Yo Yo
JF-Expert Member
- May 31, 2008
- 11,217
- 1,702
Mbunge wa Viti Maalum Al-Shymaa Kwegiar akiwa na washiriki wa Miss Totoz
Fatuma Issa (7) ameibuka kidedea katika shindano la kumpata Malkia wa Watoto, Miss Totoz Temeke 2009 katika Ukumbi wa Equator Grill baada ya kuwashinda warembo wenzake 11 katika shindano lililokuwa gumu na la aina yake wakati majaji Mariam Chaheli, Jowalipokuwa wakichuja nafasi ili kumpata mrembo wa Ukweli kwa Watoto wa Wilaya ya Temeke.
Shindano hilo ambalo lengo lake ni kukuza na kuendeleza Sanaa kuanzia ngazi za chini lilikuwa na mvuto na msisimko mkubwa kutokana na watoto kuchuana vikali kila mmoja akiitaji kuibuka na ushindi na kuweka rekodi ya kwanza katika maisha yake katika shindano hilo, warembo waliobahatika kupanda jukwaani ni pamoja na Janey Anthony, Fatuma Issa, Zaituni Hassan, Neema Ally, Ester Frenk, Ashura Omary,Mariam Karama,Nasra Ally, Yunis Anthony, Angela Silayu,Happy Peter, na Eda Damian.
..........
"shindano hili kusema kweli ni la kipekee, ukiwatazama watoto unagundua kuwa pia wanaitaji kupatiwa mafunzo haya ikiwa mapema ili ifikapo wakati wa mshiriki anakuwa apati tabu na pia anakuwa ana tena aibu kama tunavyowashuhudia baadhi ya washiriki wanashindwa hata kujielezea, kujibu swali hata kama siyo gumu, ukweli wengi wao wanakuwa na aibu, hivyo watoto wakianza kufunzwa angali wadogo bila shaka siku zijazo tutakuwa na washiriki wengi wa Urembo"alisema Al-Shymaa
.......
kikubwa ninawaomba watu mbalimbali kujitokeza kusaidia kufanikisha shindano hili ambalo ni changamoto kwa watoto wetu, ili pia waweze kujitambua umuhimu wao juu ya masuala ya Urembo wakiwa bado wadogo kama ilivyom katika masuala mengine kama mpira wa miguu, na kikapu watoto wanaanza kuelimishwa wakiwa wadogo na hivyo kukua wakijua namna ya kuvitumia Vipaji vyao"alisema Jack
Mshindi wa kwanza katika shindano hilo alizawadiwa TV na Cheni, wa pili na wa tatu Radio na Cheni wa nne na tano walipatiwa cheni kila mmoja, sambamba na washiriki wote kupatiwa vifaa vya shule ikiwamo vitabu, peni, na madaftari ambavyo vyote vilikabidhiwa na mgeni Rasmi Mh. Mbunge Viti Maalum, Al-Shymaa Kwegiar.
http://michuzijr.blogspot.com/2009/08/fatuma-issa-7-ameibuka-kidedea-katika.html#comments
Attachments
Last edited: