Mass Failure secondary ni matokeo ya Mgomo Baridi waalimu na uduni wa huduma

MPadmire

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,928
3,225
Haya madaktari waliona watu wanakufa na vigogo wanapelekwa India kwa sababu ya vifaa duni hospitali za Taifa, wakaona hapana.

Sasa kwa upande wa secondary za serikali hasa za kata, wanafunzi wanafeli sana.

Kwanza mishahara midogo ya waalimu na pia inachelewa.

Huduma mbovu, hakuna madawati, msongamano wa wanafunzi.

Maabara hakuna

Watoto wa vigogo wanasema St st na nje ya nchi.

Waalimu wanakosa morali ya kufundisha badala yake wanafikiria njia mbadala za kupata kipato.

Waalimu wengi wamekopa sacos, benki na wamefungua maduka, na wamenunua taxi.

Hivyo wanafunzi wanafeli.

Hiyo ni sawa na mgomo baridi ambao ni mbaya zaidi kuliko mgomo kamili
 
Only 9% ndo waliofaulu kwa division 1-3 na almost 90% wamepata division 4 na 0 hii mass itaenda wapi.
Kama wanafaulu mitihani ya kawaida yawezekana wanafaulu ila hawamalizi syllabus unategemea nini. Ukosefu wa walimu na lack of commitments wa walimu, serikali na wanafunzi wenyewe.
 
Kuna utata mkubwa hapa kama kweli wanafunzi wanashindwa kihalali au wanafelishwa kama ilivyokuwa zamani mtihani wa darasa la saba.Mtihani wa darasa la saba wengi walikuwa wanafelishwa sababu shule za sekondari zilikua chache then hapakuwepo sehemu ya kuwapeleka.
Leo hii shule za O level zimeongezeka lakini za Advance bado ni ndogo then hapo waweza pata jibu mkuu.Wakishinda wote kwenda Advance shule zipo za kutosha? Mfano kata yangu inashule za kata tatu wanafunzi waliohitimu ni 485 hakuna shele ya Advance,je wangeshinda wote wangeenda wapi?
Mbona sijawai sikia kuwa shule moja ya Advance asa ya serikali kuwa imekosa wanafunzi?SERIKALI INAWANGAMIZA WATU WAKE KUPITIA ELIMU HASA WALE MASKINI.Dhambi hii itawaandamana mpaka kiama.
 
Chanzo cha matokeo haya duni ajabu na ya kusikitisha ni nini hasa?

-Is it walimu(unqualified ,lack moral,or outright sabotage?)

-is it vitendea kazi(teaching aids,labs,books?)

-is it students,they have simply decided not to learn?

-is it system failure as whole kuanzia uoongozi wizara,walimu wazazi, wanafunzi kwa ujumla?

We need answers and we need them fast. This is a major crisis requires immediate attention. Ajabu sote kimya.

Just wondering kwa nini waziri wa Elimu asiwajibike?

Aibu,Aibu,Aibu and yet we are expected to compete in EA labor market. Na credentials hizi? God forbid.

On brighter note napongeza private schools Zanzibar for relatively good performance(laurate international,Zanzibar commercial,highview sec)
 
kuna utata mkubwa hapa kama kweli wanafunzi wanashindwa kihalali au wanafelishwa kama ilivyokuwa zamani mtihani wa darasa la saba.mtihani wa darasa la saba wengi walikuwa wanafelishwa sababu shule za sekondari zilikua chache then hapakuwepo sehemu ya kuwapeleka.
Leo hii shule za o level zimeongezeka lakini za advance bado ni ndogo then hapo waweza pata jibu mkuu.wakishinda wote kwenda advance shule zipo za kutosha? Mfano kata yangu inashule za kata tatu wanafunzi waliohitimu ni 485 hakuna shele ya advance,je wangeshinda wote wangeenda wapi?
Mbona sijawai sikia kuwa shule moja ya advance asa ya serikali kuwa imekosa wanafunzi?serikali inawangamiza watu wake kupitia elimu hasa wale maskini.dhambi hii itawaandamana mpaka kiama.

kwanza naomba nikusahihishe hakuna mwanafunzi alikuwa anafelishwa zamani,bali kulikuwa na kuchaguliwa wala si kufaulu,pili mimi si msemaji wa baraza la mitihani lakini napenda nikufahamishe kwamba walimu wanafanya kazi ya kusahihisha kufuata muongozo na kwa uzalendo sana hakuna kuonea au kupendelea mtu,unapata ulichopanda,ila mgomo wa walimu ni wa siku nyingi sana afadhali wa madaktari,who cares ?watanzania ni bishoo mnajifanya mna pesa kupeka watoto wao shule st. St. Nchi hii msishangae majina ya viongozi wa nchi,mashiraka ya umma na taasisi mmbalimbali yakawa yanajirudia yale yale kwa saqbabu ndiyo wanaosoma walala hoi ni mizero tu,tanzania wake up tuokoe elimu ya nchi
 
Mbona majibu yako wazi, tukisema waziri au uongozi wa wizara uwajibike ni kuwaonea. Watajiuzu wangapi? Ninachokiona watumishi wa umma work morali imeparalize completely. Kupata leseni ya biashara utazungushwa mpaka basi, polisi anaetoa pesa nyingi ndo anaesikilizwa, sheria zinapindishwa,nenda ardhi kutafuta hati, fuatilia kuunganisha umeme tanesco, sajili kampuni uone mziki-wandugu tunapoteza vision as a nation kitakachofuata ni total colapse of public services sehemu ambayo inagusa wananchi wengi wa kawaida
 
Kufeli wanafunzi wengi wa o level hakuwagusi serikali kwani tayari wamepunguza idadi ya watakaojiunga A-level na hata kupunguza idadi ya watakaojiunga na elimu ya juu. Nikuwepo kule Hanang kwa Mh. Mary Nagu shule za makao ya wilaya imeanza na div. three kwa mfano Katesh sec. {Div.iii-8, iv-47 na 0-57} na Ganana sec.{div. III-3, IV-44 na o-27} shule mbili hizi ziko makao makuu ya wilaya, hivi ikiwa shule zimeshindwa kufaulisha hata 50% ya wanafunzi wanaohitimu, wakuu haitoshi kutafuta chanzo cha tatizo? Hao zaidi ya 50% waliobaki mtaani unadhani watafanya shughuli gani iliyo halali kwa Hanang na hata kwa Tanzania nzima?
 
watoto tu wasiku hizi vichwani hamna kitu wenye akili zetu tushaga maliza
 
Only 9% ndo waliofaulu kwa division 1-3 na almost 90% wamepata division 4 na 0 hii mass itaenda wapi.
Kama wanafaulu mitihani ya kawaida yawezekana wanafaulu ila hawamalizi syllabus unategemea nini. Ukosefu wa walimu na lack of commitments wa walimu, serikali na wanafunzi wenyewe.
Mkuu, hizi stats ni za kweli hizi??? Halafu tuna waziri wa elimu, makatibu wa wizara ya elimu, maafisa elimu, waalimu wakuu... hawa wote wanaendelea na 'kazi' bila wasiwasi kabisa!!! Jamani taifa hili linahitaji mwanajeshi kuruta au mtu kutoka nje kabisa ya system alirejeshe kwenye msitari. 9% div 1 - 3 ????
 
Hahaa...walioandika bongo flavour wamenikumbusha kanuni moja kama hujui unachotakiwa kufanya basi fanya unachojua!
 
Back
Top Bottom