Masikini Ze Comedy Imekosa Legal Advice

Augustoons

JF-Expert Member
Oct 31, 2007
409
30
Ze Comedy yapigwa ‘Stop' TBC

na Sarah Kassim
SERIKALI jana ilitoa tamko kuwa kundi la sanaa ya maigizo la Ze Comedy, lililoasisiwa na Televisheni ya East Africa (EATV), halipaswi kutumia jina hilo katika televisheni nyingine kwa sababu, ni alama ya huduma (trade mark), mali ya EATV.

Akizungumza katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki, Yustus Mkinga alisema, Ze Comedy ni mali ya EATV iliyo na hakimiliki (Copy right) ya kazi za Ze Comedy.

"Ze Comedy ilianzishwa na EATV na kwamba, kabla ya hapo, hapakuwa na kipindi wala kikundi kilichoitwa Ze Comedy.

"Ze Comedy kama alama ya huduma (service mark) ni mali ya EATV ambayo pia ina hakimiliki (copy right) ya kazi za Ze Comedy," alisema ofisa huyo mkuu wa Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA).

Mkinga alisema, EATV ndicho kituo pekee chenye haki za kipekee, za kiuchumi za kazi zote za Ze Comedy kwani ndiyo waanzilishi wake, ikijumuishwa kuwaunganisha wasanii husika kuanzia hatua ya awali hadi mwisho, kurushwa kwa kipindi kwani wasanii walikuwa wakilipwa haki zao zote kila baada ya kipindi.

Alisema, kitendo cha kituo kingine kurusha kama inavyotaka kufanya Kituo cha Tanzania Broadcasting Corporation (TBC), si tu ni ukiukwaji wa haki za EATV na kinyume cha sheria ya Hakimiliki, pia ni ushindani usio halali (unfair competition), kinyume cha sheria ya ushindani Na. 8 ya mwaka 2003.

Mkinga alisema kwa mujibu wa barua za EATV kwa COSOTA, TBC ndiyo inayotarajia kurusha kipindi cha Ze Comedy, hivyo EATV ikaomba ufafanuzi wa kisheria kwao (COSOTA) kuhusu suala hilo huku nakala zikitumwa kwa mkuu wa kikundi cha wasanii hao, Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga'.

Alisema, COSOTA iliitaka EATV kueleza namna Ze Comedy ilivyoanzishwa na kuelezwa kuwa awali wasanii 15 walishindanishwa ili kupata sita kati yao na kuhusu uhusiano wa kikazi kati ya EATV na wasanii, watayarishaji, waongozaji na wapiga picha na EATV ikasema, ukitoa wasanii, wengine walikuwa na mkataba wa kikazi.

Kuhusu onyo la hakimiliki, EATV ilijitetea kuwa kila baada ya kipindi, kulikuwa na maneno yaliyosomeka EATV(c) kwa maana kwamba, kazi na ubunifu wote unaofanywa katika kipindi hicho, ni mali ya EATV na si vinginevyo.

Alisema, kwa kuwa Ze Comedy ni kipindi kinachomilikiwa, baada ya kuanzishwa na EATV kwa kushirikisha na wasanii, kipindi hicho kinalindwa chini ya Ibara ya 7 (1) (a) na 13 (a) ya mkataba wa Roma wa Ulinzi wa Wasanii, Wazalishaji wa Mkanda na Mashirika ya Utangazaji mwaka 1961 na kifungu cha 34 (1) ( a) cha sheria na. 7 ya Hakimiliki ya 1999.

Mkinga alisema, kwa vile kipindi cha Ze Comedy kinajumuisha maigizo ambayo yanabadilika kutokana na ujumbe uliokusudiwa, hata majina yanayotumika katika uigizaji, yaani Joti, Masanja Mkandamizaji na mengineyo, vyote ni mali ya EATV vinavyoweza kuendelea kutumiwa.

Katika hali ya kusikitisha haya ndiyo yanayowapata vijana wetu kipenzi wa zecomedy sasa. Hii yote inatokana na uhasama wa tembo wawili wao ni nyasi tu hapa. Je tutaacha kundi hili life je, jf tunawasaidiaje? Maana kinachowapata wao ndio kilichoipata iliyokuwa jambo forums hadi tulipopiga chenga kwenye domain rights na copy right hadi kuwa jamii forums. Hawa nao wakisaidiwa huenda wakpiga bao kama sisi. Na huko TBC naona kama ndio wamekweisha sasa. Mnasemaje wana jamvi?
 
Hakuna cha uhasama kabisa EATV wana haki kabisa!Hao vijana si watafute jina jingine wanaweza wakajiita THE comedy na si ze comedy na hayo majina wanaweza wakayapindisha kidogo tu kazi inaendelea badala ya kuzidi kulalamika
 
Hakuna cha uhasama kabisa EATV wana haki kabisa!Hao vijana si watafute jina jingine wanaweza wakajiita THE comedy na si ze comedy na hayo majina wanaweza wakayapindisha kidogo tu kazi inaendelea badala ya kuzidi kulalamika

waambieni wajiite The Comedy house
 
Mi sioni tatizo kwa EATV kutetea haki yao, hao the comedy kwanza hawana tena umaarufu kama ilivyokuwa mwanzo, ni kwa sababu kuna kipindi walinunuliwa na mafisadi wakawatetea na kisha kuwaponda watu wanaopigana dhidi ya mafisadi.

Kwanza huko kwenye TV ya Taifa wataweza kumsema mkapa?, kikwete?, mawaziri? Jibu ni kwamba hawawezi badala yake wataenda kutetea ufisadi
 
waambieni wajiite The Comedy house
Mimi siamini kama wanashindwa kuwa creative!ni kitu rahisi sana mbona there is always a solution bwana!waambieni waje wasome hii thread naamini wana JF wengi watawasaidia kuwapa mawazo badala ya kulalamikia EATV kitu ambacho kinawapotezea muda tu!
 
Ni yaleyale ya Rai. Ukiwauzia mafisadi gazeti linalotetea maslahi ya taifa, Hata ukiibuka na lingine linaitwa Raia Mwema ni hasara tu!
 
....mimi nafikiri bora ze comedy ...na mengi waelewane ...warudi EATV,....kitendo cha jana TVT /TBC kukataa kuonesha hotuba ya SLAA kimenipa hisia kuwa hawa vijana WATAPOKONYWA UHURU WAO TBC hata kama tido ana nia njema lakini...SERIKALI IMEONESHA NIA OVU YA KUTOPENDA KUKOSOLEWA....NA INAONEKANA VIJANA HAWATAKUWA NA UHURU KAMILI....

TUNAOMBA MZEE MENGI NA REGINA WAWARUDISHE HAWA VIJANA ...WAWAPE MKATABA MNONO...ILI WATUSAIDIE KUPAMBANA NA UFISADI
 
Hii inaonyesha vitu viwili vikubwa sana kwa wasanii wetu.

  • umuhimu wa wasanii wetu kuwashirikisha wanasheria kabla ya kusaini mikataba wanayopewa na producer na watangazaji wao, hawa vijana wamekuwa wakitumia majina hayo isipokuwa jina la kikundi siku nyingi sana kwenye kazi zao za kutafuta riziki za kila siku lakini kwa kuwa hawakuyaandikisha the they have no right to them kwani EATV waliyasajiri kama majina ya TV na sio kama ya wasanii.
  • Umuhimu wa wasanii wetu kuangalia masirahi ya mbele zaidi kuliko kufikiria hapo walipo bila kujali effect ya kesho kwenye masirahi wanayopata, EATV wako right pamoja na kwamba wao ndo wamewaibia ze comedy right yao lakini kwa kuwa hawakuandikisha majina yao mapeema the kazi yao ndo imefika mwisho.

But if they are creative enough watakuja na kitu kingine kipya lets sit and wait tarehe moja july.
 
Hawa ni wajinga kwani waliona kuwa wamekuwa maarufu wakadhani kuwa wako juu ya sheria?

Hawahitaji huruma hawa kwani hata ningekuwa mimi wa EATV ningetetea haki yangu ,na huo ndio mfano wa kuigwa .
 
Maisha ni mapambano. Kama kwenye hili wameshindwa basi hawana budi kuanza upya. I hope safari hii watainuka katika misingi itakayolinda maslahi yao.

Ze Comedy ni mfano mdogo tu unaoonyesha ni jinsi gani kutofahamu kwa wengi wetu kuhusu mambo haya ya mikataba na sheria zingine kunavyotukwamisha katika mambo mengi.

Hali hii ndio inayowarahisishia wabadhirifu na walafi wachache kuweza kuendelea na uhujumu wao wa mali za umma.
 
Hawa ni wajinga kwani waliona kuwa wamekuwa maarufu wakadhani kuwa wako juu ya sheria?

Hawahitaji huruma hawa kwani hata ningekuwa mimi wa EATV ningetetea haki yangu ,na huo ndio mfano wa kuigwa .

Mimi sidhani kama wamejiona kuwa maarufu ila wamerubuniwa na wafanyabiashara wasiojua masuala ya kisheria na wao walikumbumbumbu katika masuala ya sheria. Hivi tuseme TBC nao hawajui sheria za haki miliki? au walikuwa na lengo la kuwayumbusha hawa vijana na kuua vipaji vyao? inasikitisha.

Kuhusu EATV wana haki, huwezi kuibiwa huku unaona halafu ukabaki kimya. Warudi EATV waendelee kuwakandamiza mafisadi kwa kubonyeza kizenji.
 
Nasikia EATV kwanza walikuwa hawana issue nao kuhama....hawa jamaa walikuwa wanalipwa 4m(kuna watu wanasema per episode....sina uhakika nalo) Kila mtu akawa na gari lake,wamepangiwa nyumba nzuri tu Mbezi.Tatizo likaja pale walipomkubali Manji kuwa mlezi wao.
 
Nasikia EATV kwanza walikuwa hawana issue nao kuhama....hawa jamaa walikuwa wanalipwa 4m(kuna watu wanasema per episode....sina uhakika nalo) Kila mtu akawa na gari lake,wamepangiwa nyumba nzuri tu Mbezi.Tatizo likaja pale walipomkubali Manji kuwa mlezi wao.
Walishawishiwa na Manji hawa na Manji kawafuata si kibure bure ana lake jambo!Maskini watanzania wenzangu bila kufahamu wametumbukia kwa Mangi kisa wapate utajiri wa fasta fasta!Wangetulia EATV!any way kwa vile waliamua kuhama basi wabadilishe majina na siyo kulalamika tu!
Asante
Hollo
 
Once mtu anapotaka kuanzisha kitu its best kama unakuwa na legal counsel.mimi binafsi ni law student.befor nilikuwa hata still nina wasiwasi wa akina joti kuendeleza matimizi ya hili jina 'ze comedy'.wao kama comedians wanaweza ku go an extra mile and be creative watunge jina jipya and still they will make it.If before they made it why not know?
I believe they can fly and make it big.
 
Walishawishiwa na Manji hawa na Manji kawafuata si kibure bure ana lake jambo!Maskini watanzania wenzangu bila kufahamu wametumbukia kwa Mangi kisa wapate utajiri wa fasta fasta!Wangetulia EATV!any way kwa vile waliamua kuhama basi wabadilishe majina na siyo kulalamika tu!
Asante
Hollo

Lets be frank with one another.Today money is everything.kama wewe unaona pesa si kitu kaa nyumbani ucheze kidali mpo uone mwisho wako ni nini.mnadhani hawataki kuendesha 'vogue' au 'lamborghin'?wanataka ndio maana wanatafuta penye maslahi.
 
Once mtu anapotaka kuanzisha kitu its best kama unakuwa na legal counsel.mimi binafsi ni law student.befor nilikuwa hata still nina wasiwasi wa akina joti kuendeleza matimizi ya hili jina 'ze comedy'.wao kama comedians wanaweza ku go an extra mile and be creative watunge jina jipya and still they will make it.If before they made it why not know?
I believe they can fly and make it big.
Pia hilo jina watakalotunga wafanye process zote za kulisajili ili iwe miliki yao!Wasirudie kosa walilolifanya!
 
Lets be frank with one another.Today money is everything.kama wewe unaona pesa si kitu kaa nyumbani ucheze kidali mpo uone mwisho wako ni nini.mnadhani hawataki kuendesha 'vogue' au 'lamborghin'?wanataka ndio maana wanatafuta penye maslahi.
Kwani huko walikokuwa walikuwa hawapati pesa?
 
Mimi sisumbuliwi na majina yao wala lebel ya kikundi. Wasiwasi wangu ni kwa wao kukimbilia kwa fisadi Manji.
Katika hilo sina huruma kwao hata kidogo. Wanapepeta pumba ili wapate mchele, hiki ni kichekesho. Na sioni kama kuna sababu ya JF kuwasaidia wanaokumbatia ma-fisadi. Vita yetu ni juu ya ufisadi na wanaoshabikia ufisadi. EATV ina haki ya kutetea haki miliki yao.

poleni sana ndugu, kumbukeni mlokotoka. Wengine wanatoka Misri kuelekea kwenye nchi ya asali na maziwa nyie mnatoka kwenye nchi ya asali na maziwa kuelekea Misri, tena bila kiongozi (mtaishia jangwani).
 
Lets be frank with one another.Today money is everything.kama wewe unaona pesa si kitu kaa nyumbani ucheze kidali mpo uone mwisho wako ni nini.mnadhani hawataki kuendesha 'vogue' au 'lamborghin'?wanataka ndio maana wanatafuta penye maslahi.

Frankly speaking maslahi ya kutoka kwa fisadi ni sumu.
 
Kwani huko walikokuwa walikuwa hawapati pesa?

Walikuwa wanapata sikatai lakini hata wewe hollo ukipata a better paying job you leave the old one and move to the new one.mbona christian ronaldo nalipwa mno and still anang'ang'ania better payments?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom