mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Habari wakuu,
Kiotomotela cha Benki ya Stanbic jengo la Shoppers Mikocheni ni kibovu ambapo hupelekea wateja kusumbuka sana, hivyo kutoa mwanya kwa mlinzi kutoa msaada.
Ubovu wake ni kwamba screen yake mwanga ni hafifu sana kiasi kwamba huwezi kutumia wakati jua likiwepo, kwa usiku sijui inakuwaje. Nadhani ubovu ule ni kutokana na kupigwa jua kwa muda mrefu hivyo kufifilisha mwanga.
Mimi leo nimeenda kutoa mpunga ila baada ya kuchomeka kiotomotela nilishindwa kuona chochote hata baada ya kuhangaika kwa takribani dakika 1 mpaka mashine ikaanza kutoa mlio fulani.
Akaja mlinzi kutoa msaada akiwa kavaa kapelo na kitambaa anachojifunika ili aweze kuona kwenye display. Kweli alinisaidia nikafanikiwa lakini sijapenda maana unafanya muhamala ikiwa pamoja na kuweka nywila yeye akiwa hapo hapo.
Ajabu baada ya kutoa pesa ikawa kama kasita kunirudishia kiotomotela changu mpaka nilipomwambia anipatie, huenda alikuwa kasahau.
Baada ya kuchukua mpunga nikaenda kwenye egesho la gari, kwa muda ule mpaka naondoka mlinzi alikuwa kasaidia watu wanne.
Ombi langu kwa Benki husika: Naomba sana mfuatilie na kurekebisha tatizo hili, Benki muhimu kama hii kuendekeza tatizo dogo kama hili ni ajabu sana.
Walinzi mnaowaweka pale ni kwa ajili ya kuangalia usalama wa wateja na pesa zao na sio kuwasaidia wateja kutoa pesa. Mbona viotomotela vingine vinavyozunguka pale havina tatizo kama lenu?
Nawatakia utekelezaji mwema.
Kiotomotela cha Benki ya Stanbic jengo la Shoppers Mikocheni ni kibovu ambapo hupelekea wateja kusumbuka sana, hivyo kutoa mwanya kwa mlinzi kutoa msaada.
Ubovu wake ni kwamba screen yake mwanga ni hafifu sana kiasi kwamba huwezi kutumia wakati jua likiwepo, kwa usiku sijui inakuwaje. Nadhani ubovu ule ni kutokana na kupigwa jua kwa muda mrefu hivyo kufifilisha mwanga.
Mimi leo nimeenda kutoa mpunga ila baada ya kuchomeka kiotomotela nilishindwa kuona chochote hata baada ya kuhangaika kwa takribani dakika 1 mpaka mashine ikaanza kutoa mlio fulani.
Akaja mlinzi kutoa msaada akiwa kavaa kapelo na kitambaa anachojifunika ili aweze kuona kwenye display. Kweli alinisaidia nikafanikiwa lakini sijapenda maana unafanya muhamala ikiwa pamoja na kuweka nywila yeye akiwa hapo hapo.
Ajabu baada ya kutoa pesa ikawa kama kasita kunirudishia kiotomotela changu mpaka nilipomwambia anipatie, huenda alikuwa kasahau.
Baada ya kuchukua mpunga nikaenda kwenye egesho la gari, kwa muda ule mpaka naondoka mlinzi alikuwa kasaidia watu wanne.
Ombi langu kwa Benki husika: Naomba sana mfuatilie na kurekebisha tatizo hili, Benki muhimu kama hii kuendekeza tatizo dogo kama hili ni ajabu sana.
Walinzi mnaowaweka pale ni kwa ajili ya kuangalia usalama wa wateja na pesa zao na sio kuwasaidia wateja kutoa pesa. Mbona viotomotela vingine vinavyozunguka pale havina tatizo kama lenu?
Nawatakia utekelezaji mwema.