Ndyali
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 1,661
- 948
Itakumbukwa kuwa makamanda kutoka Mbeya walijitolea kwa ghalama zao kwenda kuongeza nguvu katika vuguvugu la M4C kwa kutoa elimu ya uraia katika vijiji vyote vya mkoa wa Morogoro, kwa mafanikio ya Morogoro tayari ripoti ishatolewa na mkuu wa oparation hiyo. Walipotoka Morogoro Makamanda hao walitua katika vijiji wa mkoa wa Iringa wakienda nyumba kwa nyumba na kuharibu kabisa ngome za ccm vijijini katika vijiji vya jimbo la Mfindi, wote tulisikia Dr. Slaa akieleza mafanikio katika vijiji vya wilaya ya Mfindi, taarifa ya Dr. Slaa iliwashitua usalama wa taifa na polisi wakalazimika kupanga njama za kuwaunganisha Makamanda wa Mbeya na kesi ya mauaji ya RIP Mwangosi. Hivyo polisi waliamua kuwakusanya makamanda 32 wa Mbeya waliokuwa wamejichimbia vijijini kutoa elimu ya uraia. Siku ya leo baada ya kugundua kuwa somo lao halieleweki kwa watanzania wamewaachia, na jioni ya leo msururu mkubwa wa magali yaliyotoka kuwapokea mashujaa wetu mpakani mwa Iringa na Mbeya umepita hapa maeneo ya ccm kwa shangwe kuu ya ajabu. Kweli Mbeya wamedhamiria kuwa mashujaa wa M4C.