Special agent.
Senior Member
- Aug 25, 2015
- 101
- 71
Kila mbinu waliyopanga kutumia ili washinde uchaguzi huu imebuma, sasa hivi wamebaki na vita ya wao kwa wao tu, kila mtu ndani ya CCM hamwamini mwenzake. Hebu fikiria mtu kama Mwigulu ni wa kutiliwa shaka kweli? Kumtilia shaka Mwigulu kuwa anaihujumu CCM ni sawa na kumtilia shaka chui eti kaiba majani ya mbuzi!
Ndo maana siku hizi hata yule kiherehere wa CCM humu jamvini mwenye jina la dawa kali inayotibu magonjwa sugu ya zinaa na kuua Bacteria wa aina tofauti haonekani akipayuka payuka maana tayari ameshajua ukweli kuwa CCM haitoboi na tayari makada wake wazito wanajiandaa kuja UKAWA.
Picha halisi itachezwa baada ya baraza la mawaziri kuvunjwa hapo ndo CCM inaenda kufa yote rasmi.
Habari za uhakika kutoka chini ya kapeti nilizonazo ni kuwa vigogo wengi wa CCM wapo kama kivuli tu ndani ya chama hicho na wengi wao wapo ili kuiba siri na kuzipeleka UKAWA. Ndio maana kila kikao wanachokaa na kupanga mikakati ya ushindi asubuhi yake UKAWA wanakuwa na mkanda mzima!
Poleni CCM, lenye mwanzo lina mwisho.
Ndo maana siku hizi hata yule kiherehere wa CCM humu jamvini mwenye jina la dawa kali inayotibu magonjwa sugu ya zinaa na kuua Bacteria wa aina tofauti haonekani akipayuka payuka maana tayari ameshajua ukweli kuwa CCM haitoboi na tayari makada wake wazito wanajiandaa kuja UKAWA.
Picha halisi itachezwa baada ya baraza la mawaziri kuvunjwa hapo ndo CCM inaenda kufa yote rasmi.
Habari za uhakika kutoka chini ya kapeti nilizonazo ni kuwa vigogo wengi wa CCM wapo kama kivuli tu ndani ya chama hicho na wengi wao wapo ili kuiba siri na kuzipeleka UKAWA. Ndio maana kila kikao wanachokaa na kupanga mikakati ya ushindi asubuhi yake UKAWA wanakuwa na mkanda mzima!
Poleni CCM, lenye mwanzo lina mwisho.