aleesha
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 775
- 1,117
"Mgeni sio kwamba ananunua ardhi, na sio kwamba anapewa umiliki wa 100% hapana anapewa kibali cha kuwekeza kwa miaka kadhaa. Kwa mtu anayetoka Tanzania Bara ambaye anataka kufanya Uwekezaji Zanzibar anatumia utaratibu huo huo" Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Ally Mwinyi.
====
Rais Mwinyi, ametoa ufafanuzi kuhusu suala la uwekezaji kwa wa wageni wote wanaotoka nje ya visiwa hivyo ikiwemo Tanzania Bara kuwa hawataweza kupata umiliki asilimia 100 ya umuliki wa ardhi isipokuwa watakodishiwa maeneo hayo.
Amesema kuwa utaratibu huo upo kwa kufuata masharti yaliyowekwa ya umiliki wa ardhi ambao unataka wazawa kuwa wamiliki pekee wa ardhi.
"Mgeni (anayetoka nje ya nchi) sio kwamba ananunua ardhi, na sio kwamba anapewa umiliki wa 100% hapana anapewa kibali cha kuwekeza kwahiyo anakuwa na hati inayoonyesha kwamba amekodishwa ardhi kwa miaka kadhaa ili awekeze na masharti yanawekwa"
"Kwa mtu anayetoka Tanzania Bara ambaye anataka kufanya Uwekezaji Zanzibar anatumia utaratibu huo huo"
"Kwa upande wa umiliki wa ardhi unabaki kwa Wazanzibar pekee yao kwamba Mzanzibar aliyezaliwa hapa Zanzibar ndiye ana haki ya kumiliki ardhi kwa mujibu wa sheria zetu" Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Ally Mwinyi.
====
Rais Mwinyi, ametoa ufafanuzi kuhusu suala la uwekezaji kwa wa wageni wote wanaotoka nje ya visiwa hivyo ikiwemo Tanzania Bara kuwa hawataweza kupata umiliki asilimia 100 ya umuliki wa ardhi isipokuwa watakodishiwa maeneo hayo.
Amesema kuwa utaratibu huo upo kwa kufuata masharti yaliyowekwa ya umiliki wa ardhi ambao unataka wazawa kuwa wamiliki pekee wa ardhi.
"Mgeni (anayetoka nje ya nchi) sio kwamba ananunua ardhi, na sio kwamba anapewa umiliki wa 100% hapana anapewa kibali cha kuwekeza kwahiyo anakuwa na hati inayoonyesha kwamba amekodishwa ardhi kwa miaka kadhaa ili awekeze na masharti yanawekwa"
"Kwa mtu anayetoka Tanzania Bara ambaye anataka kufanya Uwekezaji Zanzibar anatumia utaratibu huo huo"
"Kwa upande wa umiliki wa ardhi unabaki kwa Wazanzibar pekee yao kwamba Mzanzibar aliyezaliwa hapa Zanzibar ndiye ana haki ya kumiliki ardhi kwa mujibu wa sheria zetu" Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Ally Mwinyi.