Afrikasana
JF-Expert Member
- Oct 27, 2021
- 320
- 283
Mpaka kufikia leo January 9/2022 baadhi ya wanachuo hawajapewa mikopo tangia wamefungua vyuo yani wengine wanakaribia kusaini awamu ya pili wapewe fedha,wengine walisha saini ila hawajapewa fedha zao za awamu ya kwanza mpaka sasa. Je wewe mzee unataka nini hasa kwa watoto wa wanaume wenzio?
Je kama unawatoto au wajukuu waliopo masomoni hujawapa pia hela za kujikimu kwa miezi miwili sasa?
Hivi hizo hela kama zingekua za kwako siungetaka kusujudiwa kabisa?
Naomba kukuuliza hivi nikwanini unampangia mtu mkopo,unamsainisha kisha humpatii haki yake?
Hivi nikwanini wanachuo ambao hamkuwapa mkopo mwaka wa kwanza na mkaanza kuwapa mkopo mwaka wa pili hamtaki kuwapa malimbikizo ya mwaka wa kwanza?
Au wewe mzee ni mwanasiasa unapenda sana kuona maandamano ya watoto maskini hapo kwenye ofisi za bodi?
Hivi mzee unadhani wewe utaishi milele hapo bodi?
Au una maagano gani na mamlaka iliyo kuteua?
Kama huogopi mamlaka ya uteuzi umeiweka mkononi je Mungu humuogopi?
Mzee unakera sana,nielewe nikisema unakera. Wewe mzee ni jipu haiwezekani unakaa na fedha za wanachuo karibia miezi miwili huwapi.
Au hata wewe hujala na kunywa muda wote huo?
Hivi hiyo ni roho ya mzazi wa kitanzania kweli ambaye ameenda shule?
Tofauti yako msomi wewe na asiyesoma au asiyejua umuhimu wa elimu ni ipi?
Mzee ninayo maswali mengi lakini ngoja nikuache uendelee kuyatafakari hayo.
Jambo la ajabu huyo mama anayejiita Veronica Nyahende nae anasema eti bodi itaanza kutoa mikopo ndani ya masaa 24. Hivi huyo anafanya watu ni mazuzu?
Miezi miwili hutoi hela leo unahadaa watu na habari za masaa 24? Masaa 24 unayajua au unayasikia?
Miezi miwili umeshindwa masaa 24 utayaweza?
Wewe mama huwezi kuwa serious
Hiyo bodi imejaa majipu matupu kuanzia makao makuu mpaka wasimamizi wa kanda hadi vyuoni. Simu hampokei mkipigiwa
Mmejaa harufu za rushwa hata yatima na maskini pia mnatamani wawape rushwa ndio mtimize wajibu
MAMLAKA HUSIKA ONDOENI HAO WAZEMBE WAMEVIMBIWA VIYOYOZI
Je kama unawatoto au wajukuu waliopo masomoni hujawapa pia hela za kujikimu kwa miezi miwili sasa?
Hivi hizo hela kama zingekua za kwako siungetaka kusujudiwa kabisa?
Naomba kukuuliza hivi nikwanini unampangia mtu mkopo,unamsainisha kisha humpatii haki yake?
Hivi nikwanini wanachuo ambao hamkuwapa mkopo mwaka wa kwanza na mkaanza kuwapa mkopo mwaka wa pili hamtaki kuwapa malimbikizo ya mwaka wa kwanza?
Au wewe mzee ni mwanasiasa unapenda sana kuona maandamano ya watoto maskini hapo kwenye ofisi za bodi?
Hivi mzee unadhani wewe utaishi milele hapo bodi?
Au una maagano gani na mamlaka iliyo kuteua?
Kama huogopi mamlaka ya uteuzi umeiweka mkononi je Mungu humuogopi?
Mzee unakera sana,nielewe nikisema unakera. Wewe mzee ni jipu haiwezekani unakaa na fedha za wanachuo karibia miezi miwili huwapi.
Au hata wewe hujala na kunywa muda wote huo?
Hivi hiyo ni roho ya mzazi wa kitanzania kweli ambaye ameenda shule?
Tofauti yako msomi wewe na asiyesoma au asiyejua umuhimu wa elimu ni ipi?
Mzee ninayo maswali mengi lakini ngoja nikuache uendelee kuyatafakari hayo.
Jambo la ajabu huyo mama anayejiita Veronica Nyahende nae anasema eti bodi itaanza kutoa mikopo ndani ya masaa 24. Hivi huyo anafanya watu ni mazuzu?
Miezi miwili hutoi hela leo unahadaa watu na habari za masaa 24? Masaa 24 unayajua au unayasikia?
Miezi miwili umeshindwa masaa 24 utayaweza?
Wewe mama huwezi kuwa serious
Hiyo bodi imejaa majipu matupu kuanzia makao makuu mpaka wasimamizi wa kanda hadi vyuoni. Simu hampokei mkipigiwa
Mmejaa harufu za rushwa hata yatima na maskini pia mnatamani wawape rushwa ndio mtimize wajibu
MAMLAKA HUSIKA ONDOENI HAO WAZEMBE WAMEVIMBIWA VIYOYOZI