Masikini CCM! Mbeleko tegemezi ya polisi yazidi kukatika, kipi cha kufanya isizidi kuadhirika?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Ni baada ya RPC Mwanza kukataa agizo la kamati ya ulinzi ya wilaya (kamati za fitina) kuwakamata wabunge wa Chadema.

Nawaomba CCM wakae kitako na kutafakari (soul searching) angalau wawe wanajenga hoja za msingi kujibu zile za Chadema, hasa kuhusu wizi na ufisadi dhidi ya Watanzania! Acheni polisi wafanye kazi zao halisi kwa umma!

Friday, December 14, 2012


Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Evarist Mangu, amesema kuwa hawezi kumkamata Mbunge wa Nyamagana kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ezekiah Wenje, kwa kuwa hajapata taarifa rasmi.

Kamanda Mangu amesema kuwa hana taarifa zozote kama Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Nyamagana mkoani hapa imeliagiza Jeshi la Polisi kumkamata mbunge huyo na kuongeza kwamba ofisi yake haiwezi kufanyia kazi maagizo yanayotolewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya.

Kamanda Mangu alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na NIPASHE kwa njia ya simu. NIPASHE lilitaka ufafanuzi kutoka kwa Kamanda Mangu kama Wenje ameshakamatwa au la ukiwa ni utekelezaji wa agizo lililotolewa juzi na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga.


"Sina taarifa, hata hivyo, mimi sifanyii kazi kwa maelekezo ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya; isipokuwa ninafanya kazi kwa maelekezo ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa," alisema Kamanda Mangu.

Hata hivyo, Kamanda Mangu hakusema iwapo alimeshapokea taarifa zozote juu ya agizo hilo kutoka kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Nyamagana, Ally Kitumbu, ambaye kwa mujibu wa Konisaga, aliagizwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama kwamba anatakiwa amtie nguvuni na kumhoji Wenje.

Juzi Konisaga alisema Wenje anapaswa kukamatwa kwa kuwa amekuwa wakitoa kauli za uchochezi na upotoshaji kuhusiana na mgawanyo wa vyanzo vya Halmashauri za Manispaa za Nyamagana na Manispaa ya Ilemela, ambazo zilimegwa kutoka katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Aidha, Mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia anatuhumiwa kwa kutoa kauli hizo, lakini Konisaga hana mamlaka ya kuamuru akamatwe kwa kuwa DC Konisaga siyo Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Jana Wenje hakupatikana ofisini kwake kuzungumzia agizo la Konisaga na hata alipitafutwa kwa simu iliita bila majibu.

Katibu Muhtasi wake aliliambia NIPASHE ofisini kwake jana mchana kwamba mbunge huyo yuko jijini Dae es Salaam kikazi.

Katika hatua nyingine, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Tito Mahinya, alikataa kutoa ufafanuzi kuhusu ni kiasi gani cha fedha (asilimia 40) ya fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza kabla ya kuanzishwa kwa Manispaa ya Ilemela.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Wilson Kabwe, aliwaambia waandishi wa habari kuwa fedha hizo ziliingizwa kwenye akaunti ya Manispaa ya Ilemela, Desemba 10, mwaka huu.

Mahinya alidai kuwa hawezi kutoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari kwa sababu hiyo ni siri ya ofisi.

Hata hivyo, alitupilia mbali ombi la NIPASHE la kutaka kuonyeshwa maazimio ya kikao cha Baraza la Madiwani na wabunge wa Ilemela na Nyamagana wakiwamo.

Hata hivyo, Kabwe aaliwaambia wandishi wa habari kuwa Baraza liliketi Septemba 27, mwaka huu na kuridhia utaratibu utakaotumika kuhusu mgawanyo wa mali mara baada ya kuanzishwa kwa Manispaa ya Ilemela.

Aliendelea kusisitiza kuwa wabunge wote wawili, Kiwia na Wenje walikuwapo katika Baraza hilo na kuongeza kuwa yaraka hizo ni taarifa za ndani za Halmashauuri ya Jiji la Mwanza ambazo hazitakiwi kuitolewa kwa vyombo vya habari.

Kwa upande wake, Meya wa Manispaa ya Ilemela, Matata, alisema mgawanyo wa asilimia 40 ya fedha zinazotakiwa kutumwa kwenye akaunti ya Manispaa ya Ilemela ni kutokana na fedha zilizokuwamo kwenye akaunti ya Jiji la Mwanza wakati Manispaa hiyo inaanza kujitegemea.

"Sina hakika kama Halmashauri ya Jiji la Mwanza imeshatuma fedha katika akaunti ya Manispaa ya Ilemela. Lakini pia siyo kweli kwamba Ilemela itaendelea kupokea asilimia 40 kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza eti kutokana na vyanzo vya mapato," alisema Matata wakati akizungumza na gazeti hili.

Alisema baada ya kufunguliwa rasmi kwa kupata mgawo wa watendaji pamoja na uongozi wa madiwani, Manispaa ya Ilemela inatakiwa ianze kukusanya mapato kutokana na vyanzo vilivyomo ndani ya wilaya hiyo, na siyo vinginevyo.

"Hatuwezi kuendelea kupokea asilimia 40. Kwa sababu mikataba iliyofungwa wakati wa nyuma inaweza kuhamishwa kisheria na sisi kama Manispaa tukakusanya mapato katika vyanzo vya mapato vilivyomo kwenye ardhi yetu kama kawaida." alisema.

Alisema hata miradi ya maendeleo iliyomo kwenye ardhi ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela inatakiwa ikabidhiwe katika Manispaa ya Ilemela.



CHANZO: NIPASHE

 
Ni baada ya RPC Mwanza kukataa agizo la kamati ya ulinzi ya wilaya (kamati za fitina) kuwakamata wabunge wa Chadema.

Nawaomba CCM wakae kitako na kutafakari (soul searching) angalau wawe wanajenga hoja za msingi kujibu zile za Chadema, hasa kuhusu wizi na ufisadi dhidi ya Watanzania! Acheni polisi wafanye kazi zao halisi kwa umma!

Hawana habari kwamba vya chee vinaumiza -- in fact vinaibisha.
 
Mabavu yao na sasa wafikia ukingoni. Nimesikia wameangukia pua huko Mwanza tena, yule diwani msaliti waliompitisha kuwa Meya kwa mabavu katimuliwa na mahakama! Aibu ilioje hiyo!

Huyu PM ni mfu -- anaruhusu madudu katia halmashauri ambayo yanakuja kuiaibisha ofisi yake!
 
Hali ni mbaya sana kwa CCM hapa Mwanza
1/Wameshindwa rufaa ya jimbo la Ilemela
2/Diwani Matata kashindwa mahakamani.
3/RPC kagoma kuwakamata wabunge wa CHADEMA
 
WOKOVU UNAKARIBIA........Muda si mrefu polisi nao watachoka, maana wataona wanabeba lidude ambalo halibebeki, wataamua kulitupa chini hapo ndio utaona kuwa CCM hawana pumzi ya kumaliza mchezo kaitka dakika 90, ni wepesi mno na ushindi 2015 njia ni nyeupe.
 
Big up sifongo, ccm ni TUFE ZITO twasubiri litupwe chini, then tulisahau kama lili-exist in the universe.
 
Hali ni mbaya sana kwa CCM hapa Mwanza
1/Wameshindwa rufaa ya jimbo la Ilemela
2/Diwani Matata kashindwa mahakamani.
3/RPC kagoma kuwakamata wabunge wa CHADEMA

Yule Shabab Kinana kaanza na gia mbaya - au nuksi inamuandama kutokana na ufisadi wake.
 
Mkuu ndicho walichobaki nacho ccm na heko kwako RPC kwani inaonyesha wewe unajua nini maana ya kiapo ulichokula maana wenzako wanaapa kishahi tu. Pia ccm mjue mwisho wa ubaya ni aibu nayo aibu ndo imewakaribia sasa
 
Friday, December 14, 2012


Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Evarist Mangu, amesema kuwa hawezi kumkamata Mbunge wa Nyamagana kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ezekiah Wenje, kwa kuwa hajapata taarifa rasmi.

More... See 1st post

 
Naona RPC anashuhudia UNYAMA wa CCM Inavyowafanyia CHADEMA Mkoani MWANZA; Yeye kama POLISI anaona Sasa ATUKUZE na KUFUATA SHERIA... zaidi ya Unyama wa CCM
 
Kwa nini mwandishi hakumuliza kamanda wa Polisi wa wilaya ya Nyamagana ambaye aliagizwa na Kamati ya usalama ya wilaya ambaye ndiye anawajibika na maelekezo haya. Kinyume chake ameenda kumuuliza kamanda wa mkoa alitarajia jibu gani zaidi ya alivyjibiwa?
 
Muone huyo meya wa kichina bwana matata kama vile kachaguliwa kwa uwazi na haki ; shame on him
 
Kuna post humu ilisema matata katimuliwa!! Mara tena hii hapa!!inanichanganya,ngoja niirudie ile post kama bado itakuwepo.
 
Na ujue kwamba mbeleko ya polisi hutengenezwa kwa nguo ya turubai. sasa kama hii inakatika, basi imekula kwao CCM. I hate that party!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom