Alfu Lela Ulela
JF-Expert Member
- Oct 29, 2010
- 1,255
- 77
Jana nimepata taarifa kupitia vyombo vya habari (Chanel Ten-taarifa ya saa 1jioni na TBC-kwny usiku wa habari), kuhusu mpango wa NEW HABARI CORPORATION kuisaidia familia ya aliyekuwa mhariri msaidizi wa gazeti la RAI marehemu Dany Mwakiteleko.
Miongoni mwa ahadi alizotoa Bashe ni kumlipa mke wa Dany mshahara wa mumewe kwa miaka mitano, na kusomesha watoto wawili wa Dany pamoja na other two depandants hadi level ya University.
Lakini kabla sijapongeza hatua hiyo naomba kumuuliza Bashe maswali kadhaa ya msingi ambayo majibu yake yatatupa taswira ya alichosema jana.
Kwanza,
je kwa mshahara wa miaka mitano atakaolipwa mkewe, inamaanisha kuwa atapoteza stahili zake nyingine alizokuwa nazo Dany kama mwajiriwa? Mbona hatujasikia suala ka pension ya Dany?
Pili,
Je Dany ni mwajiriwa wa kwanza wa NEW HABARI kufariki? Ikiwa sivyo, je aliyemtangulia Dany alifanyiwa hivyo? Kama hakufanyiwa, je ni vigezo gani vimetumika kumpa Dany offer hiyo?
Tatu,
Je utaratibu huu ni kwa Dany pekee au ni wafanyakazi wote wa NEW HABARI? Je akifa mwingine utaratibu utakuwa huohuo?
Nne,
Je mshahara atakaolipwa mkewe Dany utakuwa ukipanda kila mwaka au atalipwa mshahara Dany aliostaafia kwa miaka yote mitano?
Sita,
mtoto mdogo wa Dany yuko darasa la sita. Ameahidiwa kusomeshwa hadi chuo kikuu, je kampuni itakuwepo kwa kipindi chote hicho?
Vipi ikiwa kampuni itakufa mwakani?
Saba,
nani atasimamia utekelezaji wa ahadi hizo?
NB:Ikumbukwe ahadi zilizotolewa ni hisani (courtesy). Hisani hailazimishwi kulipwa. Hakuna mkataba familia ya Dany imesaini ili hayo yaliyoahidiwa yasipotekelezwa familia ichukue hatua.So utekekezaji wake utategemea kudra za NEW HABARI, na Bashe kama MD.
Mwisho natoa rai kwa media houses nyingine (hasa za Reginald Mengi) kuiga mfano waliounesha NEW HABARI.
Mungu ibariki tasnia adhimu ya habari,
Mungu ibariki TZ.
Miongoni mwa ahadi alizotoa Bashe ni kumlipa mke wa Dany mshahara wa mumewe kwa miaka mitano, na kusomesha watoto wawili wa Dany pamoja na other two depandants hadi level ya University.
Lakini kabla sijapongeza hatua hiyo naomba kumuuliza Bashe maswali kadhaa ya msingi ambayo majibu yake yatatupa taswira ya alichosema jana.
Kwanza,
je kwa mshahara wa miaka mitano atakaolipwa mkewe, inamaanisha kuwa atapoteza stahili zake nyingine alizokuwa nazo Dany kama mwajiriwa? Mbona hatujasikia suala ka pension ya Dany?
Pili,
Je Dany ni mwajiriwa wa kwanza wa NEW HABARI kufariki? Ikiwa sivyo, je aliyemtangulia Dany alifanyiwa hivyo? Kama hakufanyiwa, je ni vigezo gani vimetumika kumpa Dany offer hiyo?
Tatu,
Je utaratibu huu ni kwa Dany pekee au ni wafanyakazi wote wa NEW HABARI? Je akifa mwingine utaratibu utakuwa huohuo?
Nne,
Je mshahara atakaolipwa mkewe Dany utakuwa ukipanda kila mwaka au atalipwa mshahara Dany aliostaafia kwa miaka yote mitano?
Sita,
mtoto mdogo wa Dany yuko darasa la sita. Ameahidiwa kusomeshwa hadi chuo kikuu, je kampuni itakuwepo kwa kipindi chote hicho?
Vipi ikiwa kampuni itakufa mwakani?
Saba,
nani atasimamia utekelezaji wa ahadi hizo?
NB:Ikumbukwe ahadi zilizotolewa ni hisani (courtesy). Hisani hailazimishwi kulipwa. Hakuna mkataba familia ya Dany imesaini ili hayo yaliyoahidiwa yasipotekelezwa familia ichukue hatua.So utekekezaji wake utategemea kudra za NEW HABARI, na Bashe kama MD.
Mwisho natoa rai kwa media houses nyingine (hasa za Reginald Mengi) kuiga mfano waliounesha NEW HABARI.
Mungu ibariki tasnia adhimu ya habari,
Mungu ibariki TZ.