
-Hiyo pesa ya kunikalisha huko Dar es salaam kwa siku zote za usaili nitatoa wapi?
-Je nyie hamtambui kuwa jiji la Dar es salaam kwa sasa lina idadi kubwa sana ya watu inayotokana na kulundikana kwa taasisi zinazotoa huduma muhimu kama hii ya kwenu?
-Nyie kama taasisi ya watanzania na siyo taasisi yawana Dar es salaam mna mikakati gani ya kuhakikisha kwamba katika mchakato wa kutoa ajira kwa watanzania unakuwa ni wa haki ukizingatia kwamba watafuta kazi wengi sana wanashindwa kuhudhuria usaili kutokana na sababu nilizozitaja hapo juu?
-kama mnashindwa kugawa vitengo vyenu kikanda kutokana na baadhi ya watendaji mlionao kukataa au kugoma kwenda mikoani mbona wapo watanzania ambao siyo wa Dar es salaam lakini bado wanasifa na wanaweza wakafanya kazi nzuri huenda kuliko hata hao?
MWISHO- je ni sahihi kwamba mtu yeyote anayetafuta kazi ni lazima atafute mahali pa kujishikiza Dar es salaam au awe na ndugu ama pesa zitakazo muwezesha kuhudhuria usaili unaofanyikia huko? Hamuoni kwamba mwishoni mtajikuta kwamba mnaajiri tu watu wa Dar es salaam kutokana na sisi wa mikoani kushindwa kuja huko kwa sababu ya michosho ya mchakato mzima katika mchakato wa ajira?