state agent
JF-Expert Member
- Jul 1, 2019
- 1,764
- 2,511
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Jery Muro ameiambia ITV muda mfupi kuwa mashine za kutengeneza vitambulisho vya utaifa wilayani humo zote imeibiwa usiku wa kuamkia leo.
Taarifa hiyo imekuja muda mfupi baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kutoa ratiba ya kuandikisha na kusajili vitamburisho hivyo kwa mkoa huo wiki hii mpaka tarehe 20/01/2020.
Watu hao wasijulikana mpaka muda huu hawajakamatwa hata mmoja wao
Chanzo: ITV habari za hivi punde
Taarifa zaidi;
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amesema Ofisi ndogo za NIDA zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Arusha zimeibiwa vifaa vyote na Watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo
Amesema vifaa vilivyoibwa ni pamoja na Kompyuta Mpakato nne na Kamera si chini ya tatu pamoja na vifaa vingine vilivyokuwa vikiingiza majina kwenye mifumo na katika wizi huo unaonekana ni wa ndani kwani milango haikuvunjwa
Aidha, amesema tukio hilo limewashtua na ni mara ya pili tukio kama hilo kutokea ikiwa mara ya kwanza lilitokea ofisi za NIDA Makao Makuu Wilaya ya Arumeru ambapo baadhi ya vifaa viliibwa taratibu kwa muda mrefu
Ameida kuwa wizi huo unaonekana umefanyika kimtandao kwasababu Ofisi ndogo za NIDA kwenye ukanda huo zipo karibu kabisa na jengo la NMB lenye walinzi na Halmashauri ina Walinzi wake
Amewaomba Wananchi kuwa watulivu kwa kipindi hiki ambacho yeye na Kamati ya Ulinzi na Usalama wanaendelea kufuatia na vile vile ameeleza kuwa kwa sasa hakutakuwa na huduma katika ofisi hiyo ya Halmashauri ya Arusha
Taarifa hiyo imekuja muda mfupi baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kutoa ratiba ya kuandikisha na kusajili vitamburisho hivyo kwa mkoa huo wiki hii mpaka tarehe 20/01/2020.
Watu hao wasijulikana mpaka muda huu hawajakamatwa hata mmoja wao
Chanzo: ITV habari za hivi punde
Taarifa zaidi;
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amesema Ofisi ndogo za NIDA zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Arusha zimeibiwa vifaa vyote na Watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo
Amesema vifaa vilivyoibwa ni pamoja na Kompyuta Mpakato nne na Kamera si chini ya tatu pamoja na vifaa vingine vilivyokuwa vikiingiza majina kwenye mifumo na katika wizi huo unaonekana ni wa ndani kwani milango haikuvunjwa
Aidha, amesema tukio hilo limewashtua na ni mara ya pili tukio kama hilo kutokea ikiwa mara ya kwanza lilitokea ofisi za NIDA Makao Makuu Wilaya ya Arumeru ambapo baadhi ya vifaa viliibwa taratibu kwa muda mrefu
Ameida kuwa wizi huo unaonekana umefanyika kimtandao kwasababu Ofisi ndogo za NIDA kwenye ukanda huo zipo karibu kabisa na jengo la NMB lenye walinzi na Halmashauri ina Walinzi wake
Amewaomba Wananchi kuwa watulivu kwa kipindi hiki ambacho yeye na Kamati ya Ulinzi na Usalama wanaendelea kufuatia na vile vile ameeleza kuwa kwa sasa hakutakuwa na huduma katika ofisi hiyo ya Halmashauri ya Arusha