Mashirika kama TTC sioni sababu kwanini lisiizidi Vodacom na Airtel au kwanini Posta lisiwe zaidi ya DHL

BLUE BALAA

JF-Expert Member
Nov 30, 2010
1,222
764
Napongeza sana kushuhudia transformation inayokwenda kufanyika TANESCO kulifanya shirika la kujiendesha kibishara. Sina wasiwasi na uwezo wa MD Maharage Chande pamoja na bodi yake inayongozwa na gwiji wa ufuatiliaji wa miradi Omary Issa. Lakini pia naangalia wajumbe kama Zawadia Nanyaro alikuwa PWC, Mchechu, Mafuru na Balozi Maharaj kwakweli nje ya mapungufu ya kibinadamu ila the business minded members wapo katika taasisi hii. Nimemsikiliza Maharage yeye kwenye speech yake anaitazama TANESCO kama

1. Wana bidhaa isiyo na mpinzani ndani ya Nchi
2. Wana uwezo wa kuhudumia nchi za jirani ambazo hazina nishati ya umeme wa kutosha
3. Wana asset za 13.Trillion hivyo wanakopesheka
4. Wana monthly billions hivyo they have a vibrant cashflow
5. Wana customer base over 7million people hivyo wana uwezo waku triple number of customer
6. Wana infrastructure nchi nzima hivyo distribution ya umeme siyo tatizo.

Kwa maana hiyo napongeza sana Serikali kwa focus yao ila mashirika kama TTC sioni sababu kwanini lisi izidi Vodacom na Airtel au kwa nini Posta lisiwe zaidi ya DHL, UPS, SDV ambazo wamefikia kumuliki na ndge zake na meli kwa ajili ya shipping na courier services. Nchi ina tunu ya vijana wengi wenye transormative minds wapewe mashirika haya na siyo kuweka watu kuendesha kimazoe
 
Ttcl hahaha Hawa jamaa sijui shida huwa ni nini? Posta wanataka fufuka ila wap? Sijui Haya mashirika shida huwa ni nini?
 
Ttcl hahaha Hawa jamaa sijui shida huwa ni nini? Posta wanataka fufuka ila wap? Sijui Haya mashirika shida huwa ni nini?

Shida hapo nyuma waliingiliwa sana na wanasiasa kupitia bodi zao. Yani bodi zilikuwa zina wabunge, mawaziri wastaaf etc wakawa ndio wanakwamisha plans za bodi. Ndio hivyo hivyo tu mashirika kama TANAPA, NCAA yamekuwa yakiyumbishwa. Naangalia shirika kama AICC unashangaa wanafanya nini tangia mwaka 1977 wanafanya real estate lakini they don't move
 
Shida hapo nyuma waliingiliwa sana na wanasiasa kupitia bodi zao. Yani bodi zilikuwa zina wabunge, mawaziri wastaaf etc wakawa ndio wanakwamisha plans za bodi. Ndio hivyo hivyo tu mashirika kama TANAPA, NCAA yamekuwa yakiyumbishwa. Naangalia shirika kama AICC unashangaa wanafanya nini tangia mwaka 1977 wanafanya real estate lakini they don't move
Sahihi mkuu hata vyama vya ushirika kuingia kwa wanasiasa kumeviyumbisha mno kuna wakati vyama, mashirika vinashindwa fanya maamuzi kwa uwepo wa wanasiasa (hawajui lolote ila wanajidaia nguvu zao kisiasa)

Siku ikiwekwa vigezo angalau mbunge awe na elimu Kuanzia diploma Basi ndo siku tutaanza piga hatua kimaendeleo
 
Sahihi mkuu hata vyama vya ushirika kuingia kwa wanasiasa kumeviyumbisha mno kuna wakati vyama, mashirika vinashindwa fanya maamuzi kwa uwepo wa wanasiasa (hawajui lolote ila wanajidaia nguvu zao kisiasa)

Siku ikiwekwa vigezo angalau mbunge awe na elimu Kuanzia diploma Basi ndo siku tutaanza piga hatua kimaendeleo

Wala vigezo vya elimu siyo factor ya uweledi kuna watu wengi hawajawahi kuuona mlango wa sekondari lakini wana operate kwa weledi wa hali ya juu sana
 
Wala vigezo vya elimu siyo factor ya uweledi kuna watu wengi hawajawahi kuuona mlango wa sekondari lakini wana operate kwa weledi wa hali ya juu sana
Kweli kabisa,mfano mdogo tu Msukuma jinsi anavyoelezea bungeni nondo zake unazionaje
 
Back
Top Bottom