Masheikh wapiga kambi Bungeni kushinikiza Mahakama ya Kadhi kupita

kyalankota

JF-Expert Member
Jul 27, 2014
2,560
1,399
Masheikh mbalimbali nchini wamejikusanya na kupiga kambi mjini Dodoma maeneo ya bunge ili kuhakikisha mahakama ya kadhi inapitishwa na bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
==========================

DSC_0701-640x430.jpg

MASHEIKH na Wanazuoni wa Kiislamu nchini wameamua kupiga kambi mjini Dodoma ili kuhakikisha wakati Bunge linajadili Mahakama ya Kadhi wawe eneo hilo kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.

Uamuzi huo umekuja baada ya kauli ya Maaskofu kuingilia madaraka ya Bunge kwa kulitaka lisijadili Mahakama ya Kadhi ambapo Tasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania wamesema wamesikitishwa na kauli hiyo na sasa wameamua kuweka kambi Dodoma ili kuona Bunge litaamua nini wakati wanajadili Mahakama ya Kadhi.

Taasisi mbalimbali za Kiislamu nchini zimeungana katika kuhakikisha Bunge linatoa fursa kuhusu Mahakama ya Kadhi ambayo imekuwa kilio cha Waislamu walio wengi kwa muda mrefu.

Akizungumza Dar es Salaam jana, kabla ya kuanza safari ya kwenda Dodoma, Katibu Mkuu wa Taasisi ya Masheikh na Wanazouni wa Kiislamu Tanzania, Sheikh Khamisi Mataka alisema kauli ya maaskofu kupitia Jukwaa la Wakristo Tanzania, ndilo limesababisha waweke kambi Dodoma ili kuwa karibu na Bunge.

Sheikh Mataka alisema hawakuwa na nia ya kwenda kuweka kambi Dodoma wakati Bunge litakapokuwa linajadili Mahakama ya Kadhi wiki hii, lakini kauli ya maaskofu imewafanya wafanye hivyo ili kuhakikisha haki inatendeka.

Alisema ikumbukwe ahadi ya marekebisho ya sheria kuitambua Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara , ni ahadi ya Serikali , hivyo alisema taasisi yao inawaomba maaskofu waachie uhuru wabunge waumini wa dini ya Kikristo kuujadili muswada huo bila shinikizo la kiimani na kuukataa.

"Tumeamua kwenda Dodoma kwa ajili ya kuwa karibuni na jikoni ambako wabunge wetu wote walio Waislamu na Wakristo watakupokuwa wanajadili Mahakama ya Kadhi , tuwe karibu.

"Kwa mujibu wa ratiba ya Bunge wiki hii moja ya muswada utakaojalidiliwa ni pamoja na Mahakama ya Kadhi.Hivyo hatuwezi kuwa mbali katika jambo ambalo linatuhusu,"alisisitiza Sheikh Mataka.

Wakati huo huo, Anicetus Mwesa anaripoti kuwa Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR Mageuzi), amesema Serikali inafanya ulaghai hata kwenye taasisi za dini.

Amesema kutokana na ulaghai huo ndiyo maana, Waziri Mkuu Mizengo Pinda mwaka jana alisema Serikali itapeleka bungeni vifungu vitakavyoifanya mahakama ya kadhi itambulike katika Katiba.

Mkosamali alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza kwenye kipindi cha tuongee asubuhi kinachorushwa na Staa Tv kilichokuwa kinazungumzia Katiba inayopendekezwa.

"Wiki hii kutatokea jambo kubwa sana bungeni, Waziri Mkuu aliwahaidi Waislamu kuwawezesha kupata mahakama, sasa wameleta bungeni vifungu viwili vitatu sasa moto wake watauona.

"Yaani serikali iko tayari kuvuruga amani ya nchi kwa kulazimisha mambo kwenye suala la Katiba wakati ukweli wanaujua kuwa mchakato huu unaoendelea si halali kisheria na kikanuni," alisema Mkosamali.

Kuhusu suala la ucheleweshaji wa kuigawa kwa wananchi Katiba pendekezwa, Mkosamali alisema Serikali inafanya makusudi ili wananchi wasijue kilichomo kwenye katiba hiyo na kwamba Watanzania wasitegemee kama itasambazwa kwani mpango uliopo ni kusambazwa chache.

Aidha, alisema mwaka huu, Ukawa watashinda uchaguzi mkuu na kwamba mwakani wataanzisha mchakato wa katiba ambao utakuwa umehusisha wananchi na wadau wote.

Naye, Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba alisema Ukawa wasitegemee ushindi wowote kwani dalili za kushindwa uchaguzi mkuu zimeonekana kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika Desemba 14, mwaka jana.

"Wananchi waliopiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa ni wale wale watakaopiga kura uchaguzi mkuu hivyo Ukawa waendelee kusubiri maumivu," alisema Nkumba.

Pia, aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kueleza umma kama muda wa kura ya maoni unatosha au hautoshi na si kukaa kimya kama ilivyo sasa.

"Tume inapaswa kueleza kama muda unatosha ama hautoshi ili Serikali iseme uamuzi mwingine. Pia, serikali inatakiwa kupeleka kwa wananchi Katiba pendekezwa ili waisome waelewe maudhui yake," alisema.

Kwa mujibu wa sheria namba tatu ya mwaka 2014, ambayo inahusu kura ya maoni inaeleza kuwa jambo la kwanza kufanyika ni uboreshaji wa daftari la wapiga kura ambao utafuatiwa na elimu kwa umma kwa miezi miwili kisha kampeni kwa mwezi mmoja.

Kura ya maoni kuhusu Katiba pendekezwa inatarajiwa kufanyika Aprili 30, mwaka huu.
Chanzo: Jambo leo
 
Masheikh mbalimbali nchini wamejikusanya na kupiga kambi mjini Dodoma maeneo ya bunge ili kuhakikisha mahakamavya kadhi inapitishwa na bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Source: JamboLeo, HabariLeo...

Sioni kama hili litawasaidia.
 
Na hapa Tawala imeweka mtu kati.
Ili ijinusuru, ichomoe mswada huo bungeni.

Upitishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni Karata muhimu kwa CCM kujihakikishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu pamoja na upitishwaji wa Katiba mpya. Mahakama ya Kadhi ikipita CCM wanao uhakika wa kura za Waislamu.
 
Upitishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni Karata muhimu kwa CCM kujihakikishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu pamoja na upitishwaji wa Katiba mpya. Mahakama ya Kadhi ikipita CCM wanao uhakika wa kura za Waislamu.

Sio Waislamu wote wanaitaka hiyo kadhi! Wanaoitaka hiyo kadhi ni waislamu maslahi!
 
Upitishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni Karata muhimu kwa CCM kujihakikishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu pamoja na upitishwaji wa Katiba mpya. Mahakama ya Kadhi ikipita CCM wanao uhakika wa kura za Waislamu.

Si kweli kuwa Waislamu wote wanaitaka Mahakama ya Kadhi ni kikundi kidogo cha Wajanja wa Bakwata ambao wanawinda mishahara toka Serikalini pasipo kujua kuwa kodi nyingi inatoka kwenye Pombe na wauza nguruwe ( kitimoto) . Waislamu wajanja hawataki Mahakama ya kadhi wao wanataka maendeleo na hao ndiyo wapiga kura, wale wenye modomo mara nyingi huwa si wapigaji kura hawana Msaada kwa lolote wapo kwa Ajili ya masilahi yao tu pasipo kujua pesa wanayoitaka walipwe inatokana na nini.
 
Masheikh mbalimbali nchini wamejikusanya na kupiga kambi mjini Dodoma maeneo ya bunge ili kuhakikisha mahakamavya kadhi inapitishwa na bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Source: JamboLeo, HabariLeo...

Huyo mhariri ana lake jambo. Inakuwaje atumie maneno KUSHINIKIZA au ni mwandishi mwenyewe bwana Mkalokota.
wamekwenda kushinikiza au kusikiliza hoja na mswaada ?

Hawa niwageni tu kama walivyo wageni wengine. Ikiwa wamekwenda kushinikiza twambieni wanamshinikiza nani kwa njia gani.

Acheni chuki
 
Taifa hili wala halina dini ila RAIA wake ndiyo mwenye dini, haiwezekani eti bunge la WANANCHI wote wenye dini na wasiyo na dini (wapagani) likae litunge sheria ya dini huu utakuwa wendawazimu. Haya mambo hapana hapa Tanzania labda kule kwingine siyo hapa kwetu haya mambo ya dini yapelekeni kwenye mabaraza ya dini zenu siyo serikalini. Lionee Uruma Taifa chini ya waasisi likipasuka wote tutapata matatizo tujifunze kuwa wavumilivu, udugu wa pamoja, kuchukuliana kwa madhaifu yetu, kuwezeshana kama watoto wa Taifa moja lisikuwa na dini na ukabila bali mambo hayo yabaki katika mioyo yetu na yasituchonganishe na kuleta uandui. Undugu wetu ni wa milele kama Waswahili na si wadini na wakabila.
 
win8

Anzisheni tu hizo mahakama zenu lakini sio kwa gharama za tusiohusika.Waislam,wakristo na wengineo wote wakitaka wagharamiwe na serikali kwenye mambo yao hili litakuwa taifa gani?
Taifa halina dini hili,tusitiane gharama zisizo na msingi.
 
Kwa msingi huo Kanisa je litakuwa limetakasika? Mana waislamu wanalipa kodi kote Tanzania na hela hiyo hiyo serikali ina-promote makanisa kupitia mfumo kiristo.
Hakuna cha Mfumo kiristo hapa Tz Serikali haina Dini na Waislamu wengi huwa hawalipi kodi kwani wengi si wachapa kazi, wale Waislamu wajanja walipa kodi na wasomi na wachapa kazi hawana Mda wa kuhangaika na Mahakama ya kadhi wapo busy na kutaka maendeleo kwani wanajua pato la Taifa hutokana na Pesa za kodi ya pombe na kitimoto ndiyo maana hawana mda wa kukaa vibalazani kudai vitu visivyo na tija.
 
kajirita

Mkuu kajirita, hiyo njia unayoipendekeza kwa CCM itawageukia na kuwamaliza! Kwanza sio CCM wote wanakubaliana na hoja ya Mahakama ya Kudhi kubebwa na serikali. HIvyo hilo litazalisha mpasuko kuzidi wa makundi ya wataka uraisi! Pili, sio "Waislamu" wote wanaokubaliana na uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, hivyo hawaitaiunga mkono CCM kwa hilo! Cha msingi washughulikie kero za wananchi zinazowapandishia hasira na chuki kwa seriakli na chama, na sio kutafuta mbinu mufilisi kama hizi!
 
mahakama ya kadhi ni mwiba kwa ccm wakiikubali ni janga kwao wakiikataa ni janga kwao, wakiikubali wanatokwa na wakiristo na wakiikataa wanatokwa na waislamu wanachotakiwa kufanya ni kutafuta ni kundi gani lina watu wengi,lakini kutokwa ni lazima,hayo ndio maoni yetu sisi kina gogo la shamba
 
Upitishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni Karata muhimu kwa CCM kujihakikishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu pamoja na upitishwaji wa Katiba mpya. Mahakama ya Kadhi ikipita CCM wanao uhakika wa kura za Waislamu.

Kwangu mimi silioni kama ni hoja ki ivyo, kwani si kila muislam anaitaka hiyo mahakama ya kadhi, Zanzibar ipo ila sidhan kama kuna watu wanapeleka mashauri yao huko, hala dini nyingine changanya na wapagani hivi wanaweza zidiwa na waiskam kweli kwa wingi?,CCM watuambie tu kwamba kwa sasa wanamkomoa Mwl Nyerere kwa kutekeleza sera za udini akizojuwa anazipiga hita, kwani ni nani asiyejua kuwa hii CCM inatamani hata Mwl Nyerere afifie au kufa kabida katika maskio na midomo ya watanzania, hata hapa ninavyoandika najua wanakerwa na mimi, ila naamini kuwa great mind never die, watahangaika sana ila mwisho wake watachemka katika kila kitu, it's just a matter of time ukweli utajipigania kuwa hii siyo nchi ya kiislam wa kikristu, hii ni Tz.
 
minyoo

Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 12 {1} inasema; Binadamu wote huzaliwa huru, na wote ni sawa. (2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. Hoja ya mashekhe kuweka kambi bungeni kwa ajili ya kujenga ushawishi (lobbing) kwa wabunge ili mahakama ya kadhi itambuliwe na katiba sidhani kama ni kosa, kwangu mimi hiyo ni haki yao ya kikatiba na pia ni wajibu wao kama viongozi wa ki imani, ninachoshindwa kuelewa kutoka kwa baadhi ya wachangiaji ni kwa nini tuwabeze na kuwakejeli kana kwamba wao hawana haki ya kutoa maoni yao?

Ninaamini wabunge watapima hoja kama mahakama ya kadhi itakuwa na manufaa kwa taifa itapitishwa kama haina itawekwa kapuni; binafsi siiungi mkono lakini napinga kejeli zinazotolewa za mashekhe kulala vibarazani au kanzu zao kuwa na kunguni na chawa au kuweka uchawi, hizo lugha haziwezi kuwa za G.T, tujiheshimu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom