Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,037
- 22,728
Kutoka Gazeti la MwanaHALISI - Sept 14, 2011
NDANI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), sasa hali si shwari tena. Wanaojiita waasisi wa "mpango wa chama wa kujivua gamba" wameanza kutuhumiana kukivuruga chama, imefahamika. Taarifa zinasema mlengwa mkuu wa kinachoitwa, "kukivuruga chama" ni Nape Nnauye, katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi.
Hatua ya Mukama inatokana na uamuzi wa CCM kumpigia magoti Rostam Aziz, mmoja wa watuhumiwa watatu wa ufisadi wanaotakiwa kujiondoa ndani ya chama hicho. Wengine wanaotakiwa kuondoka ni Edward Lowassa na Andrew Chenge.
Kwa mujibu wa waliokaribu na Nape, safari ya kiongozi huyo mjini Igunga ililenga kuwatambia baadhi ya wapinzani wake wa kisiasa waliodai Rais Kikwete amempiga marufuku kukanyaga huko wakati huu wa kampeni.
Kuthibitisha madai hayo, Nape aliandika katika mtandao wa JamiiForum, mara baada ya tukio hilo la Igunga, "Mlisema chama kimempiga marufuku Nape kukanyaga Igunga, nikasema tusubiri. Leo, mmeona nilivyotinga Igunga…"
Kwa mujibu wa mashuhuda, mara baada ya Nape kutoka nyumbani kwa wazazi wa Peter Ezekiel, alikwenda moja kwa moja kwenye baa maarufu iitwayo The Peak, ambapo inadaiwa alinisurika kichapo kutoka kwa mmoja wa mabaunsa wa CCM.
Inadaiwa kijana huyo wa miraba minne aliyefahamika kwa jina moja la Shaban, ambaye inadaiwa ni kutoka kwa kundi la Rostam Aziz, mara baada ya kumuona Nape kwenye baa hiyo alifoka, "Wewe unatafuta nini hapa?"
Naye Nape akajibu, "Wewe unafahamu unaongea na nani?" Shaban akajibu, "Ndiyo. Nafahamu kwamba wewe ni Nape Nnauye."
Kauli hiyo ilianza kumfanya Nape anyong'onyee kidogo, lakini mtoa taarifa anasema alijipa nguvu na kusema, "…Nimekuja kikazi. Tupishe tunamazungumzo yetu."
Shaban aligoma kuondoka na kisha akasema, "…Ondoka hapa, vinginevyo tutakuonyesha. Umekuja kutuharibia uchaguzi siyo?"
Mara baada ya kauli hiyo, taarifa zinasema Nape aliondoka katika eneo hilo na kuingia kwenye gari lake haraka kuelekea Singida.
Alipoulizwa na waandishi wa habari mjini Igunga kwa nini anadhani amefanyiwa vurugu, Nape alisema, "Hakuna kitu. Nilikuwa napita njia tu."
Sokomoko hilo lilitinga hadi kwa viongozi wake wakuu wa chama, Mukama na Rais Kikwete. Inadaiwa mara baada ya kupata taarifa hizo, Mukama kwa hasira alihoji, "Nape kwa nini umekwenda Igunga?"
Alisema, "Umekatazwa na Kamati Kuu usiende Igunga, sasa mbona umekwenda?" Alipojaribu kujitetea kwamba alikwenda huko kuhani, Mukama alisema, "Nani amekutuma? Nani amekuruhusu? Kijana, tafadhali usituharibie uchaguzi," Mukama anaripotiwa kufoka.
NDANI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), sasa hali si shwari tena. Wanaojiita waasisi wa "mpango wa chama wa kujivua gamba" wameanza kutuhumiana kukivuruga chama, imefahamika. Taarifa zinasema mlengwa mkuu wa kinachoitwa, "kukivuruga chama" ni Nape Nnauye, katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi.
Hatua ya Mukama inatokana na uamuzi wa CCM kumpigia magoti Rostam Aziz, mmoja wa watuhumiwa watatu wa ufisadi wanaotakiwa kujiondoa ndani ya chama hicho. Wengine wanaotakiwa kuondoka ni Edward Lowassa na Andrew Chenge.
Kwa mujibu wa waliokaribu na Nape, safari ya kiongozi huyo mjini Igunga ililenga kuwatambia baadhi ya wapinzani wake wa kisiasa waliodai Rais Kikwete amempiga marufuku kukanyaga huko wakati huu wa kampeni.
Kuthibitisha madai hayo, Nape aliandika katika mtandao wa JamiiForum, mara baada ya tukio hilo la Igunga, "Mlisema chama kimempiga marufuku Nape kukanyaga Igunga, nikasema tusubiri. Leo, mmeona nilivyotinga Igunga…"
Kwa mujibu wa mashuhuda, mara baada ya Nape kutoka nyumbani kwa wazazi wa Peter Ezekiel, alikwenda moja kwa moja kwenye baa maarufu iitwayo The Peak, ambapo inadaiwa alinisurika kichapo kutoka kwa mmoja wa mabaunsa wa CCM.
Inadaiwa kijana huyo wa miraba minne aliyefahamika kwa jina moja la Shaban, ambaye inadaiwa ni kutoka kwa kundi la Rostam Aziz, mara baada ya kumuona Nape kwenye baa hiyo alifoka, "Wewe unatafuta nini hapa?"
Naye Nape akajibu, "Wewe unafahamu unaongea na nani?" Shaban akajibu, "Ndiyo. Nafahamu kwamba wewe ni Nape Nnauye."
Kauli hiyo ilianza kumfanya Nape anyong'onyee kidogo, lakini mtoa taarifa anasema alijipa nguvu na kusema, "…Nimekuja kikazi. Tupishe tunamazungumzo yetu."
Shaban aligoma kuondoka na kisha akasema, "…Ondoka hapa, vinginevyo tutakuonyesha. Umekuja kutuharibia uchaguzi siyo?"
Mara baada ya kauli hiyo, taarifa zinasema Nape aliondoka katika eneo hilo na kuingia kwenye gari lake haraka kuelekea Singida.
Alipoulizwa na waandishi wa habari mjini Igunga kwa nini anadhani amefanyiwa vurugu, Nape alisema, "Hakuna kitu. Nilikuwa napita njia tu."
Sokomoko hilo lilitinga hadi kwa viongozi wake wakuu wa chama, Mukama na Rais Kikwete. Inadaiwa mara baada ya kupata taarifa hizo, Mukama kwa hasira alihoji, "Nape kwa nini umekwenda Igunga?"
Alisema, "Umekatazwa na Kamati Kuu usiende Igunga, sasa mbona umekwenda?" Alipojaribu kujitetea kwamba alikwenda huko kuhani, Mukama alisema, "Nani amekutuma? Nani amekuruhusu? Kijana, tafadhali usituharibie uchaguzi," Mukama anaripotiwa kufoka.
Kaazi kweli kweli..................