Mashine za kutotolesha mayai (Incubators): Upatikanaji wake, aina zake, matumizi na ushauri

Kuna jamaa yangu alinunua magomeni, incubator na inayoweza kuhatch mayai elfu tisa (9,000) hapo magomeni, cost ilikuwa arround milioni 20 za kitz, inafanya kazi mpaka leo. Yeye biashara yake ni kutotolesha vifaranga tu, unaenda na mayai yako anakucharge 300 kwa kila yai. Yakitoka yasitoke that's the cost. Nikavutiwa na biashara nikatafuta vendor china nikapata kwa dola 2900 kila kitu, hiyo iliikuwa ni hatcher ya mayai 5000 na incubator ya mayai 6000, bei ya hatcher ilikuwa dola 700, na incubator 1100, na hizo 1100 zilikuwa ni contena la futi ishirini kuja tz. Sasa hizi habari ni za mwaka 2010 mwanzoni, sijui sasa zikoje.pia kumbuka kuna tra na customs mzigo ukishafika, fanya utafiti wa gharama za kutoa mzigo. Kama uko interested ingia alibaba.com, jiridhishe mwenyewe na wauzaji kwa kusearch kama unavyofanya google. Halaf malizana nao. Ila kuwa makini, matapeli wengi. Ingekuwa vema ukawatumia watz wanaoenda kununua bidhaa zao huko japo wakachungulie kama jamaa wana kiwanda na wahakikishe usalama wa pesa zako kwa kuthibitisha mzigo unapakiwa melini.
Nb: hata hao watz usiwaamini sana, sanaa zimezidi nchini hapa.

Doltyne

naomba contacts za huyu jamaa mwenye incubator

ninao geese (bata bukini) ninawafuga na bado muda kidogo wataanza kutaga, nategemea kutumia incubator kufanya breeding ili waongezeke kwa haraka na kwa ufanisi

awaiting your response
 
Wadau naomba msaada wenu. Mimi ni mjasiliamali anayejishugulisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji. Shida yangu ni Incubator mashini ya kuangulia mayai.

Sijawa na mtaji wa kununulia incubator halisi ila nataka nianze kwa jinsi ya kiasili kabisa ya kuangua mayai japo kati ya 25 hadi 40 ili kuokoa mayai mengi yanayoharibika kwa kuachwa na kuku mwenyewe na pia ili kupata vifaranga wengi kwa wakati mmoja.

Sasa niliambiwa kuna njia fulani ya kutotolesha mayai bila kutumia incubator. Naomba msaada kwa anayefahamu.

Naomba kutoa hoja
 
Kuna njia ya kutumia pumba ila ina complications nyingi sana, nimewahi kujaribu ila sikufanikiwa.
 
Wadau naomba msaada wenu. Mimi ni mjasiliamali anayejishugulisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji. Shida yangu ni Incubator mashini ya kuangulia mayai. Sijawa na mtaji wa kununulia incubator halisi ila nataka nianze kwa jinsi ya kiasili kabisa ya kuangua mayai japo kati ya 25 hadi 40 ili kuokoa mayai mengi yanayoharibika kwa kuachwa na kuku mwenyewe na pia ili kupata vifaranga wengi kwa wakati mmoja. Sasa niliambiwa kuna njia fulani ya kutotolesha mayai bila kutumia incubator. Naomba msaada kwa anayefahamu.
Naomba kutoa hoja

Kuna incubator za kibongo zinauzwa 700,000/-,uko vizuri?
 
Sasa hizi dharau!

Mzee kama hufahamu kitu ni vema ukanyamaza.Dharau ziko wapi hapo?
Nawafahamu vijana wanatengeza hizo incubator hapahala Dar kwa gharama hizo.Zinafanya kazi vizuri tu.Zinatumia umeme na kerosine incase umeme hamna.Zinaweza ku-incubate hadi mayai 120 kwa mpigo(hii ninayotumia ina uwezo huo pia)

Unajua bei ya imported incubator wewe?
 
Mzee kama hufahamu kitu ni vema ukanyamaza.Dharau ziko wapi hapo?
Nawafahamu vijana wanatengeza hizo incubator hapahala Dar kwa gharama hizo.Zinafanya kazi vizuri tu.Zinatumia umeme na kerosine incase umeme hamna.Zinaweza ku-incubate hadi mayai 120 kwa mpigo(hii ninayotumia ina uwezo huo pia)

Unajua bei ya imported incubator wewe?

Hasira za nini mkuu.

We tayari amesema anamtaji kidogo laki 7 si utakuwa unamuumiza.

Yeye mwenyewe hata hajarespond/kubaliana kwa hyo pesa. Amekaa kimya

Halafu ameomba njia nyingine ya kienyeji tofauti na Incubator. Sasa nashangaa wewe kumbanjikia bei
 
Tatizo watanzania tuna uoga wa kufanya vitu wenyewe. Kutengeneza incubator mwenyewe ni rahisi kabisa. Nakushauri jaribu kwenda mahali penye incubator kama sido n.k uchungulie jinsi ilivyo na wewe ukatengeneze.

Kwa kuanzia unaweza kutengeneza ya mayai kati ya 50-100. Inawezekana kabisa jiamini. Pia jaribu ku-google upate info nyingi zaidi.
 
Hasira za nini mkuu.

We tayari amesema anamtaji kidogo laki 7 si utakuwa unamuumiza.

Yeye mwenyewe hata hajarespond/kubaliana kwa hyo pesa. Amekaa kimya

Halafu ameomba njia nyingine ya kienyeji tofauti na Incubator. Sasa nashangaa wewe kumbanjikia bei

Mtaji kidogo ndiyo kiasi gani cha pesa?
 
wadau nashukuru kwa mchango wenu. lakini kama nilivyodokeza wakati naleta mada hii kama mjasiliamali, nilisema wazi kwamba sijawa na mtaji wa kununulia incubator ndio maana nikapendekeza kupata msaada wa ushauri wa kutumia njia yoyote ya kiasili kama ipo. nataka kuanza ili nipate mtaji wa kununulia incubator.

namshukuru ndg yangu Katavi ameonyesha uwezekano wa njia mbadala. naamini complications ulizokutana nazo zikifanyiwa kazi kitaaluma basi itakuwa na tija zaidi kwa wajasiliamali wengi vijijini na mijini. ila tu naomba dondoo ili niifanyie kazi. namshukuru pia ndg yangu Kinyungu aliyenishauri nitengeneze mwenyewe - ni wazo zuri, actually nipo kwenye tafiti za vyanzo vya joto na jinsi gani ya kuli-control.

lakini kama yupo mdau mwenye incubator anayeweza kunitotolea mayai kwa garama naomba asaidie kwa wakati huu
 
UsIhangaike na Mtaji kwani Hilo si tatizo, Kama una soko, nitakuonesha Soliko Pesa. Totolesha kwanza kwa wenzako Wenye inc btor yai Shs mia3 hadi upate Mitaji
 
Wajameni, habari za mishe mishe. Najitokeza humu jamvini nikijua humu ni darasa murua la kuelimishana hususani ktk ujasiriamali.

Naomba msaada wenu, natarajia kuanza ufugaji kuku wa kienyeji kibiashara na ningependa kujua kama kuwa na mashine yangu ya kutotoa mayai (incubator) ni njia mwafaka. Mahali ninapoishi umeme haujafika, hivyo nikiwa na mashine itabidi kununua mafuta ya taa au dizeli.

1. Kuna thread niliwahi kuisoma jamvini humu kuwa kuna watu wanatotolesha kwa malipo. Je, ni njia ipi yaweza kuwa gharama nafuu kati ya kuwa na mashine mwenyewe (kununua mafuta) na kutotolesha kwa watu?

2. Kama kuendesha incubator ni nafuu kuliko kutototlesha kwa watu, Je, naweza kuipata mashine hiyo sehemu gani au kwa nani na kwa gharama kiasi gani? Kulingana na mtaji wangu, tuseme nahitaji yenye uwezo kuanzia mayai 100 na kuendelea.

Nawasilisha kwa maelekezo yenu
 
Kaka incubator inataka umeme wa kutosha kama umeme ukikatika hata 30 min tu umeharibu mayai mkuu ss wengine wakiihitaji wanakuwa na back up ya umeme (Generator) ushauri wangu angalia hao vifaranga unaowataka ni wa kwako wa kufuga achana na hii maneno na kama ni wa kuuza plz anza kutafuta Generator kwanza maana umeme wa ki bongo unaujua usijerudi hapa jamnvini unalia lia tu!
 
Mkuu,

Kuna wajsiriamali wanaotengeneza INCUBATORS zinazotumia mafuta ya taa. Hebu jaribu kumpigia Dr Singa 0754 502805. Hii namba ninayo kwa miaka kama mitano sasa, inawezekana kabadilisha.

Nijulishe ukifanikiwa au ukishindwa kumpata.

All the best.
 
Kaka incubator inataka umeme wa kutosha kama umeme ukikatika hata 30 min tu umeharibu mayai mkuu ss wengine wakiihitaji wanakuwa na back up ya umeme (Generator) ushauri wangu angalia hao vifaranga unaowataka ni wa kwako wa kufuga achana na hii maneno na kama ni wa kuuza plz anza kutafuta Generator kwanza maana umeme wa ki bongo unaujua usijerudi hapa jamnvini unalia lia tu!

Mkuu nashukuru sana kwa habari hiyo, itanisaidia ktk siku za mbele. Nataka kufuga kuku wa kwangu lakini kwa lengo la kuuza hapo baadaye wakiwa wakubwa. Hata hivyo kama nilivyojieleza katika post yangu ni kuwa sihitaji mashine ya umeme kwa sasa bali mafuta ya taa kwani naishi mahali pasipo na umeme.
 
Mawenzi asante kwa ufahamisho, nimewasiliana na Dr Singa akanieleza kuwa anazo mashine hizo, nafanya mipangilio nimwendee. Shukrani mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom