Maswali Magumu: Ni kweli Hospitali ya Aga Khan Hawawezi Kupima na Kugundua Kama Mgonjwa ana Malaria?

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Ninaomba nisieleweke vibaya jamani. Huu ni mnakasha kama minakasha mingine tu. Kuna minakasha zaidi ya milioni mbili hapa JF. Basi tuongeze na huu hapa.

Kwamba, Aga Khan Hospital, moja ya hospitali ambazo ni nadra sana Mtanzania wa daraja la chini kumudu gharama za matibabu pale, ikisifika kwa kutoa huduma bora kabisa Tanzania na duniani kwa ujumla. Ni kweli kabisa kwamba wanaweza kushindwa kupima na kugundua malaria? Mara mbili? Twice?

Mods msikwapue hii thread.


Tuacheni tujadili hadhi na ubora wa hospitali zetu.

Msukuma

a.k.a Mwana Chadema mpaka kufa!!!
 
Hii hali inasikitisha, lakini inatoa taswira ya hali ya huduma zetu za afya zilivyo hapa nchini.
Hatuna sehemu tunayoweza kukimbilia hata kama una pesa nyingi kiasi gani. Tutabaki kwenda kutibiwa India na ulaya hasa kwa wale wenye uwezo. Lakini kwa wenzangu na mimi tutakufa kabla ya siku zetu.
Kuna mgonjwa mmoja alikuja hapo aga khan mwaka jana, baada ya kuchukua history na examination, niliona kama anadalili zote za malaria, nikamwandikia afanye B/S cha kushangaza majibu yalikuja negative. Kutokana na wenzetu kuwa na akili nyingi na wengi wa wagonjwa hao kuwa ni wasomi alikataa katakata dawa za malaria nilizomwandikia kwa kusema kwamba hawezi kuzitumia kwa kuwa vipimo vimeonesha hana malaria. Wiki moja baadaye yule mgojwa aliletwa tena hosp. mara hii alikuwa hajitambui na alikuja na majibu ya malaria yaliyoenesha alikuwa na malaria wadudu zaidi ya 1000 na alifariki baada ya siku mbili. Its so sad na inasikitisha, Nadhani kuna umuhimu wa mamlaka zinazohusika kufanya ukaguzi hadi kwenye baabara za mahospitali ili wateja tuwe na uhakika wa majibu tunayopewa.
Lakini pia ni lazima hizi hospitali ziajiri watu competent ili waweze kutoa huduma bora.
 
Sio kweli, Hiyo hospital hawashindwi kutoa hayo Majibu,swali ni Je ni kweli huyo Mtu ana Malaria au la, Maana tunasikia kafanyiwa upasuaji, Upasuaij na Malaria wapi na wapi
 
Back
Top Bottom