Maswali magumu ya Tundu Lissu hayawezi kamwe kujibiwa na utawala huu wa Rais Magufuli

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Tunashuhudia Tundu Lissu akiendelea "kuisambaratisha" serikali hii ya awamu ya tano huko katika vyombo vya habari vya kimataifa

Tumeshuhudia namna ambavyo Tundu Lissu "alivyoichanachana" serikali hii ya awamu ya tano kwenye mahojiano yake katika kipindi maarufu cha Hardtalk cha BBC

Tumeshuhudia pia namna Tundu Lissu alivyomtoa "knockout" Balozi wa Tanzania huko Umoja wa Mataifa, Wilson Masilingi, katika mahojiano yao na chombo cha habari cha VoA

Yamekuwepo maswali mengi yakiulizwa hivi seriakali hii ya awamu ya tano hawana watu mahiri wa kuyajibu hayo maswali ya Tundu Lissu??

Jibu nitakalokupa hapo ni hakuna mwanasiasa yeyote kutoka nchini Tanzania ambaye ni Mcha Mungu wa ukweli mwenye ubavu wa kuyajibu maswali hayo ya Tundu Lissu

Hebu niyaweke baadhi ya maswali hayo:-

1. Ni kwanini eneo alilopigwa risasi Tundu Lissu, panapokuwepo na ulinzi wa masaa 24 ya kila siku wa walinzi wenye silaha, hapakuwa na walinzi, katika siku hiyo ya tukio tarehe 7/9/2017??

2. Ni kwanini vyombo vya ulinzi na usalama vya ndani, vimegoma kushirikisha vyombo vya nje vya uchunguzi katika tukio la kushambuliwa kwa Tundu Lissu??

3.Je kama vyombo vya ulinzi na usalama vilitoa sababu kuwa hawawahitaji wachunguzi wa nje kuja kuchunguza tukio hilo/kwa madai kuwa wao wana uwezo wa kuwabaini wahalifu hao, ni kwanini hadi sasa, zaidi ya mwaka mmoja na nusu, tokea tukio hilo litokee, hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyekamatwa na Jeshi letu la Polisi na kufanyiwa mahojiano na kuburuzwa mahakamani??

4. Ni kwanini CCTV camera zilizokuwa kwenye nyumba ya Waziri Medard Kalimani, nyumba iliyoko jirani kabisa ya tukio la mashambulizi, zilionyofolewa na kupelekwa mahali kusikojulikana, mara tu baada ya shambulizi lile??

5. Ni kwanini Spika Ndugai amegoma kutoa stahiki za malipo ya matibabu, ambayo ni stahiki ya kila Mbunge anapopata na matatizo ya kuumwa, kwa mujibu wa kanuni za Bunge letu??

Hayo ndiyo maswali magumu kabisa ambayo naweza kudiriki hakuna mtendaji yeyote wa serikali hii ambaye atadiriki kujitia "kitanzi" na kuyajibu maswali hayo, kwa kuwa wahenga walisema PENYE UKWELI UWONGO HUJITENGA!

Nimalizie kwa kusema kuwa siyo KWELI kuwa Mbunge Tundu Lissu analichafua Taifa hili na kuwatukana viongozi wa serikali bila sababu za msingi, bali anataka mumjibie maswali yake anayoyauliza

Majibu SAHIHI yasiyo ya "kutunga" kutoka kwa watendaji wa serikali hii ya awamu ya tano tutayasubiri sana na pengine tutasubiri hadi Yesu Kristo arejee hapa dumiani, bila ya kupata majibu SAHIHI ya maswali hayo!

Tukumbuke msemo wa wahenga unaosema MWISHO WA UBAYA AIBU!
 
Hvi mnafikiri hao wa nje wanaweza kufanya nin hapa tz kwa mwendlezo wa lissu kuhojiwa?

wakati ukuta.
 
Hvi mnafikiri hao wa nje wanaweza kufanya nin hapa tz kwa mwendlezo wa lissu kuhojiwa?

wakati ukuta.
Wewe hujui kuwa Jiwe anachokifanya ni kuabuse power tuliyompa.......

Hivi kama nchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi inasema ni ya vyama Vingi, ni kwanini basi Jiwe "awa-treat" wapinzani hao kama wahaini??

Mfano wa dhahiri ni kwanini Viongozi wa Chama kikuu cha upjnzani cha Chadema, mbunge Freeman Mbowe na Mbunge mwenzake Esther Matiko waendelee kusota rumande kwa zaidi ya miezi miwili hivi sasa, kwa kile wanachokiita wamedharau mahakama??
 
Jiwe anadai anainyoosha nchi, Lissu anamnyoosha Jiwe.

JIWE is a politician who is a paradox. He seems to have good intensions for his country but the way he implements his policies in order to achieve his goals hurts the same people he says he wants to protect!

He has to change his governance style, he should pay more emphasis on the needs of his citizenly as opposed to things. Serikali huanguka sio kwasababu hakuna fly -overs bali kwasababu watu hawana chakula!!!!
 
Vyombo vya ulinzi na usalama vya Jiwe ndio watuhumiwa, swali ni nani wa kuwawajibisha??
Kwa sasa hivi tunaweza kusema hakuna.....

Bur the day will come when everything which is hidden will be disclosed to the Public!
 
Kama hawana madhara kwanini mnaweweseka na Lissu kuhojiwa??
Ndilo swali la msingi la kumuuliza huyo kada wa Lumumba.......

Hivi ni kwanini hivi sasa vitanda vimekuwa havilaliki pale Magogoni kwa kuwazia vigongo vinavyoporomoshwa na Tundu Lissu kwenye vyombo vya habari vya kimataifa??
 
Tatzo lenu mnapenda kukubari kila kinenwacho na watu pasipo kuja na uthbitisho
Ndilo swali la msingi la kumuuliza huyo kada wa Lumumba.......

Hivi ni kwanini hivi sasa vitanda vimekuwa havilaliki pale Magogoni kwa kuwazia vigongo vinavyoporomoshwa na Tundu Lissu kwenye vyombo vya habari vya kimataifa??

wakati ukuta.
 
Tatzo lenu mnapenda kukubari kila kinenwacho na watu pasipo kuja na uthbitisho

wakati ukuta.
Siyo kukubali tunachoambiwa........

Bali tunataka maswali yanayoulizwa na Tundu Lissu yajibiwe kwa usahihi, pasipo kutumbukiza propaganda
 
Kwa hiyo hawa wabunge wapo juu ya sheria?
Wewe hujui kuwa Jiwe anachokifanya ni kuabuse power tuliyompa.......

Hivi kama nchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi inasema ni ya vyama Vingi, ni kwanini basi Jiwe "awa-treat" wapinzani hao kama wahaini??

Mfano wa dhahiri ni kwanini Viongozi wa Chama kikuu cha upjnzani cha Chadema, mbunge Freeman Mbowe na Mbunge mwenzake Esther Matiko waendelee kusota rumande kwa zaidi ya miezi miwili hivi sasa, kwa kile wanachokiita wamedharau mahakama??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliona Balozi Masilingi akimkazania sana mgonjwa arudi Tanzania.Je wana nia ya kumfanya nini akirudi?
 
Niliona Balozi Masilingi akimkazania sana mgonjwa arudi Tanzania.Je wana nia ya kumfanya nini akirudi?
Hata mimi nilishangaa kwa Balozi Masilingi kususitiza kwa nguvu zote kuwa Tundu Lissu na dereva wake warudi haraka Tanzania!

Inabidi tuweke question mark nyingi sana????????????

Kuna nini Tanzania hadi huyu Balozi asisitize sana arudi Tundu Lissu??
 
Back
Top Bottom