Masikini hamjali masikini mwenzie, anamjali tajiri asiye mjali yeyote Kati yao

ChizzoDrama

JF-Expert Member
Sep 29, 2019
1,317
1,229
Hakika wahenga waliosema ukistaajabu ya Mussa hujayaona ya Filauni hawakukosea. Masikini kumfariji masikini mwenziye ni mara chache sana lakini masikini huyu huyu yupo tayari kupanda hata gari akatoe pole kwa tajiri fulani.

Haya tunayaona ,katika jamii tunazo toka mahala ambapo kuna matabaka ya walio na wasionacho

Hivi ulishawahi kuona msiba unapotokea katika nyumba ya kitajiri hapo mtaani kwenu? Jinsi watu wanavyo jihimu kuchotelea maji, kwenda mashineni, kubeba kuni na shughuli zinginezo hapo. Na wote hawa wanakuwa ni masikini kwa asilimia kubwa huku matajiri wengi wakisubiri muda fulani wa kuuaga mwilli ndiyo waje na kwenda kuzika shughuli iishe.

Tizama unapotokeà msiba kwenye nyumba ya hoehae kama huyo marehemu alikufa Saa 11
Basi balozi atazunguka kila nyumba kuamsha watu kuwa kuna jirani kafariki
Ili vijana wawahi kuchimba lakini kila nyumba atakayo gusa kijana anasema anaumwa

Akifika nyumba inayofuata wa nyumba ya nyuma utaskia "SIKUKUELEWA BALOZI NILIKUA USINGIZINI" Yaani watavutana mpaka basi

Masikini tunashindwa kujaliana sisi kwa sisi matajiri nao hawatujali ila tunalazimisha kuwajali wao (aibu hii) tubadilike

Masikini mwenzio anae kupa 1000 ukikosa unga na watoto ni wa maana kuliko, kuliko tajiri aliye tayari kukununulia pombe hata za laki na kisha uende zako
 
Nimesoma heading tu, hivi ukiwa na kiu utajenga urafiki na mwenye kibuyu cha maji au utajenga urafiki na mwenye kiu kama wewe? Its simple logic, acha upoyoyo.
dhana Kama yako ndiyo chimbuko hasa la ile kitu mnaita UTUMWA ,, alafu kuchangia siyo lazima Kama huwezi kuwa na lugha zenye staha
Hizo mambo za "NIMESOMA HEADING TU" tumezichoka humu jaribu kuja na jambo jipya

Mimi poyoyo nawakilisha TU ndugu genius
 
dhana Kama yako ndiyo chimbuko hasa la ile kitu mnaita UTUMWA ,, alafu kuchangia siyo lazima Kama huwezi kuwa na lugha zenye staha
Hizo mambo za "NIMESOMA HEADING TU" tumezichoka humu jaribu kuja na jambo jipya

Mimi poyoyo nawakilisha TU ndugu genius
Wewe umeuliza swali kwenye heading, na umejibiwa,kama jibu linaashiria utumwa au la is not the issue. Nimesoma heading tu, ndio ukweli huo.
 
Hakika wahenga waliosema ukistaajabu ya Mussa hujayaona ya Filauni hawakukosea. Masikini kumfariji masikini mwenziye ni mara chache sana lakini masikini huyu huyu yupo tayari kupanda hata gari akatoe pole kwa tajiri fulani.

Haya tunayaona ,katika jamii tunazo toka mahala ambapo kuna matabaka ya walio na wasionacho

Hivi ulishawahi kuona msiba unapotokea katika nyumba ya kitajiri hapo mtaani kwenu? Jinsi watu wanavyo jihimu kuchotelea maji, kwenda mashineni, kubeba kuni na shughuli zinginezo hapo. Na wote hawa wanakuwa ni masikini kwa asilimia kubwa huku matajiri wengi wakisubiri muda fulani wa kuuaga mwilli ndiyo waje na kwenda kuzika shughuli iishe.

Tizama unapotokeà msiba kwenye nyumba ya hoehae kama huyo marehemu alikufa Saa 11
Basi balozi atazunguka kila nyumba kuamsha watu kuwa kuna jirani kafariki
Ili vijana wawahi kuchimba lakini kila nyumba atakayo gusa kijana anasema anaumwa

Akifika nyumba inayofuata wa nyumba ya nyuma utaskia "SIKUKUELEWA BALOZI NILIKUA USINGIZINI" Yaani watavutana mpaka basi

Masikini tunashindwa kujaliana sisi kwa sisi matajiri nao hawatujali ila tunalazimisha kuwajali wao (aibu hii) tubadilike

Masikini mwenzio anae kupa 1000 ukikosa unga na watoto ni wa maana kuliko, kuliko tajiri aliye tayari kukununulia pombe hata za laki na kisha uende zako
Kabisa ni ukwel mtupu
 
Hii mada imenikumbusha mwitikio wa watanzania wanyonge kwny lile tukio LA kutekwa kwa MO

Na mwitikio wa MO kwa matukio ya kutekwa Watanzania wenzie Wanyonge.
 
Back
Top Bottom