Sarah Simbaulanga: Mwanamke wa kwanza kuiba pesa ndefu katika historia ya benki zote nchini

Embu tupe data kidogo Mkuu...sijui km namfaham sana so far as navyojua ni mwanamama aggressive aliyetumia kalamu yake vizuri kuiibia serikali!...sina hakika na kumbu kumbu zangu!

My point exactly...

how did we get to this ?, Hivi wizi ni miaka gani ilianza kuwa Sifa...., kweli inabidi tubadilike na tuone wizi ni wizi na hakuna sifa ya kuwa mwizi.
 
Huyu wakati ule akitoroka alitumia pia jina la bandia la Khadija Alli Mkimbau, nakumbuka jinsi tulivyokuwa tukiifuatilia ile kesi yake, ni TAifa zima liliguswa, sijui kama hali ya mioyo ya waTanzania itarudia kipindi kile
 
pasco,
Mbasi yale yalikuwa ni SWARAJ MAZDA Mzee....alinunua mengi mno....huyu mama alikuwa mwizi mkubwa lakini kumbuka kwamba kuna wizi mkubwa sana ulishafanyika pale NBC Ila kwa sababu watu walikuwa wanakula na viggo akina Marehemu Nsekela walivumiliwa tu.

Tuliokuwa NBC nadhani tunakumbukumbu nzuri jinsi matawi ya MASDO House na NBC Chalinze yalivyokwapuliwa pesa hadi yakafungwa...so was a bad moment to remember lakini unatukumbusha udhaifu wetu ulivyoanza siku nyingi.
 
Mwanakijiji

Asanye sana kwa kutukumbusha Kesi ya Huyo Mama na nikilinganisha na Kesi Ya sasa Hivi (tena ya Moto) ya Mwasibu wa Tanesco Aliyeiba Billion 1.3 Tzs.

Hv Unataka kuniambia Huyu Mwasibu kaiba Peke yake? KWELI....tehe teh tehe tehe tehe

Tupe mambo Mwanakijiji na Big Up sana
 
nakumbuka vizuri wakati wa kesi ya mama huyu nilikuwa kati ya darasa la 2-3 maana alikuwa topic kwenye magazeti ya Uhuru ila kaja kutoka miaka 6 baadaye kwa msamaha wa Rais, nafikiri wakati ule bado viongozi wa kitanzania walikuwa na "socialistic hearts"

maana halisi ya soft hearts kwani tamaa mbaya hazikuwepo sijui ni kwasababu ya Mwalimu hivyo walikuwa na idhamu ya woga au la!! Maana siku hizi hawa viongozi have "pure capitalistic hearts" and Mwalimu is no more ohoooo life is good to them. Ndio sababu inatubidi sisi wananchi tuvalie njuga haki zetu wenyew, MWANZO MWISHO
.:clap2:
 
MTM,

Nakumbuka nilisoma na mtoto wake wa kike shule ya secondari kibiti, miaka ya 90' , Yaani watu walikuwa wanaongea chini chini, huyu mnamuona ni mtoto wa simbaulanga, Kwa kuwa mie nilikuwa mwanafunzi kutoka bara na kijijini ndani ndo nilisikia historia ya simbaulanga
 
Hakufanya jema mkulu , huyu mama alikuwa mwizi,aliiba, aliiba fedha nyingi, alikuwa pale NBC Foreign branch sasa hivi ni makao makuu ya NMB Post mpya.Alishirikiana na kijana mmoja wa kiarabu jina lake nimesahau kigodo.Back then ilikuwa fedha nyingi approximately 60ml

Alishirikiana na Toroha Mohamed Toroha. Jina lingine huyu dada aliitwa Hadija Ally Kimbau
 
.. kwanini tulikuwa very serious wakati ule..? Leo kuna mama mwingine anatuhumiwa kuiba bilioni 1.3 na hakuna watu wanaoshtuka!

Mabadiliko ya kisera yameleta yote haya Mkuu.Enzi za mwalimu za Ujamaa na kujitegemea, enzi za Azimio la Arusha watu wakikaririshwa Rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa mtu aliyeweza kwenda kinyume basi huyo hakuwa binadamu wa kawaida.Azimio la ZNZ LILIPOFUTA Azimio la Arusha ikawa kama vile Adam alivyokula tunda dhambi ikaingia duniani!
mimi binafsi nilimchukulia Sara Martin Simbaulanga kama mtu hatari sana hasa ukizingatia magazeti ya wakati ule yalivyokuwa yakiripoti habari ile. .
HAKUNA jinsi ungeacha kumchukia maana alifanya kitu cha ajabu kinyume na mtu wa kawaida...ni kama leo usikie jirani yako kamchinja mwanaye kama kuku!
Mkuu Heshima yako,
Una kumbukumbu nzuri sana juu ya kesi ile, Sara na mumewe Toroha walitoka nadhani kwa msamaha wa rais, walikuwa wanaishi kule Kawe Mzimuni, mumewe nadhani alifariki kama sikosei mwaka juzi.
Toroha hakuwa mume wa Sra bali mshkaji tu,.. mumewe ama walitengana au kuachana

Nakumbuka kama huyu mama alikuwa na uhusiano na Jamaa fulani ambaye alimpa yale madola.
Huyo jamaa ndio alimponza Sara kama leo akina papa Msofe wanavyojua kuwavuta karibu wale wanaojua watawasaidia kukamilisha deals.Mkaka alicheza na saikolojia ya Sara tu ... kumwona ana matatizo ya ndoa hivyo akijifanya anampenda kumbe ana ajenda yake.
Mastermind alikuwa marehemu TOROHA MOHAMED TOROHA huyu mama alikuwa 'inside person'
Haswa! SARA alikuwa kiwezesho tu!

Wengi walichosahau ni the love story behind yule mdada aisee..
Haikuwa genuine love bali opportunity kwa mkaka Toroha! Ndio tatizo la kuingia kwenye mapenzi ukiwa na matatizo.Huwezi kufikiria vizuri na hapo ndipo unajikuta umeruka majivu ukakanyaga moto!

Phillemon Mikael,
30.M MIAKA YA 1980/90 si mchezo! Walikamatiwa Jacaranda hotel Nairobi walikojificha baada ya msako mkali!

Mtizamo na fikra kuhusu uhalifu vimebadilika.Siku hizi mwizi/fisadi ni shujaa!

Hapo sasa watasikitika kweli! Na ndio maana siku zinavyoenda ukubwa au kiwango cha wizi kinaongezeka maana ni mawili - uibe kidogo ushindwe kuhonga mlolongo wa sheria - uishie jela au uibe kikubwa uweze kununua uhuru wako na heshima yako!
 
Nilisoma darasa moja na mtoto wake wa kiume pale Mwenge primary school wilaya ya kinondoni, dada yake alikuwa darasa la juu yetu.

Mama alipokwapua fedha ilikuwa shock kweli pale shuleni kwani pia alitoroka na wane wawili ambapo kabla ya kukamatwa nairobi walikwenda kula nchi Ujerumani kipindi cha baridi kisha wakarejea nairobi mpaka walipokamatwa.

Baada ya kukamatwa, wanae walirudi shuleni na kumalizia masomo yao ya awali. Dada mtu alikuwa anaona aibu na kujistukia sana ila mdogo mtu ndo alikuwa chakaramu na kutusimulia kila matanuzi waliyoyafanya....Walikuwa wanaishi maeneo ya Kawe kama sikosei.

Baadhi ya magari yao yalizuiliwa pale central police na sijui yaliishia wapi maana ni kitambo kweli kimepita.
 
Kwa hiyo humjui ATHUMANI MAUMBA wa 1987 pale mnazi mmoja?....fataki la wakati huo kaka

Nakumbuka kesi ya Maumba yalitajwa mafuta fulani ya mgando aliyokuwa anatumia kwenye shughuli yake, basi yale mafuta ukinunuliwa nyumbani kwenda nayo boarding skuli unaona noma kishenzi!-yale mafuta kama kuna mtu anayakumbuka tafadhali
 
Back
Top Bottom