Elections 2010 Maskini Karagwe

Igabiro

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
242
27
Kuna tetesi kuwa karagwe CCM wamechukua jimbo, hii ni baada ya kijina wa CHADEMA aliyekuwa akiongoza kwa tofauti ya kura 500+ kukubali kurudia kuhesabu kura, hii inatokana na Mh. wa zamani (Sr. Kahama) kumuaidi (pleadge) kiasi cha 200Millioni ili hata akishindwa apoze machungu. Hii ni very sad. Ilitakiwa aige mfano wa Mrema wa Arusha mjini yeye alisema kura hazihesabiwi upya labda kama Mungu anashuka.
 
Acheni umbeya jamani. Nimekuwa hapa tangu day one ya kupiga kura.
Hakuna cha mtu kuhongwa hapa, bali uchakachuaji wa system tu ndio umezamisha jahazi la Chadema.
Leo asubuhi waliletwa maafisa watendaji wa kata wote na kuulizwa kura za Blandes kutoka kila kata.
Walizotaja ni tofauti na zilizojazwa katika fomu ya msimamizi wa uchaguzi. Yaelekea syetms ilichakachua formu za msimamizi na kuingiza nyingine mpya zenye figures za kumsaidia Blandes.

Msiwakatishe tamaa watu, hakuna aliyehongwa katika Chadema, labda kama kahongwa msimamizi ili aruhusu system kuchakachua.
 
Kwahiyo unaona hao CCM wanaohonga kama unavyosema wanfaa kutuongoza.Tume ya uchaguzi iliandaliwa kuipa ushindi CCM kwa gharama zote.
 
CHADEMA wangekuwa na njaa, Lema angekuwa wa kwanza kuchukua bil.3 za EL vs Batilda.
Watu wa Arusha tulikomaa kuwa hakuna kura kuhesabiwa tena.
Hicho kilichofanyika Karagwe ni uhuni wa CCM na Mzee Kahama.
 
Hakuna uwanja sawa wa ushindani katika uchaguzi huu.Tume inaripoti Ikulu unategemea nini?
Pale ambapo vyama vingine vimeshinda hususani Chadema ni kwa sababu nguvu ya umma ilikuwa kubwa.
Haya mambo ya kuhongwa ni propaganda tu maana nimesikia kuwa kilombero G.S amehongwa million 200,huku nako million 200,inakuwaje figure zifanane?Hamjui hata kudanganya,kweli nyie mabogas.Huu ni mpango wa kukichafua chama,kamwe hautafanikiwa.
 
Kuna tetesi kuwa karagwe CCM wamechukua jimbo, hii ni baada ya kijina wa CHADEMA aliyekuwa akiongoza kwa tofauti ya kura 500+ kukubali kurudia kuhesabu kura, hii inatokana na Mh. wa zamani (Sr. Kahama) kumuaidi (pleadge) kiasi cha 200Millioni ili hata akishindwa apoze machungu. Hii ni very sad. Ilitakiwa aige mfano wa Mrema wa Arusha mjini yeye alisema kura hazihesabiwi upya labda kama Mungu anashuka.

Mtu yeyote mwenye taarifa za uhakika kuhusu uchakachuaji huu? Maana kama hali itaendelea hivi inaelekea CCM wamepanga kuhakikisha majimbo yote yaliyosalia yanaangukia mikononi mwao.
 
kuna watu knye hiki kijiwe chetu wametumwa na mafisadi tuwe makini nao sana, wanaleta habari za umbeya
 
kuna tetesi kuwa karagwe ccm wamechukua jimbo, hii ni baada ya kijina wa chadema aliyekuwa akiongoza kwa tofauti ya kura 500+ kukubali kurudia kuhesabu kura, hii inatokana na mh. Wa zamani (sr. Kahama) kumuaidi (pleadge) kiasi cha 200millioni ili hata akishindwa apoze machungu. hii ni very sad. Ilitakiwa aige mfano wa mrema wa arusha mjini yeye alisema kura hazihesabiwi upya labda kama mungu anashuka.

source please
 
Kudadadeki, karagwe kwishnei, chadema tunajapinga upya kuanza na wave nyingine ya mashambulizi, aluta continua
 
Mbea mkubwa au ni wale nduguze wameteuliwa na JK,jina lako tumeliona
maana ww unabariki ufisadi
 
kweli kijiwe kimevamiwa tuwe macho na wanajamii ambao wametumwa na mafisadi kutuharibu. lakini sisi tunasema hatudanganyiki hivyo vibia na vichips wanavyohongwa shair zao. hiki sio kijiwe cha ccm tafadhalini mliotumwa na mafisi ya ahadi
 
Karagwe wanasema wanatokomea migombani sasa. Wakiibuka watastrike. Hakuna kulala
 
Hakuna uwanja sawa wa ushindani katika uchaguzi huu.Tume inaripoti Ikulu unategemea nini?
Pale ambapo vyama vingine vimeshinda hususani Chadema ni kwa sababu nguvu ya umma ilikuwa kubwa.
Haya mambo ya kuhongwa ni propaganda tu maana nimesikia kuwa kilombero G.S amehongwa million 200,huku nako million 200,inakuwaje figure zifanane?Hamjui hata kudanganya,kweli nyie mabogas.Huu ni mpango wa kukichafua chama,kamwe hautafanikiwa.


Hawa nao wameshirikiana na CCM kuchakachua ......... the-the-the...

WAANGALIZI wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu uliofanyika Oktoba 31,kutoka Jumuiya ya Ulaya ( EU EOM) na Umoja wa Afrika wamesema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa huru na haki, utulivu na amani.

Waangalizi hao walitoa kauli hizo kwa nyakati tofauti wakati walipofanya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana(leo) kuhusu taarifa ya awali ya uchaguzi huo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mwangalizi Mkuu wa EU EOM, David Martin alisema uchaguzi huo ambao ni wa nne kufanyika nchini tangu mfumo wa vyama vingi kuanzishwa Tanzania, hadi sasa kwa ujumla umefanyika kwa amani na mpangilio mzuri.

" Siku ya Uchaguzi Mkuu ilijitokeza kwa utulivu mkubwa na kwa ujuml a waangalizi wa uchaguzi wa Ujumbe Maaalumu wa Jumuiya ya Ulaya(EU EOM) ulikadria mchakato mzima wa uchaguzi huo kuwa ama ulikuwa ‘mzuri' au ' kuridhisha' katika asilimia 95 ya vituo vyote vya kupigia kura walivyovitembelea upande wa Tanzania Bara na upande wa Zanzibar," alisema Martin.

Aliongeza kuwa kwa ujumla taratibu muhimu katika vituo vya kupigia kura zilitumwa kwa ulinganifu kwa kila kituo cha kupigia kura nchini kote, licha kuwepo mapungufu machache.

Martin alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) zilisimamia chaguzi kwa namna ya kitaalamu, hivyo kwa sehemu kubwa ziliwapatia watu watu wote haki ya kupiga kura.

Aliongeza kuwa ujumbe huo utabakia nchini kuzidi kufuatilia kwa karibu zaidi zoezi la kuhesabu matokeo ya uchaguzi, utangazaji wa matokeo na matukio yoyote yatakayojitokeza baada ya uchaguzi.

"Taarifa hii ni ya awali .Taarifa ya kina ya mwisho itatolewa baina ya miezi miwili na miezi mitatu baada ya mchakato mzima wa uchaguzi kukamilika," alisema.

Kwa upande wake Kiongozi wa waangalizi hao, kutoka AU, Rais wa zamani wa Jamhuri ya Sierra Leone, Dk. Ahmad Tejan Kabbah alisema uchaguzi huo umefanyika wa amani na umefanyika kwa mujibu wa sheria za uchaguzi wa Tanzania .

Aliongeza kuwa umefanyika kwa kuzingatia Azimia la Durban Demorasia katika Chaguzi za Afrika la Julai mwaka 2002.

" Waangalizi wa Umoja wa Afrika wamesema uchaguzi umefanyika kwa huru, haki , uwazi na uadilifu(Credible)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom