Maslahi ya Taifa ndiyo nini?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Siku za hivi karibuni kumekuwa na matumizi ya maneno hayo kuwa tunafanya jambo fulani kwa "maslahi ya Taifa" au watu fulani hawakufanya jambo fulani kwa "maslahi ya Taifa" n.k Kilele cha matumizi ya neno hilo ni madai ya Machunde wakati wa kujitoa kwenye Kamati ya Madini kuwa "wote tunajali maslahi ya Taifa" na hivyo isionekane kuwa wapinzani peke yao ndio walinzi wa haya "maslahi ya Taifa".

Sasa nimebakia najiuliza maswali kadhaa kuhusu hili dubwasha linaloitwa "maslahi ya Taifa" na majibu yake yatanisaidia kuandika makala yangu ya Jumatano. Na kama kawaida nayakaribisha mawazo yenu kwenu ninayo majibu yangu kuhusu maswali haya ila ningefurahi kujua majibu yenu kwani vichwa vingi ni bora kuliko kimoja (in certain cases anyway).

a. Maslahi ya Taifa ni nini?
b. Tunaweza kutambua vipi kitu au jambo fulani ni la maslahi ya Taifa?
c. Je maslahi ya Taifa yaweza kuwa sawa na maslahi ya kundi fulani la watu?
d. Je tunaweza kuhakikisha vipi kuwa watawala wanafanya mambo kwa maslahi ya Taifa?
e. Je mtu aweza kuwa mzalendo wa kweli bila kuweka mbele maslahi ya Taifa?
f. Je maslahi ya Taifa yakitishiwa ni jukumu la nani kuyalinda?
g. Je maslahi ya Taifa ni kitu kile kile na Taifa la Maslahi?
h. Je mtu anaweza kufanya kazi au utumishi wa umma au binafsi bila kujali maslahi ya Taifa na akawa mtumishi mzuri?
 
MKJJ,
maslahi ya taifa (national interest/ public interest) could be equated with a word that is not very much in circulation these days and that is 'manufaa ya umma', umma being an arabic word meaning masses. therefore literary speaking maslahi ya taifa is a relative term..the opposite of which is maslahi ya mtu binafsi ama kikundi cha watu.

kwa mfano katika public interest litigation, hasa hasa zile zinazohusu uchafuzi wa mazingira, public interest imetafsiriwa kumaanisha walio wengi! siku hizi hatusikii wale watu ambao mwalimu alikuwa 'akiwastaafisha kwa maslahi ya umma'... hapa inamaana kuwa kazi waliyokuwa wanaifanya ilikuwa ni kujineemesha wao, na kama sio wao binafsi basi taifa lilikuwa halineemeki kwa wao kuendelea kubaki kazini! kwa maana nyingine wao kuachia ngazi ni neema kwa taifa!
chukulia issue ya rada. kikundi cha watu kinasaini mkataba, ambao taifa linaingia hasara lakini wao wanawekewa chao kwenye accounti za siri geneva. hapo ni maslahi binafsi zaidi kuliko taifa!
kuna miongozo katika utumishi wa umma ( nawapongeza watanzania ambao wamewahi kutunukiwa shahada za 'utumishi wa umma uliotukuka')..enzi hizi za kupeana takrima sijui kama kuna kutukuka katika utumishi!

hapa UK kuna miongozo ya namna watumishi wa serikali wanavyopaswa kufanya iwapo watapewa zawadi ama kukirimiwa. zawadi binafsi ilitakiwa isizidi pauni 50, zaidi ya hapo lazima u declare.(akipwa mkeo, mwanao nayo pia imo)..ukishindwa hatua za kinidhamu zitafuata!hii ilikuwa ni katika juhudi za kudhibiti watumishi wa umma wasiwe na tamaa, kwani wakendekeza wanauza nchi.
Ndio maana kuna masharti ya kutaja mali za viongozi/watumishi wa umma. Na kama una miliki hisa katika kampuni inabidi uziachie (karamagi huyo!)kwani lazima kutakuwepo na 'mgongano wa kimaslahi'. je unategemea pale kwetu bongo tume ya maadili ya viongozi inaweza kufuatilia mambo haya? kama vyombo vingine vya dola Tanzania, tume hii ipo kulinda maslahi ya viongozi na siyo maslahi ya Taifa. Ndio maana hawa jamaa wanauza nchi bila kusikia uchungu wala kuona aibu!!

So the measure of public interest could be expressed as whenever for all intents and purposes in the estimation of a 'reasonable person'the end result of a process, procedure or transaction is without doubt to the benefit of the public at large and any benefits accruing to individuals in the course of such transactions is for the benefit of the public at large!
 
Prince, naona umeanza mjadala vizuri kweli; ina maana maslahi ya umma (walio wengi) ni lazima yawe ndiyo maslahi ya Taifa? Je maslahi ya wengi hayawezi kwenda kinyuma na maslahi ya Taifa?
 
MKJJ
maslahi ya wengi kwenda kinyume na maslahi ya taifa hiyo nayo imo! but it is subject to time limitations.kwa mfano kuna baadhi ya nchi hapa duniani 'vyama vya wafanyakazi..kwa maana ya labour unions' vina nguvu kubwa sana and they most often hold the entire economy hostage kwa kudai mishahara ya juu, likizo kede kede na marupurupu mengine ambayo huongeza cost of production/providing service and making the entire economy uncompetitive. This is what happened in the UK wakati wa Thatcher na hata Blair alipoigia madarakani, the New in New Labour meant kuachana na utegemezi wa vyama vya wafanyakazi. Leo hii marekani inabakia kuwa taifa pekee kubwa ambalo halijasaini mkataba wa Kyoto, kisa utapelekea kupoteza mamilioni ya nafasi za kazi! mbona siyo hivyo kwa nchi zingine zenye viwanda??these other countries are now leading the technology in the green revolution which is creating millions of jobs!!!
Ujerumani wakati wa Third Reich ni mfano wa taifa ambalo maslahi ya wengi yalikuwa kinyume na maslahi ya taifa. Ni kweli kwamba siyo wajerumani wote walikuwa bega kwa bega na Hitler lakini pia ni dhahiri kwamba wengi wao walimuunga mkono..na ndio maana mwanzoni alifanikiwa sana! Lakini mwisho wake ujerumani kama taifa lilipata hasara!!!
Ni dhahiri shahir kwamba siyo lazima mara zote maslahi ya wengi yakawa ni maslahi ya taifa pia!!!
 
MKJJ,

Kwa neno moja malahi ya taifa yanaweza kuwekwa kama ustawi wa jamii. Kwa maana ya kwamba yeyote anaifanya jambo lolote lenye kuleta tija kwa jamii kwa jumla basi ni maslahi ya taifa. na Jamii nayo ina makundi(wanawake, watoto, wanaume, Vijana, wazee,n.k) so kama mtu anafanya jambo kwa kulenga kundi fulani kwenye jamii bila kubagua kwa dini, rangi, kabila, cheo n.k) basi hilo jambo lina maslahi ya taifa specifically kwa kundi husika. naamini maelezo haya yanajibu maswali meningine yote but one.

Nalo ni mtu anayefanya kazi Mfano muuza madawa ya kulevya akapata faida kubwa na kutoa misaada kwa jamii bado hajali mslahi ya taifa maana anaangamiza na kudumaza akili za wanajamii so hata kama ni mchapa kazi bado unaweza kujeopadize maslahi ya umma so anakosa sifa ya kujali maslahi ya taifa/umma
Nawakilisha
 
ok.. hebu endeleeni na sehemu ya hayo maswali mengine.. mmenipa definition nzuri ya Maslahi ya Taifa...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom