Mashindano ya 'U-Miss' Yamezidi. Michezo Mingine Tumeisahau?...Twisted Priority?

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Tanzania yetu kwa kweli imeneemeka na kutunukiwa, maana warembo ni kede wa kede, kanda zote na mikoa yote ya nchi kuna warembo wa kumwaga. Hadi jirani zetu hutubu juu ya neema hii. Kwa nyakati mbali mbali nimebahatika kukutana na watu, tena akina dada toka Zambia na Kenya wote wakisifia Tanzania kwa kuwa na akina dada wengi walio warembo kuliko huko makwao. Ma'braza' ndiyo kabisaa usiseme.... wanakodolea da'zetu utafikiri kuna jinamizi lililojitokeza na kumeza akina dada wote huko makwao, kisha wakafunuliwa macho na kutahamaki kuona Tanzania bado kuna madada wana exist!!

Nikiwa mmoja wa wapenzi wa kuona dada zetu wanapendeza, kung'ara, kujawa na utashi, utanashati na madoido mbalimbali yenye kuzingatia maadili ya jamii katika urembo, mapenzi yangu haya kinamna yanaonekana kuingiliwa. Maana ghafla bin vuu, nimebakiwa na mshangao ulliochangamana na kero kutokana na kuongezeka kwa matukio ya 'u-miss'. Hivi kulikoni Waheshimiwa? Hivi nini kimetokea na imekuwaje siku hizi?!!!....

Kila kukicha tunasikia mashindano ya u-miss...kila kona, kila blog inaongelea u-miss, utasikia mara:

-miss mwananyamara, miss tabata, miss peramiho,
-miss kinondoni, miss kantalamba, miss ibadakuli, miss mabibo
-miss rukwa, miss kivukoni, miss bugurunikwamanyani, miss kyela
-miss mikoroshoni, miss mabatini, miss kahama, n.k..

Si hivyo tu, pia pameanza kujitokeza ma-miss matukio:

-miss wasomi, miss whatever.. n.k..

Cha kushangaza kama si kusikitisha ni kule kuona jamii nzima iko ndani ya wimbi hili, ikielea nalo bila kuuliza. Yaani inavyoonekana sasa ni kuwa kila mmoja amekuwa shabiki. Kwa kweli nadhani ni wachache wanaoona kuwa hapa kuna jambo lililojitokeza bali limefichika, ni jambo lenye madhara katika jamii, ni jambo la 'twisted priority'.

Katika twisted priority hii ni kwamba, uwezo wa kuwepo mashindano haya tunao, mazingara na malengo ya kuwepo mashindano haya yapo. Tatizo ni kwamba, vyote hivi vimevurugika au kukaa shaghalabagala na hivyo nia, malengo na madhumuni ya kumwendeleza Mtanzania kupitia mashindano katika sanaa hii nako kumevurugika kama si kuingia dosari.

Sitoendelea kuandika mengi kuhusiana na ma-miss wetu, ila nina wito kwa taasisi husika na wadhamini wa mashindano au sanaa hii:

Taasisi/Wizara:

==>Je, wanataarifa gani za kutupatia wanajamii kuhusiana na mchipuko huu wa mashindano? (wanaukubalia au kuukataa..)

==>Kama Wizara imeona jambo hili la kuongezeka kwa ghafla si jema, je imeandaa mkakati gani kulikabili?

==>Je Wizara na Taasisi husika zinashirikiana vipi na waandaji wa mashindano haya? (swala la vibali..)

Wadhamini:

==>Kwa vile wana uwezo wa kumudu udhamini, je ni mpango gani wanao katika kuchochea taaluma za vijana mashuleni kupitia mashindano mbalimbali?

==>Je, wanafikiria nini kuhusiana na swala la kuanzisha mashindano katika jamii ambayo yatatoa motisha kwenye mambo ambayo yanailenga jamii na mazingira yake kwa kuzawadia vijana au makundi ya vijana. Mfano katika:

---- Ujenzi wa vyoo
---- Usafi wa mazingira
---- Upandaji miti
---- n.k..

==>Ukiachilia mbali kuwezesha kujulikana kwa warembo wa Kitanzania ndani na nje ya nchi, je, wanampango gani na kuwawezesha warembo hawa kushiriki katika shughuli za maendeleo yanayogusa jamii moja kwa moja?

==>Ukiachilia mbali zawadi wanazowapatia washindi, je ni mpango gani wanao katika kuwezesha sanaa hii kuliingizia taifa fedha za kigeni bila kukiuka maadili yetu?

Napenda kumaliza kwa kusema kwamba, nia na madhumuni katika hayo yote niliyouliza ni kujua sisi kama wanajamii tuna mpango upi katika kuwawezesha vijana wawe wabunifu, washirikiane katika sekta mbalimbali ili 'hela hizo' za udhamini zisiende tu kwenye 'vipaji' vya watu ambavyo wamezaliwa navyo, bali hela na zawadi nyinginezo ziambatanazo na u-miss zitumike katika kuongeza tija, ubunifu na ufanisi wa kazi za vijana.

Shukrani; Naomba kutoa hoja.

SteveD
.

 
Wenzako wanaona umiss ni kama mchezo,

Wakikuuliza je una msimamo gani kuhusu ligi za mpira za sehemu zote ulizotaja utakuwa na msimamo gani?
 
Ebwana hili suala ni kweli kabisa sasa linaboa kwa sasa kutokana na uwepo wa uwingi wa mashindano haya, halafu kwa upande mwingine ukiangalia inakuwa kama washiriki wanakuja kujiuza vile. (Mtanisamehe dada zangu na wapenzi wote wa Mashindano haya lakini ndio ninavyoona kwa sasa)
 
Wenzako wanaona umiss ni kama mchezo,

Wakikuuliza je una msimamo gani kuhusu ligi za mpira za sehemu zote ulizotaja utakuwa na msimamo gani?

Pundit, swali zuri... jibu langu ni fupi na litakaa 'kiswali-swali';

-Sina uhakikika kama umelinganisha u-miss na michezo mingine kama riadha, kurusha tufe, table tenis, ndondi n.k... ambayo huweza hata kwenda Olympics.

-Ili kujibu, ngoja ni assume kuwa umelinganisha;
-Basi naomba nitumie mifano ili kujibu...

Leo hii nikienda Dodoma na kukutana na vijana kama kumi hivi, vijana walio wastaarabu na wenye uchu wa maendeleo katika michezo, mfano riadha. Basi nikawapatia vifaa vya michezo, mafunzo makali n.k. ili mradi tu kuwawezesha katika hiyo riadha... chances ni kwamba, kati ya hao vijana 10, kutatokea walau 2 hivi ambao watakuwa nyota ya Taifa....baada ya kijana mmoja wapo kuwa mshindi wa tatu katika riadha Africa.

Unaweza kubisha na kusema hivyo hivyo kwenye mashindano ya u-miss, lakini ukweli wa mambo ni kuwa, katika mashindano haya, na kwa kuchukua warembo kumi hivi kutoka Iramba, Singida, kama mfano, na kutumia resources ambazo zitakuwa same in monetary value kama kwa wanariadha... halafu basi mashindano hayo yakivuka kiwango cha taifa na kuwa kiwango cha kimataifa, na mmoja wa washiriki ambaye atakuwa kati ya hao 10, ang'are na kushika labda nafasi ya 3 hivi kwenye miss Africa....

Swali: Tukichukulia sekta ya utalii; Je kati ya hawa washindi wa tatu katika haya mashindano mawili tofauti, yupi anaweza kuendelea zaidi na kuvuka mashindano ndani ya Africa kuliwakilisha Taifa na kulitangaza, at the same time, kijana huyo aendelee kuwa mshindi na mshindi kwenye mashindano yanayofatia?
Samahani kwa kuwa hypothetical.

SteveD.
 
Steve,

Ndio maendeleo tunayoyaona ni maendeleo hayo......

Kwa hiyo sio kwamba priority zetu ziko twisted, hapana ziko straight kabisa. Siku tutakayoona ujenzi wa vyoo, upandaji miti, na usafi wa mazingira ni maendeleo ndio siku ambayo priority zetu zitakapo kuwa twisted!
 
mimi naona tunaweza kuendeleza mashindano ya umiss na pia kufanya mambo mengine ya maendeleo!kuwepo mashindano ya umiss hayazuii shughuli zingine
 
mimi naona tunaweza kuendeleza mashindano ya umiss na pia kufanya mambo mengine ya maendeleo!kuwepo mashindano ya umiss hayazuii shughuli zingine

Tatizo ni vipaumbele vyetu viko wapi...kama watu wako tayari kudhamini mamilioni kwenye mashindano ya umiss lakini hawadhamini ujenzi wa angalau jengo moja la shule au zahanati kwenye mji ambao hayo mashindano yanafanyika then kuna tatizo.
 
mimi naona tunaweza kuendeleza mashindano ya umiss na pia kufanya mambo mengine ya maendeleo!kuwepo mashindano ya umiss hayazuii shughuli zingine

Sawa Hollo, kama QM ndipo nami hapo ninaposema kuwa, wadhamini hawa na uwezo wao, wangewezesha na kupendezesha mengi sana katika jamii zetu pale ambapo wangeamua:
---kuzawadia wachimba na wazibua vyoo,
---kuzawadia waziba mashimo barabarani,
---kuzawadia vijana waliosadia vibibi vizee wengi visivyojiwezwa,
---kuzawadia n.k.

Sawa unaweza kusema kuwa kuna taasisi maalum kwa ajili ya kushughulika na maswala kama haya. Lakini the bottom line ni kwamba, inaonekana hatutumii uwezo wetu wenyewe pamoja na pesa tulizo nazo kuendeleza au kuchangia shughuli za kijamii ambazo zinalenga wengi badala ya watu wachache wenye 'vipajii vya kuzaliwa navyo'.

SteveD.
 
Tatizo ni vipaumbele vyetu viko wapi...kama watu wako tayari kudhamini mamilioni kwenye mashindano ya umiss lakini hawadhamini ujenzi wa angalau jengo moja la shule au zahanati kwenye mji ambao hayo mashindano yanafanyika then kuna tatizo.
unajua kwa nini wanadhamini ni kwa sababu na wao wanafaidika"that is business"
ila mimi naona huyu akidhamini umiss, fulani adhamini hayo mambo ya muhimu zaidi kuliko u miss!si unajua tena watu wanaangalia upepo!
Any way mimi na wewe twaweza kuwa wadhamini ok let our priorities ziwe katika mambo ya mazingira kwa mfano.
 
SteveD,

Nilifikiri mademu warembo ndio wanafanya dunia yako izunguke. Kumbe na wewe unajua kutamka "twisted priorities"?

Sawa, lakini mimi sitakuwekea mabandiko ya movie clips za warembo kutoka U-tube kama wewe na Brazameni mlivyo fanya kwenye thread ya kuuliza kama watu wanaweza ku-sacrifice party kufuatilia maswala ya Billali.

Ungeweza kusema tu wewe hukubaliani na hilo wazo kwa sababu utakuwa busy unafuatilia "Latina a##"

Lakini haikuwa lazima kubandika mi clips ya hip hop clowns. Nimesoma mawazo yako hapo juu nikagundua ulichofanya was beneath you. Mwachie Brazameni.

Baadae, mtu wangu.
 
KM, Umenikamata!!

Lakini sababu ya kuweka hivyo niliitamka.

Kimoja ambacho nitakuuliza hapa ni kuwa:
-kupi KUNGELI/KUTAWEZA kufanyika, maandamano hayo au watu kwenda kwenye hiyo party?
 
Pundit, swali zuri... jibu langu ni fupi na litakaa 'kiswali-swali';

-Sina uhakikika kama umelinganisha u-miss na michezo mingine kama riadha, kurusha tufe, table tenis, ndondi n.k... ambayo huweza hata kwenda Olympics.

-Ili kujibu, ngoja ni assume kuwa umelinganisha;
-Basi naomba nitumie mifano ili kujibu...

Leo hii nikienda Dodoma na kukutana na vijana kama kumi hivi, vijana walio wastaarabu na wenye uchu wa maendeleo katika michezo, mfano riadha. Basi nikawapatia vifaa vya michezo, mafunzo makali n.k. ili mradi tu kuwawezesha katika hiyo riadha... chances ni kwamba, kati ya hao vijana 10, kutatokea walau 2 hivi ambao watakuwa nyota ya Taifa....baada ya kijana mmoja wapo kuwa mshindi wa tatu katika riadha Africa.

Unaweza kubisha na kusema hivyo hivyo kwenye mashindano ya u-miss, lakini ukweli wa mambo ni kuwa, katika mashindano haya, na kwa kuchukua warembo kumi hivi kutoka Iramba, Singida, kama mfano, na kutumia resources ambazo zitakuwa same in monetary value kama kwa wanariadha... halafu basi mashindano hayo yakivuka kiwango cha taifa na kuwa kiwango cha kimataifa, na mmoja wa washiriki ambaye atakuwa kati ya hao 10, ang'are na kushika labda nafasi ya 3 hivi kwenye miss Africa....

Swali: Tukichukulia sekta ya utalii; Je kati ya hawa washindi wa tatu katika haya mashindano mawili tofauti, yupi anaweza kuendelea zaidi na kuvuka mashindano ndani ya Africa kuliwakilisha Taifa na kulitangaza, at the same time, kijana huyo aendelee kuwa mshindi na mshindi kwenye mashindano yanayofatia?
Samahani kwa kuwa hypothetical.

SteveD.

Itategemea na vipaji vyao individually, which says nothing to elevate any game or competitive activity agains beauty pageants.

My point ni kwamba, kama unaamini beauty pageants ni wrong priority basi uamini pia na mpira ni wrong priority, hapo utakuwa consistent.

Lakini haya mambo ya kulaumu the whole establishment of pageantry (labda kwa sababu ya wachache wanaoharibu) huku tunalalamika kwamba mpira haupewi kipaumbele is nothing but mfumodume.

Kama tunataka kuwa waimla na ku suspend michezo na burudani ili tufanye kazi (arguably, wengine wanaweza kukuambia burudani na michezo ni kazi) then tufanye hivyo across the board.

Kama tuna matatizo kwenye pageants ni wapi hakuna matatizo? Mpira una matatizo kibao mbona tunawashikia bango ma miss tu?

Kama kuna matatizo tuyaongelee haya matatizo.Mamiss wanajiuza, mamlaka zinazohusika zinawachuja vipi (kazi ngumu!) Utamaduni wetu unasemaje (nenda kafanye reasearch ya sagulaga uone kujiuza in some ways kupo hata kwenye utamaduni, kwa hiyo inawezekana hawa ma miss wanaenda na teknolojia ya muda huu tu badala ya kuwa na ngoma ya sagulaga leo kuna contests za u miss)

Mi sioni tatizo, as long as machangudoa hawavamii na kufanya mambo openly (I am not even sure this is not happenning, hence laying the scrutiny on individuals not the idea of pageants)
 
Itategemea na vipaji vyao individually, which says nothing to elevate any game or competitive activity agains beauty pageants.

My point ni kwamba, kama unaamini beauty pageants ni wrong priority basi uamini pia na mpira ni wrong priority, hapo utakuwa consistent.

Lakini haya mambo ya kulaumu the whole establishment of pageantry (labda kwa sababu ya wachache wanaoharibu) huku tunalalamika kwamba mpira haupewi kipaumbele is nothing but mfumodume.

Kama tunataka kuwa waimla na ku suspend michezo na burudani ili tufanye kazi (arguably, wengine wanaweza kukuambia burudani na michezo ni kazi) then tufanye hivyo across the board.

Kama tuna matatizo kwenye pageants ni wapi hakuna matatizo? Mpira una matatizo kibao mbona tunawashikia bango ma miss tu?

Kama kuna matatizo tuyaongelee haya matatizo.Mamiss wanajiuza, mamlaka zinazohusika zinawachuja vipi (kazi ngumu!) Utamaduni wetu unasemaje (nenda kafanye reasearch ya sagulaga uone kujiuza in some ways kupo hata kwenye utamaduni, kwa hiyo inawezekana hawa ma miss wanaenda na teknolojia ya muda huu tu badala ya kuwa na ngoma ya sagulaga leo kuna contests za u miss)

Mi sioni tatizo, as long as machangudoa hawavamii na kufanya mambo openly (I am not even sure this is not happenning, hence laying the scrutiny on individuals not the idea of pageants)
Naona unanitwika Dunia unnecessarily.

And my scrutiny is on the frequency and inevitability to which we all find ourselves engulfed in without realizing what have been our aims in first place.

One choses to talk about samaki as a variety in food doesn't mean one have and must talk about maembe ng'ong'o and binzari, just as so to cover the other variety!

Hapo kwenye research, pana utamu, maana ndipo hapo nilipotoa hoja yangu kwa wizara husika....ya kuwa, je wanatamko lolote kuhusiana na mwongezeko huu...
 
Sawa Hollo, kama QM ndipo nami hapo ninaposema kuwa, wadhamini hawa na uwezo wao, wangewezesha na kupendezesha mengi sana katika jamii zetu pale ambapo wangeamua:
---kuzawadia wachimba na wazibua vyoo,
---kuzawadia waziba mashimo barabarani,
---kuzawadia vijana waliosadia vibibi vizee wengi visivyojiwezwa,
---kuzawadia n.k.

Sawa unaweza kusema kuwa kuna taasisi maalum kwa ajili ya kushughulika na maswala kama haya. Lakini the bottom line ni kwamba, inaonekana hatutumii uwezo wetu wenyewe pamoja na pesa tulizo nazo kuendeleza au kuchangia shughuli za kijamii ambazo zinalenga wengi badala ya watu wachache wenye 'vipajii vya kuzaliwa navyo'.

SteveD.
sasa steve si ni bora hata wadhamini wanaodhamini umiss maana utleast wanawasaidia hao mabinti!ok Steve umejaribu ni pesa ngapi tunateketeza wakati wa harusi?kuanzia kitchen party hadi harusi yenyewe!mimi naona hao wadhamini wanaowadhamini mabinti nawapa hongera kwa kweli!yaani hadi kizawadia washimba mashimo barabarani tusubiri wadhamini?mimi naona tunazo pesa za kusaidia vibibi as far as tunateketeza mamilioni kwenye harusi kwa kuajirisha hao ambao tayari ni matajiri kwa kununua pombe zao!
So jukumu ni letu wenyewe!
 
sasa steve si ni bora hata wadhamini wanaodhamini umiss maana utleast wanawasaidia hao mabinti!ok Steve umejaribu ni pesa ngapi tunateketeza wakati wa harusi?kuanzia kitchen party hadi harusi yenyewe!mimi naona hao wadhamini wanaowadhamini mabinti nawapa hongera kwa kweli!yaani hadi kizawadia washimba mashimo barabarani tusubiri wadhamini?mimi naona tunazo pesa za kusaidia vibibi as far as tunateketeza mamilioni kwenye harusi kwa kuajirisha hao ambao tayari ni matajiri kwa kununua pombe zao!
So jukumu ni letu wenyewe!
......and we shall maintain the status quo!!!
 
Tatizo ni kwamba watu wavivu wa kubuni mbinu nyingine za entertainment na investment katika urembo.

Sasa imekuwa kama biashara ya vocha, kila kona kuna kibanda na kila mtaa una shindano lake la mamiss!!!
 
Kabla sijatoa opinion, naomba tu niweke link hapa la Michu jnr na comment ya mtu mmoja;

miss chan'gombe kumekucha

"hivi ukishika kiuno ndo umeshakua miss??????????? katika line nzima hapo sijaona mtu wa kuitwa miss."
 
halafu kwa upande mwingine ukiangalia inakuwa kama washiriki wanakuja kujiuza vile. (Mtanisamehe dada zangu na wapenzi wote wa Mashindano haya lakini ndio ninavyoona kwa sasa)

Biashara ni matangazo na nimebahatika kushiriki nikiwa katika Kamati ya Taifa ya Maandalizi ya Mashindano makubwa sana ya Urembo kutokea Tanzania na pamoja na hayo kushiriki katika Usimamizi wa mashindano toka ngazi za mikoa mpaka Taifa.

Kwa kweli kinachofanyika katika mashindano hayo kwa asilimia kubwa sana (Kama 85%) na Ukahaba usio na kichwa wala miguu. Hayo ni mashindano kwa ajili ya kunufaisha wajanja wachache sana na asilimia kubwa ya washiriki kama si wote mafanikio wanyopata ni kuwa wanatongozwa na wanaume mbali mbali na kuishia kufanya Umalaya sema ni katika stlye ya kistaarabu zaidi.

Kwa kweli kwa sasa haya mshindano yananirudisha kipindi cha nyuma, kipindi cha biashara ya watumwa ambapo walikuwa wananadiwa; yule mwenye nguvu na afya bora akipata bei ya juu zaidi. Sasa now ni soko huria ambao bidhaa bora sokoni (Washiriki wa mashindano ya urembo) ndo anakuwa na soko zaidi kwa Wanaume wenye uchu.

Haya Mashindano hayana dira kabisa. Uendeshaji wake umevuruga nia na maudhui ya Sanaa nzima ya urembo.

Hashim Lundenga, Gideon Chipungahelo na wengine ni muda wenu kujibadilisha na kufanya kitu ambacho jamii itajivunia badala ya kumrubuni binti mmoja kwa gari na wengine kuwauza kwa Wanaume wenye Uchu ili tu mpate pesa zao wakiwa kama wadhamini ama watu wenye nafasi katika nchi hii!!!
 
sasa steve si ni bora hata wadhamini wanaodhamini umiss maana utleast wanawasaidia hao mabinti!ok Steve umejaribu ni pesa ngapi tunateketeza wakati wa harusi?kuanzia kitchen party hadi harusi yenyewe!mimi naona hao wadhamini wanaowadhamini mabinti nawapa hongera kwa kweli!
Naomba nikuulize swali moja...umewahi enda kuomba udhamini wa mashindano ya Umiss na ukakutana na vikwazo ambavyo watakupatia mpaka kuweza kukupa udhamini huo

Sidhani kama ungekuwa unajua hawa wadhamini wanafanya nini na nini ungewapa hizo Praise.

Waulize Mamiss wenyewe nadhani ndo utasikia kilio chao lakini nao kwa kuwa wanakuwa kama ndo wamefungwa wanaishia kulia na kurudi kule kule.
 
Naomba nikuulize swali moja...umewahi enda kuomba udhamini wa mashindano ya Umiss na ukakutana na vikwazo ambavyo watakupatia mpaka kuweza kukupa udhamini huo

Sidhani kama ungekuwa unajua hawa wadhamini wanafanya nini na nini ungewapa hizo Praise.

Waulize Mamiss wenyewe nadhani ndo utasikia kilio chao lakini nao kwa kuwa wanakuwa kama ndo wamefungwa wanaishia kulia na kurudi kule kule.
...mithili ya watumiaji wa madawa ya kulevya wanavyokuwa nobbled na ma-dealers.

...MwM, una raise jambo muhimu sana kwenye jamii yetu ambalo ni muhimu liwekwe hadharani.

SteveD.
 
Back
Top Bottom