Masikio yangu yote yametoboka ngoma

Nimekuelewa vizuri sana, na kwa uhakika umekwenda Ekenywa kwa Dr Ole kama sikosei.
Naomba tuwasiliane offline ili tuangalie namna tunavyoweza kusaidiana.

Ahsante
 
Nimekuelewa vizuri sana, na kwa uhakika umekwenda Ekenywa kwa Dr Ole kama sikosei.
Naomba tuwasiliane offline ili tuangalie namna tunavyoweza kusaidiana.

Ahsante

haswaa umenikumbusha dr ole yupo magomeni.
 
Nimekuelewa vizuri sana, na kwa uhakika umekwenda Ekenywa kwa Dr Ole kama sikosei.
Naomba tuwasiliane offline ili tuangalie namna tunavyoweza kusaidiana.

Ahsante

haswaa umenikumbusha dr ole yupo magomeni.
 
HABARI ndugu zangu mimi ninamatatizo ya kusikia ngoma zimepasuka nimehangaika sana kutafuta tiba lakini wapi.ninamshukuru mungu wakati nimeanza kuugua nilikuwa kidogo ninapesa hivyo nilizunguka sana katika hospitali zote kubwa na ndogo,sikuwa na shida na pesa ila shida yangu ilikuwakupona masikio lakini hamna kitu mpaka nikaamua kununua mashine ya masikio. sasa je ninaweza nikaja nikasikia tena ?au ndo SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA? nipeni data wazee.

Kama utakwenda CCBRT waulize kama wanafanya huduma hii:Tympanoplasty (Repair of Perforated Ear Drum)

Bofya hapa Eardrum Problems, Perforated Eardrum, Ear Tubes Tampa Bay & Pediatric ENT
 
pole sana mkuu kwa hayo matatatizo
Kutokana na maelezo yako, sidhani hiyo quinine ndio iliyosababisha hayo, nadhani hiyo kazi yako uliyokuwa unaifanya mwanzo (Drilling), inaweza kuwa ndio chanzo kikuu cha wewe kupata matatizo hayo ya masikio, nadhani kutokana na mazoea ya hiyo kazi ulikuwa unajiexpose kwenye kelele bila kuwa na protection ya kutosha, inawezekana kuwa ngoma hazijapasuka ila inawezekana kuwa ndio umepoteza uwezo wa kusikia moja kwa moja

Kwa faida ya wengine wanaofanya kazi kwenye mazingira ya kelele,
-kwanza ni muhimu kupima kelele zinazotoka kwwenye mashine au kifaa unachotumia
- pili inakupasa kujua kutokana na hizo kelele wewe inakupasa ukae hapo (Ukifanya kazi ) kwa muda gani? (hipo chati inayoelezea kiwango cha kelele na muda ambao mtu anapaswa kuwepo hapo)
kama kuna ulazima wa wewe kuwepo hapo (kwenye kelele) kwa muda mrefu, basi inakupasa kuvaa PPE (personal protective equipment), na kwa kesi ya masikio hapa tunazungumzia EAR plugs na EAR Muff
hapo katika uvaaji wa hivyo vifaa ndipo kunakuwa na tatizo la kutojua ufaeje na maada ya kuvaa ukae kwenye kelele kwa muda gani
uwezo wa ear plug na ear muff kukinga kelele unaandikwa NRR, sasa ukona NRR 30, basi ujue hicho kifaa chako kinauwezo wa kupunguza kelele kwa kiwango hicho cha 30dB

hapa huwa zinaenda hivi
mfano
kama mashine yako inagenerate 50dB za kelele ambazo zinakupasa kuwa hapo kwa lisaa limoja tu, kwa hiyo utakapo vaa ear plug inayosoma NRR 30, inamaa unaweza kupunguza hiyo kelele kwa 30dB hivyo hiyo mashine yako itakuwa inakupa kelele zenye kiwango cha 20dB ambazo unaweza kukaa say masaa mawili mpaka na nusu, lakini unapozidisha tena kukaa say 12hrs lazima utaathirika

kutosikia kunakosababbishwa na kelele haiji siku moja, unaweza kupata madhara hayo hata baada ya miaka kadhaa baada ya kuacha kazi
 
Mheshimiwa saana kwa tatizo lako unaweza kuwaona wataalamu wakakuweka viwambo bandia na ukawa sawa kabisa yaani namaanisha wataalamu wa Pua,sikio na kichwa.
By the way Pole saana mkuu.
 
poa natamani upone haraka mkuu yes nilihisi hlo 2lipoonana pole sana mkuu

nikweli dr bila shaka uliniona ninavyo cheza na mdomo wa mtu anaeongea na mimi.maana mtu akichengesha tu mdomo simpati. HUJAFA HUJAUMBIKA.
 
kaka nguvuri3 kwanza nashukuru kwa kunifariji pili kwa ushauri wako juu ya kuonana na mabingwa .mkuu pia umesema Ningependa kufahamu sababu zilizopelekea masiko yako kutoboka. Je umewahi kuwaona wataalam wakathibitisha kuwa ngoma zimetoboka? [ Eardrum perforation].Pili unapotumia mashine unazosema, je hali inakuwaje katika usikivu. mkuu mimi ninahisi sababu zinaweza kuwa mbili kuu 1 nimewahi kufanya kazi kwenye mazingira ya kelele kama driller sehemu ambayo ilikuwa inalipua miamba kwa baruti 2niliwahi kuugua TB ambapo madaktari hawakuishitukia mapema wakawa wananitibu maralia kwakuwa sasa sikuwa napata nafuu waliamua kunichoma quinini ambazo ndo ziliniziba masikio hivyo nikawa sisikii tena. kuhusu mabingwa wa masikio nimeonana nao zaidi ya watano .bugando mmoja,muhimbili mmoja,ekenwa dispnsr mmoja,murugwanza mmoja,kahama hospital mmoja (huyu alikuja toka kenya) kifupi wote walikuwa wananipa moyo sana na nilijitahidi mno kuhudhulia kiliniki. vipimo vyao vilionyesha kwamba ngoma zimetoboka na sikio la kushoto linasikia kwa 20% huku jingine linasikia kwa 10%ningekuwa mtoto mdogo wangenipasua kisha wazibe ila kwa kuwa mimi ni mtu mzima haita saidia.wakanipa mfano mtu mzima akivunjika mguu kuunga huwa ni kazi ngumu sana. kuhusu hii mashine ninayoitumia nashukuru inanisaidia ila wakati mwingine huwa inazimika tu nakaa hata siku tatu siendi kazini kwakuwa sisikii na kazi zangu ni za ufundi hivyo wateja wangu ili wakupe kazi mpaka msikilizane mkubaliane. mashine yenyewe inauzwa bei ghari sana hivyo kumudu kununua mashine ingine kama spea ni kazi. kumbuka ni miaka mitatu tu iliyo pita tangu nipate tatizo hili. nashukuru kwa kunisoma.
Mkuu NA Mimi nilipata ukiziwi kutokana NA sababu ya kuugua Malaria Kali na kupigwa dawa ya QUUININE na nilishawahi kupewa machine za usikivu lkn kwa BAHATI mbaya zilinisaidia kusikia SAUTI tu na sio kuelewa kwahiyo niliacha kuzitumia sababu tatizo lilionekana ni NEVA/mfumo Wa fahamu na sasa naendelea kupambana na maisha name nishaizoea hali hii na kujikubali
Usikate tamaa
 
nashukuru sana mkuu, ndugu usiombe hili tatizo limpate mtu ukubwani afu awe hana pesa ya kununua hiyo mashine.nikikumbuka mimi ilivyo nikuta nusu nife kwa mawazo nikakonda sana maana duniani nilikuwa najiona nipo peke yangu sina wakuongea nae hata ile lugha ya viziwi siifaham yaani nikajikuta nawachukia watu wote maana nilikuwa nikiwaona wanaongea nahisi wananiteta mimi.
Mkuu jisikie kawaida tu ila hata Mimi mwanzo ilikuwa hivyo lkn kwa sasa ni muda mrefu tangu nipate hilo tatizo na nimesoma Shule na chuo drs la kawaida tu..nilikaza hivyohivyo na kufanikiwa kuhitimu vizuri tu
 
Asante Bitoz
Mkuu jisikie kawaida tu ila hata Mimi mwanzo ilikuwa hivyo lkn kwa sasa ni muda mrefu tangu nipate hilo tatizo na nimesoma Shule na chuo drs la kawaida tu..nilikaza hivyohivyo na kufanikiwa kuhitimu vizuri tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom