Maswali 6 ya wazi kwa Mhe.Lukuvi!

Makala Jr

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
3,395
1,110
Mods msiunganishe uzi. Mhe.Lukuvi awali ya yote nakupongeza kwa kutoa tamko la 'serikali' kuhusu tukio la bomu lilitokea Soweto, Arusha tar.15/06/2013 ambapo CHADEMA walikuwa wakihitimisha kampeni. Mheshimiwa; Kauli uliyoitoa leo bungeni imeniacha na maswali 6 kama ifuatavyo: Umesema tukio la Soweto ni sawa na lile la kanisani Olasiti, umejuaje? Unawaambia nini waumini wa kanisa Katoriki waliokuwa wanasubiri uchunguzi rasmi ukamilike na kutolewa? Umesema wananchi waliwazuia Askari kumkamata mhalifu je, walikula njama ili awadhuru ama kuwaua kabisa? Umesema unajua tukio la Soweto ni mwendelezo wa kuchochea ukabila,ukanda,udini,uchama na rangi.Sasa kwanini unatangaza 100/= mln kwa atakayetoa taarifa unazozijua? Umetutaka Watanzania tujiulize kwanini Arusha, je tusijiulize yaliyotokea Nyololo,Iringa mwaka jana alipouwawa Mwangosi? Ulipotuhumiwa na Mhe.Chiku Abwao ulibisha, umepataje taarifa ambazo IGP Mwema hana?
 
Hivi jamani tujiulize. Wananchi walipata wapi nguvu za kuanza kuwazuia polisi wasimshike mtuhumiwa pamoja na hamaki ikiyotokea kutokana na kishindo cha bomu.
 
mmary; Kwakuwa hatujapata taarifa ya wananchi wanaodaiwa kuwashambulia polisi, je haiwezi kuwa mhusika alikimbilia upande waliokuwepo polisi?
 
Last edited by a moderator:
Abdul Mohammed; Lukuvi na Nape akili zao ni sawa huwa hawatazami walikotoka na walipo wala wanakoelekea!
 
Last edited by a moderator:
mmary; Kwakuwa hatujapata taarifa ya wananchi wanaodaiwa kuwashambulia polisi, je haiwezi kuwa mhusika alikimbilia upande waliokuwepo polisi?

Mheshimiwa Mbowe amesema mhusika baada ya kulipua bomu alichukuliwa na polisi, na tukio lile liliratibiwa na CCM, serikali na jeshi la polisi.
 
Mods msiunganishe uzi. Mhe.Lukuvi awali ya yote nakupongeza kwa kutoa tamko la 'serikali' kuhusu tukio la bomu lilitokea Soweto, Arusha tar.15/06/2013 ambapo CHADEMA walikuwa wakihitimisha kampeni. Mheshimiwa; Kauli uliyoitoa leo bungeni imeniacha na maswali 6 kama ifuatavyo: Umesema tukio la Soweto ni sawa na lile la kanisani Olasiti, umejuaje? Unawaambia nini waumini wa kanisa Katoriki waliokuwa wanasubiri uchunguzi rasmi ukamilike na kutolewa? Umesema wananchi waliwazuia Askari kumkamata mhalifu je, walikula njama ili awadhuru ama kuwaua kabisa? Umesema unajua tukio la Soweto ni mwendelezo wa kuchochea ukabila,ukanda,udini,uchama na rangi.Sasa kwanini unatangaza 100/= mln kwa atakayetoa taarifa unazozijua? Umetutaka Watanzania tujiulize kwanini Arusha, je tusijiulize yaliyotokea Nyololo,Iringa mwaka jana alipouwawa Mwangosi? Ulipotuhumiwa na Mhe.Chiku Abwao ulibisha, umepataje taarifa ambazo IGP Mwema hana?

Maswali mazuri na ya msingi.

Lakini je... unafikiri Lukuvi ana upeo wa kujibu haya maswali? Huyu, Mwigulu na Nape ni watu walioamua kujilaani kwa upumbavu wao.
Huyu Mungu ninayemjua mimi hatowaacha waendelee kuumiza umat mkubwa hivyo kwa upumbavu wao. Mwisho wao utakuwa wa aibu sana.
 
Naongezea swali la 7;
Kama kweli Polisi hawakuhusika na ulipuaji huo, kwa nini Lukuvi anakuja na kauli ya kuwatetea badala ya kuwalaumu kwa kushindwa kuimarisha ulinzi?
 
Back
Top Bottom