Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
1. Mashine hiyo imetengenezwa wapi na kwa lengo gani kabla ya ujio wa corona?
2. Je, ni dawa gani inatumika kunyunyizia watu kiasi kwamba wanajiexpose pumzi na ngozi zao kwa dawa hizo?
3. Je, dawa hizo zina vitu gani vyenye uwezo wa kuua corona kwa manyunyu lakini zisiwe na madhara kwa tu kupumulia au kuingia kupitia ngozi?
4. Kutokana na swali la 4; je inawezekana dawa hizi hazina vitu vyovyote vikali (active ingredients) ambazo zinaweza kusababisha kansa (carcinogens)? Visije kuua virusi vya corona lakini vikawa na madhara kwenye chembe za ngozi!
5. Dawa au mashine yoyote ya kufanya tiba inatakiwa ipitiwe utafiti wa kisayansi kuona uwezo wake kufanya unachofanya (efficacy) na kwa usalama (safety). Je, mashine hizi zimefanyiwa utafiti wapi na wa namna gani kuonesha kuwa zinafanya kile inachodaiwa kufanya?
6. Na kutokana na hilo la 5 je mtu akishapita kwenye hii mashine anakuwa amejikinga kwa muda gani? Ni kuwa virusi haviwezi kumgusa (vikimgusa vinakufa kama nzi kwenye moto). Je akibadilisha nguo bado ana "kinga" hiyo?
7. Wizara ya Afya inatakiwa kujibu maswali haya na watu wa TFDA pia.
Haya ni baadhi ya maswali tu. NI wazi kuwa Rostam anataka kutoa msaada na hili ni jambo zuri kweli kweli lakini bila kujibu au kutoa maelezo ya kujibu maswali haya (na labda mengine) ni vizuri watu waangalie na kufikiria mara mbili kabla ya kupita kwenye mashine hizi wakiamini kuwa wameua virusi vya corona na hivyo wako "clear".
Ninachojua ni kuwa mashine za namna hii zimekuwa zikitumika kuspray kwenye maeneo kama aiport, migodi n.k kwa ajili ya decontaminate watu. Na zipo za aina nyingi lakini linapokuja suala la corona ni kwa kiasi gani ziko effective ndio hasa swali langu.
Nje ya hapo, kama majibu ya maswali haya yote yanakubalika kiakili na yana msingi wa kisayansi RA anastahili pongezi za dhati na badala kumsubiria yeye tu serikali iwezeke kwenye kupata vifaa vingi zaidi.
MMM
NB: Mashine hii isije kuwa kama kikombe cha fulani.
BAADHI YA MASHINE ZA AINA HII: