Mashine ya Kuchakata mhogo bei gani

wakurochi

JF-Expert Member
Dec 4, 2017
2,647
2,936
Hii ni mashine inakatakata mhogo mbichi vipande vipande kama slesi za mkate kwa kipimo unacho set. Kipimo kinachotakiwa sasa hivi ni sentimeta moja ya unene wa mhogo.. Baada ya hapo vipande vile vinaanikwa na kuuzwa. Soko lipo hata kama una tani ngapi. Tatizo nihizi mashine.

Mi naona ni fursa kwa mafundi kutengeneza hizi mashine watapiga hela ndefu kama watakuwa makini kuzifanya zinunulike yaani wajitahidi kupunguza gharama.

Zilizopo za mchina zinatumia umeme/Generator kama umeme hamna. Fundi anaweza kutengeneza ya "manual" yaani mfumo wa kuzungusha puli na hendeli kwsababu kuchakata eka 2 tu kwa mkono sio mchezo ni shughuli pevu.

Nawsilisha kwenu great thinkers

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom