Maswali kwa polisi na madaktari kuhusu mlipuko Arusha

gagonza

JF-Expert Member
Oct 18, 2009
309
98
Kwanini polisi waliwapiga watu risasi za moto waka watu wanajiokoa? Wamepigwa watu zaidi ya 3 waliopigwa risasi ya moto tumeokota maganda mawili ya risasi.

Pili kwanini madaktari wa Mount Meru Hospital walipoambiwa majeruhi kutoka mkutano wa CHADEMA walikimbia madaktari wote?
 
sasa ndugu yangu siyo swala la kujiuliza...wakati sababu inajulikana kuwa ni njama za ccm hizo na hakika awatashinda kabisa usicheze na Mungu akisha amua kutenda jambo juu ya maisha ya watu wake
 
kama madaktari walifanya hivyo ,itakuwa walienda nje ya maadili yao ya kazi kabisa..... shame upon them
 
kama na madaktari walikimbia kutibu wahanga, mmmmhhhhh very sad. Who is behind the bombing?
 
Upo mwisho tu...ingawa taarifa zako unazithibitishaje?
 
kwa suala la police hilo halina mjadala kwa sababu siyo mara yao ya kwanza kuhujumu mikusanyiko ya chadema si tu isiyo halali hata ile ambayo ni halali.kwa madaktari inawezekana ni taharuki tu akili zao hazikujiandaa kupokea tukio kama lile kwa muda ule.siyo rahisi jambo kubwa kama hili likawa limepangwa kwa kushirikisha watu wengi kiasi hicho.ni watu wachache wanaojua wanachofanya kwa maslahi yao kisiasa.kwa kutomkamata walau kwa mahojiano tu Mwigulu,na Mwampamba naona police bado hawapo tayari kuwapata na wahusika wa hili pia.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom