Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hakuna muislamu anayeomba dua kwa jina la Yesu au Jibril au hata Muhammad. Kufanya hivyo ni kufuru kubwa.Missile nation umekosea.Mimi pia nilisikiliza hio dua.kama huelew dua zinavyoombwa rudi ukae chini ufanye research yako vizuri. usifikri shekh mkubwa kama yule alivamia tu kuomba dua .
hawataki kuwa wanafiki,
Kwani alhadi Musa ni mwislam?Hawa Mashehe wanauaibisha Uisilamu
Usimtetee Alhad. Alhad kakosea. Halafu kwa hayo maneno yako ya mwisho unatakiwa uzingatie haya; "Ijue Haqq, utawajua walio katika Haqq".Missile nation umekosea.Mimi pia nilisikiliza hio dua.kama huelew dua zinavyoombwa rudi ukae chini ufanye research yako vizuri. usifikri shekh mkubwa kama yule alivamia tu kuomba dua .
Nichukue nafasi hii kukushangaa wewe mtoa mada kwa kuchelewa kuifahamu bakwata, alhad na genge lake hawako pale kwaaajili ya ALLAH wanamaslahi yao binafsiKatika kile kinachoonekana ni unafiki wa dhahiri wa BAKWATA, Masheikh wa BAKWATA wameanza kutumia podium mbalimbali za hadhara kumfanyia kampeni Mgombea uraisi wa CCM.
Wiki kadhaa zilizopita Sheikh wa BAKWATA wa mkoa wa Dar es salaam bwana Alhadi, alionekana kung'aka na kumshambulia Muinjilisti Mwingira kwa madai kuwa anafanya kampeni madhabahuni, lakini haikupita hata miezi mitatu Sheikh huyo anasimama kwenye majukwaa ya kisiasa na kutumia jina la dini kumpigia kampeni Mgombea uraisi wa CCM.
Tofauti na Askofu Bagonza na Mwamakula ambao wao huombea mikutano bila ya kuwaambia wananchi wamchague nani, huyu sheikh wa BAKWATA wa Dar es salaam amekwenda mbali na kupiga kampeni kabisa kuuombea kura mgombea huyo wa CCM.
Wakati huohuo, Sheikh huyo wa BAKWATA wa mkoa wa Dar es salaam amewashangaza sana Waislamu kwa kwenda kinyume kabisa na Imani ya dini ya dini hiyo kwa kufanya maombi kwa jina la Yesu kitu ambacho ni marufuku na ni kufuru kubwa sana kwa mujibu wa dini hiyo. Katika dini ya Uislamu inapaswa kuomba kwa Jina la ALLAH(Mwenyezi Mungu muumba mbingu na nchi) peke yake na si kwa jina la Kiumbe yeyote hata awe nabii au hat Malaika. Kwa mujibu wa dini ya Kiisamu Yesu ni nabii na Siyo Mungu.
Kauli hiyo imedhihirisha kuwa Sheikh huyo anaweza kufanya lolote hata kufanya kufuru ya wazi ilimradi awe karibu na watawala.
Kitendo cha Sheikh Alhadi kusema kuwa anaomba kwa jina la Yesu, kisha baadae kutamka Bismillah Rrahmaani rrahiim (yaani kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema) anaimply kuwa Jina la Allah ndiyo Jina la Yesu kitu ambacho ni kufuru kubwa sana kwa muislamu kuifanya.
Matendo haya ya BAKWATA kushindwa kulinda misingi ya dini ya uislamu yanaendelea kujitokeza mara kwa mara na yamekuwa yskiwakera waislamu wengi.
Ni wajibu wa Sheikh Mkuu na waislamu kiujumla kuchukua hatua maana hii tabia ya Masheikh hawa kuvunja misingi ya waziwazi ya dini ya kiislamu kwa sababu ya maslahi machache ya dunia yatapotosha watoto wa kiislamu na waislamu wengine kuikosa Tawhidi ya kweli.
Kama Alhadi alidhani waislamu watampa kura mgombea wa CCM kwa kufanya kufuru ya wazi namna hii basi ndiyo kwanza kamharibia!
Ndiyo tatizo la hawa ndugu zetuTatizo ni elimu. Mtu kaishia madrasa, unatarajia nini.
Ni tawi la CCM siku zoteUzuri ni kwamba BAKWATA ilishadharauliwa na kila mtu nchi hii.
Wala sio tatizo kuishia madrasa tu,Ndiyo tatizo la hawa ndugu zetu
Sio kweli tatizo kuishia madrasa bali ni udhaifu wa mtu binafsi kushindwa kuwa mwadilifu kwa dini yakeTatizo ni elimu. Mtu kaishia madrasa, unatarajia nini.
Mbona mnashangilia Sheikh Ponda aliposema Waislamu wote wamchague Lissu. Je Ponda siyo kiongozi wa dini? Kumbe mkuki kwa nguruwe.Katika kile kinachoonekana ni unafiki wa dhahiri wa BAKWATA, Masheikh wa BAKWATA wameanza kutumia podium mbalimbali za hadhara kumfanyia kampeni Mgombea uraisi wa CCM.
Wiki kadhaa zilizopita Sheikh wa BAKWATA wa mkoa wa Dar es salaam bwana Alhadi, alionekana kung'aka na kumshambulia Muinjilisti Mwingira kwa madai kuwa anafanya kampeni madhabahuni, lakini haikupita hata miezi mitatu Sheikh huyo anasimama kwenye majukwaa ya kisiasa na kutumia jina la dini kumpigia kampeni Mgombea uraisi wa CCM.
Tofauti na Askofu Bagonza na Mwamakula ambao wao huombea mikutano bila ya kuwaambia wananchi wamchague nani, huyu sheikh wa BAKWATA wa Dar es salaam amekwenda mbali na kupiga kampeni kabisa kuuombea kura mgombea huyo wa CCM.
Wakati huohuo, Sheikh huyo wa BAKWATA wa mkoa wa Dar es salaam amewashangaza sana Waislamu kwa kwenda kinyume kabisa na Imani ya dini ya dini hiyo kwa kufanya maombi kwa jina la Yesu kitu ambacho ni marufuku na ni kufuru kubwa sana kwa mujibu wa dini hiyo. Katika dini ya Uislamu inapaswa kuomba kwa Jina la ALLAH(Mwenyezi Mungu muumba mbingu na nchi) peke yake na si kwa jina la Kiumbe yeyote hata awe nabii au hat Malaika. Kwa mujibu wa dini ya Kiisamu Yesu ni nabii na Siyo Mungu.
Kauli hiyo imedhihirisha kuwa Sheikh huyo anaweza kufanya lolote hata kufanya kufuru ya wazi ilimradi awe karibu na watawala.
Kitendo cha Sheikh Alhadi kusema kuwa anaomba kwa jina la Yesu, kisha baadae kutamka Bismillah Rrahmaani rrahiim (yaani kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema) anaimply kuwa Jina la Allah ndiyo Jina la Yesu kitu ambacho ni kufuru kubwa sana kwa muislamu kuifanya.
Matendo haya ya BAKWATA kushindwa kulinda misingi ya dini ya uislamu yanaendelea kujitokeza mara kwa mara na yamekuwa yskiwakera waislamu wengi.
Ni wajibu wa Sheikh Mkuu na waislamu kiujumla kuchukua hatua maana hii tabia ya Masheikh hawa kuvunja misingi ya waziwazi ya dini ya kiislamu kwa sababu ya maslahi machache ya dunia yatapotosha watoto wa kiislamu na waislamu wengine kuikosa Tawhidi ya kweli.
Kama Alhadi alidhani waislamu watampa kura mgombea wa CCM kwa kufanya kufuru ya wazi namna hii basi ndiyo kwanza kamharibia!
Ponda ni kiongozi wa Taasisi gani ya Kiislamu?Mbona mnashangilia Sheikh Ponda aliposema Waislamu wote wamchague Lissu. Je Ponda siyo kiongozi wa dini? Kumbe mkuki kwa nguruwe.
Kazi ya dini ni kupinga uovu na sio kubarikiMbona mnashangilia Sheikh Ponda aliposema Waislamu wote wamchague Lissu. Je Ponda siyo kiongozi wa dini? Kumbe mkuki kwa nguruwe.