Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,985
- 20,263
Baada yakuzisoma makala zake tano zenye udhui la kulandana kwa jicho la tatu zaidi, imenilazimu kumuuliza maswali machache ili kujua zaidi msingi wa makala zake na yatarajiwayo KESHO.
1. Mkuu Mwanakijiji, maamuzi ya kamati kuu yalikuwa halali ama haramu kwamjibu wa katiba ya Chadema ya mwaka 2006?
2. Kutokana na maamuzi hayo, kuna haja ya chama kuacha katiba na kusaka kinachoitwa suluhu kwenye meza ya mduara?
3. Ipi nafasi ya Chadema katika uzingatiaji wa katiba yake na miiko ya chama katika mfumo huu wa vyama vingi nchini?
4. Wewe umekuwepo katika anga za siasa za Tanzania kwa mda mrefu sana, na umekuwa karibu kisiasa na wanasiasa wengi akiwemo Zitto Kabwe, je ipi nafasi ya Zitto Kabwe wa leo katika siasa za Chadema zinazotembea na kuishi katika katiba yake?
5. Vyama vya CUF, CCM na NCCR MAGEUZI vimeshaadhibu wanachama wake tena kwakuwavua uanachama kabisa huko nyuma, naomba uwathibitishie makutano wa jf ama popote pale kama uliwahi kutumia nguvu inayoshahabiana na hii unayotumia leo katika kubatilisha maamuzi ya cc ya Chadema,
Majadiliano ya hoja ni msingi wa ujenzi wa taifa lenye tija katika nyanja zote,
NB
Mods nawaomba msiunganishe uzi huu na zingine,
1. Mkuu Mwanakijiji, maamuzi ya kamati kuu yalikuwa halali ama haramu kwamjibu wa katiba ya Chadema ya mwaka 2006?
2. Kutokana na maamuzi hayo, kuna haja ya chama kuacha katiba na kusaka kinachoitwa suluhu kwenye meza ya mduara?
3. Ipi nafasi ya Chadema katika uzingatiaji wa katiba yake na miiko ya chama katika mfumo huu wa vyama vingi nchini?
4. Wewe umekuwepo katika anga za siasa za Tanzania kwa mda mrefu sana, na umekuwa karibu kisiasa na wanasiasa wengi akiwemo Zitto Kabwe, je ipi nafasi ya Zitto Kabwe wa leo katika siasa za Chadema zinazotembea na kuishi katika katiba yake?
5. Vyama vya CUF, CCM na NCCR MAGEUZI vimeshaadhibu wanachama wake tena kwakuwavua uanachama kabisa huko nyuma, naomba uwathibitishie makutano wa jf ama popote pale kama uliwahi kutumia nguvu inayoshahabiana na hii unayotumia leo katika kubatilisha maamuzi ya cc ya Chadema,
Majadiliano ya hoja ni msingi wa ujenzi wa taifa lenye tija katika nyanja zote,
NB
Mods nawaomba msiunganishe uzi huu na zingine,