Elections 2010 Maswali haya yanahitaji majibu ya Dr. Slaa na Chadema mapema iwezekanavyo

Nimekuwa nikisikia minong'ono ya chini chini ambayo sasa imeanza kupazwa sauti na wagombea wa CCM kuwa ahadi za mgombea urais wa Chadema, Dr W Slaa, ni za uongo na hazitekelezeki. Kuna watu ambao ninawafahamu kuwa hawaipendi CCM lakini sasa wanaanza kuwa na mashaka na ahadi za Chadema kuwa kikingia madarakani kitatoa huduma za elimu na afya bure na pia kuwa kila kitu kitafanyiwa kazi ndani ya siku 100.

Ninashauri Chadema waanze kujibu haya maswali kwa kutoa vielelezo vya namna ambavyo wataweza kutoa elimu na afya bure, nawashauri watoe takwimu za idadi ya wanafunzi katika kila ngazi na gharama za kumsomesh mwanafunzi mmoja au kundi la wanafunzi 100 na waonyeshe ni namna gani watapata mapato ya kugharimia huduma hizi, kwa kusema tu jumla jumla kuwa kuna fedha inapotea kwenye misamaha ya kodi bila kutoa vielelezo watapoteza kura nyingi za watu ambao wangewapigia kama watapewa maelezo na vielelezo vinavyojitosheleza. Ikiwezekana waanze sasa kutupa hata mfano budget ya serikali yao kwa muhtasari.

Hii itawaziba midomo akina Kinana, Makamba, Kikwete na wengine kusema kuwa haya wanayoahidi Chadema na Slaa ni uongo. Pia itatoa fursa kwa watu makini kupima na kuona kuwa inawezekana watoto wao wakapata huduma bure na bora wakiwachagua Chadema. Nadhani kila mtu anataka kupata huduma bora na kwa gharama nafuu.

Kingine cha msingi ambacho nawashauri waanze kufanya ni kutoa maelezo ya namna ambavyo watatekeleza hayo wanayoyaahidi, nadhani hakuna Mtanzania leo hii ambaye hajui kuwa CCM ni genge la wahuni wasipoteze muda wao uliobaki kuelezea haya wajikite kwenye namna watakavyoshugulikia ikiwa ni pamoja na kutoa takwimu na vipeperushi. Naamini hii itawasaidia zaidi kuliko kupoteza muda wao kulipua makombora ya namna ambavyo Kikwete anaendesha nchi hii kama shirika la ukoo wao, tunajua na tunaelewa yote haya. Tunaomba tupatiwe majibu ya namna tutakavyotoka hapa


Nadhani bado hujawaelewa CHADEMA na itakuchukua muda mrefu kuwaelewa. Hili linatokana na ufinyu wa elimu yako, kwani inaonekana dhahiri kwamba HUKUFUNDISHWA kufanya tathmini (analysis) kwa mambo ya kiuchumi na kisiasa. Ahadi za CHADEMA zinatekelezeka. Ngoja nikupe mifano miwili tu!

1) Bunge la Jamhuri lililopita, lilipitisha bajeti ambayo ni dhahiri kwamba haikidhi mahitaji ya wananchi kutokana na ufinyu wake na upendeleo kwa matumizi yasiyo na lazima. Hili linatokana na kwamba Bunge hilo lilikuwa ni la chama kimoja, CCM, ambacho kilikuwa na idadi kubwa ya wabunge, na wabunge wachache wa upande wa upinzani. Hivyo, CHADEMA wasingeweza kufanya maamuzi yoyote yale kwa manufaa ya taifa.

2) Iwapo Dr. Slaa atachaguliwa kuwa Rais, ataweza kuunda Serikali yenye wizara chache, hivyo kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, na kupunguza kwa kiwango kikubwa idadi ya mawaziri na manaibu waziri. Chukua idadi ya mawaziri na manaibu waziri waliopo sasa, weka (kwa mfano) thamani ya wastani wa Toyota LandCruiser VX (mpya) kuwa TZS Milioni 200, kisha fanya hesabu. Kama idadi inazidi mawaziri na manaibu waziri 40, hesabu za haraka ni TZS Mil. 200 x 40 ambapo unapata jumla ya TZS 8,000,000,000, yaani, TZS Bilioni 8. Slaa ameahidi kuunda Serikali yenye mawaziri na manaibu waziri 20 tu! Kwa hiyo, ukiondoa nusu ya hao mawaziri na manaibu utapata jumla ya TZS Bilioni 4 kwa magari yao tu, hivyo tayari atakuwa ameokoa TZS Bilioni 4. Lakini hili litafanyika ENDAPO kiwango cha magari ya mawaziri na manaibu waziri kitakuwa ni Toyota LandCruiser VX, ambayo kwa kweli ni gari kubwa na ya anasa! Je, haiwezekani mawaziri na manaibu hawa kununuliwa, kwa mfano, gari zuri kama vile Toyota Rush (ambayo ina engine ndogo ya 1,500 CC na pia ni gari zuri sana), au magari mengine kama vile Toyota RAV4 model mpya? Lazima tuweke vipaumbele kwenye matumizi sahihi ya fedha za walipakodi.

Hii ni mifano miwili tu, ya mambo ambayo YANATEKELEZEKA kwa muda wa siku 100. Bunge la kwanza la Serikali mpya litakaa kikao chake Dodoma wakati huo, na sheria za kurekebisha bajeti (baada ya kuundwa kwa baraza la mawaziri na manaibu - iwapo italazimika kuwaweka - wachache, na kuwaapisha) ili tuwe na bajeti yenye TIJA, si HASARA na UFISADI!

Tuweke kipaumbele kwenye elimu, afya, miundombinu (kwa manufaa ya Watanzania wengi). Kuwasomesha watoto wetu bure, kuanzia chekechea hadi Form VI INAWEZEKANA. Tunakusanya kodi nyingi sana (trilioni kadhaa kwa mwezi!), lakini faida yake haionekani.

Jana nimeona picha ya mtu akipelekwa hospitali, hoi, kwa machela yaliyoundwa kwenye baiskeli! Halafu bado wanadai ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI na KASI ZAIDI? Za kuifilisi nchi?

Msinitie kichefuchefu asubuhi yote hii! Tena leo Ijumaa!

-> Mwana wa Haki
 


Kama bado wachanga kaeni pempeni subirini siku mkikomaa ndio tutawapa nchi
uongozi sio swala la majaribio ndugu hatuwezi kuwaamini watu wanao shindwa hata kujenga ofisi za kisha tukatumaini kujenga nchi yetu
Hayo maneno hata mtoto wa darasa la kwanza sasa hivi huwezi kumdanganya CCM imeshindwa kutawala katika nyanja zote tunataka mabadiliko,nchii tunawapa wengine sasa hivi wawe wachanga au wazee wananchi tumeamua,umeona mwenye kila kula ya maoni hata ile ya gazeti la serikali inaonyesha wananchi wameamua kaeni pembeni kidogo mutajifunza kwetu inavyowezekana kuongoa nchi yenye utawala bora na uwiano sawia kwenye huduma za msingi ,kwambie aliye kutuma kwamba hatudanganyiki
 
Nadhani bado hujawaelewa CHADEMA na itakuchukua muda mrefu kuwaelewa. Hili linatokana na ufinyu wa elimu yako, kwani inaonekana dhahiri kwamba HUKUFUNDISHWA kufanya tathmini (analysis) kwa mambo ya kiuchumi na kisiasa. Ahadi za CHADEMA zinatekelezeka. Ngoja nikupe mifano miwili tu!

1) Bunge la Jamhuri lililopita, lilipitisha bajeti ambayo ni dhahiri kwamba haikidhi mahitaji ya wananchi kutokana na ufinyu wake na upendeleo kwa matumizi yasiyo na lazima. Hili linatokana na kwamba Bunge hilo lilikuwa ni la chama kimoja, CCM, ambacho kilikuwa na idadi kubwa ya wabunge, na wabunge wachache wa upande wa upinzani. Hivyo, CHADEMA wasingeweza kufanya maamuzi yoyote yale kwa manufaa ya taifa.

2) Iwapo Dr. Slaa atachaguliwa kuwa Rais, ataweza kuunda Serikali yenye wizara chache, hivyo kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, na kupunguza kwa kiwango kikubwa idadi ya mawaziri na manaibu waziri. Chukua idadi ya mawaziri na manaibu waziri waliopo sasa, weka (kwa mfano) thamani ya wastani wa Toyota LandCruiser VX (mpya) kuwa TZS Milioni 200, kisha fanya hesabu. Kama idadi inazidi mawaziri na manaibu waziri 40, hesabu za haraka ni TZS Mil. 200 x 40 ambapo unapata jumla ya TZS 8,000,000,000, yaani, TZS Bilioni 8. Slaa ameahidi kuunda Serikali yenye mawaziri na manaibu waziri 20 tu! Kwa hiyo, ukiondoa nusu ya hao mawaziri na manaibu utapata jumla ya TZS Bilioni 4 kwa magari yao tu, hivyo tayari atakuwa ameokoa TZS Bilioni 4. Lakini hili litafanyika ENDAPO kiwango cha magari ya mawaziri na manaibu waziri kitakuwa ni Toyota LandCruiser VX, ambayo kwa kweli ni gari kubwa na ya anasa! Je, haiwezekani mawaziri na manaibu hawa kununuliwa, kwa mfano, gari zuri kama vile Toyota Rush (ambayo ina engine ndogo ya 1,500 CC na pia ni gari zuri sana), au magari mengine kama vile Toyota RAV4 model mpya? Lazima tuweke vipaumbele kwenye matumizi sahihi ya fedha za walipakodi.

Hii ni mifano miwili tu, ya mambo ambayo YANATEKELEZEKA kwa muda wa siku 100. Bunge la kwanza la Serikali mpya litakaa kikao chake Dodoma wakati huo, na sheria za kurekebisha bajeti (baada ya kuundwa kwa baraza la mawaziri na manaibu - iwapo italazimika kuwaweka - wachache, na kuwaapisha) ili tuwe na bajeti yenye TIJA, si HASARA na UFISADI!

Tuweke kipaumbele kwenye elimu, afya, miundombinu (kwa manufaa ya Watanzania wengi). Kuwasomesha watoto wetu bure, kuanzia chekechea hadi Form VI INAWEZEKANA. Tunakusanya kodi nyingi sana (trilioni kadhaa kwa mwezi!), lakini faida yake haionekani.

Jana nimeona picha ya mtu akipelekwa hospitali, hoi, kwa machela yaliyoundwa kwenye baiskeli! Halafu bado wanadai ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI na KASI ZAIDI? Za kuifilisi nchi?

Msinitie kichefuchefu asubuhi yote hii! Tena leo Ijumaa!

-> Mwana wa Haki

Mwana wa Haki, naomba unitake radhi! Ninaamini kuwa mimi ni miongoni mwa Watanzania wachache wanaosoma na kufanya tathmini makini.

Binafsi naona itawezekana lakini kuna minong'ono ambayo inaanza kupazwa sauti na CCM kuwa hayatekelezeki, ninachoshauri ni kwamba wajikite kueleza jinsi inavyotekelezeka (siyo kijumla jumla kama ambavyo wewe unafanya). Kuwepo na coounter information kuonyesha kwa kina na kwa ufasaha namna itakavyotekelezwa.

Nikupe mfano:

  • Waonyeshe Mapato na pale inapowezekana waseme hiki kwa sasa hakikusanywi kwa sababu ya ufisadi wa CCM n.k.
  • Waonyeshe matumizi yale ya sasa na jinsi ambavyo wao watabadilisha. In simple terms, naamini tarakimu zinasema zaidi kuliko maneno.
Naomba nikutoe wasiwasi kuwa kura yangu ipo kwa Dr. SLAA na mbunge wangu mtarajiwa ni John Mnyika, diwani simjui jina ila ninajua atatoka CHADEMA (Kata ya Kibamba)
 
Wameshindwa kujenga hata ofisi zao za chama tangu waanzishwe, wataweza hayao wanayo yadai kwa siku 100
Aliyekwambia CHADEMA wakiingia serikalini watatumia fedha zao ni nanai?
Unaishi wapi wewe? ....you sound like my grandma.....na yeye haelewi kama wewe.
 


Kama bado wachanga kaeni pempeni subirini siku mkikomaa ndio tutawapa nchi
uongozi sio swala la majaribio ndugu hatuwezi kuwaamini watu wanao shindwa hata kujenga ofisi za kisha tukatumaini kujenga nchi yetu

Jk amekwisha sema miaka mitano tuliyompa alikuwa anajifunza! Tumpe mingine mitano aanze/afunge kazi.
 
watatekeleza wakipata, ila wanajua hawapati sasa wao wanaahidi tu
Nani anaahidi?
1) Nitajenga uwanja wa kimataifa sijui wapi!! wa nini wakati huu wa dar hujaweza kuupanua pamoja na kukuta mipango ipo tangu enzi za Mwinyi?
2) Nitajenga barabara za juu - za nini wakati hata za chini hazipo?
3) Nitaanzisha usafiri wa trni Daslam - wa nini wakati treni za kwenda mikoani umeuza kwa washkaji wako?

SEMA SASA< NANI ANA_AHIDI HAPA! MBAYUWAYU AU KIKON'GOTA
 
Jk amekwisha sema miaka mitano tuliyompa alikuwa anajifunza! Tumpe mingine mitano aanze/afunge kazi.
Alisoma hiyo degree yake kwa kutumia madesa nini? anajifunza 5 years?
Lakini hata wasaidizi wake alipokuwa wizara ya mambo ya nje wanasema jamaa ni mvivu kupitiliza, hafanyi kitu yoyote inayohusiana na kuhusisha ubongo wake....yeye alikuwa kuchekacheka tuu! na kutania wanawake ofisini.

No wonder kubambikwa vimeo vya hotuba!! is as ubongo wake uliwekwa kwenye deep freezer then ukarudishwa kwenye kasha lake!
 
Mambo mengi kama sio yote asemayo Slaa yanatekelezeka bse kuna ela nyingi ya serikali inatumika ndivyo sivyo na kumbuka siku 100 ni miezi mitatu ukianzi ana hayo maV8 na kuishia na allowance za apa na pale unaokoa mengi.
Bado haujawabana TRA na deal zao za apa na pale na hawa watu wa Madini jamani huitaji kuwa Dr kupata ela ya kuhudumia shule na afya bure
 
Hayo maneno hata mtoto wa darasa la kwanza sasa hivi huwezi kumdanganya CCM imeshindwa kutawala katika nyanja zote tunataka mabadiliko,nchii tunawapa wengine sasa hivi wawe wachanga au wazee wananchi tumeamua,umeona mwenye kila kula ya maoni hata ile ya gazeti la serikali inaonyesha wananchi wameamua kaeni pembeni kidogo mutajifunza kwetu inavyowezekana kuongoa nchi yenye utawala bora na uwiano sawia kwenye huduma za msingi ,kwambie aliye kutuma kwamba hatudanganyiki


Nimetumwa na nani tena mbona hamjiamini, nani anaweza kuwaamini ninyi wadanganyika kwa ahadi zenu za kitoto za siku 100, hata Rome haikujengwa kwa siku moja, haya ndio mambo yanaonyesha ni jinsi gani chadema wanaropoka tu
Nahizo polls zisikudanganye kabisa, muulize Mrema na Marandu wanajua

Aliyekwambia CHADEMA wakiingia serikalini watatumia fedha zao ni nanai?
Unaishi wapi wewe? ....you sound like my grandma.....na yeye haelewi kama wewe.
Hakuna aliyesema hayo unayo yasema, issue ni kuwa mmeshindwa kuratibu kujenga hata ofisi zenu kwa hiyo ruzuku iliyokuwa inafujwa na mfanyabiashara mbowe hadi ikasababisha mkakosana na marehemu wangwe
Jk amekwisha sema miaka mitano tuliyompa alikuwa anajifunza! Tumpe mingine mitano aanze/afunge kazi.
Which means alikuwa anaweka foundation na sasa anataka kumalizia kazi yake aliyo anza miaka mitano iliyopita
 
Kuna baadhi ya maswali yalijibiwa jana na Baregu na Marando kwenye kipindi cha Tuambie Maalum, kinachorushwa na TBC1. Najua wengi wenu hamuangalii hiyo channel.
 
Kuna baadhi ya maswali yalijibiwa jana na Baregu na Marando kwenye kipindi cha Tuambie Maalum, kinachorushwa na TBC1. Najua wengi wenu hamuangalii hiyo channel.

Kweli kabisa nawashauri CHADEMA wawe na column kwenye magazeti ya Majira, Mwananchi, Tanzania Daima, The Citizen, Nipashe, The Guardian, Raia Mwema na MwanaHalisi ambayo wataitumia kufafanua ilani yao... Ijulikane kuwa ni column ya Chadema. Barack Obama alikuwa na website kwa ajiri ya kampeni, Maalim Seif naye ameizindua website hii. Hapa pangekuwa mahali safi sana kuwapata watu na kuwaelezea kwa ufasaha nini ilani inasema.

Ng'wana Diyu
 
Kila kitu kinawezekana ila IMPACT YAKE ni kubwa sana kwenye ajira za watu. Vipaumbele vikibadilishwa inawezezakana kabisa ofisi za Wakuu wa Mikoa na wa Wilaya zikawa hazihitajiki kabisa ili kupisha Serikali za Mitaa zifanye kazi zake kwa uhuru zaidi, kuna mashirika mengi yanayopata ruzuku lazini kazi zake zinaweza kufanywa kwa ufanisi mkubwa na sekta binafsi. Kubadilisha mifumo hii watu wengi sana watakuwa hawana ajira serikalini
 
Back
Top Bottom