Mashamba ya Bangi yateketekezwa Tarime

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani Tarime mkoani Mara imeendesha oparesheni kali na kufanikiwa kukamata mashamba makubwa ya zao la bangi ikiwemo bangi kavu ambayo tayari imeandaliwa kwa ajili ya kusafirishwa kwenda nchi jirani kwa ajili ya kuuzwa.

Chanzo: ITV
 
Hawa watu wataendeleza biashara hii haramu na ya hasara hadi lini?
 
Sipati picha wakiiochoma moto labda wanyanganywe silaha zote maana kitakachoendelea sitaki ushahidi hapo!!!
 
Serikali itafute njia mbadala ya kuteketeza mashamba haya ya bangi. Jinsi nilivyoona wanafyeka na kuchoma kienyeji zoezi hili linaweza kuwaletea madhara ya kiafya askari na ukizingatia moshi wa bangi ni hatari kwa MTU asiyetumia. Nashauri zitafutwe harvesting machine kwa ajili ya kuvuna na ziwepo insilirators kwa ajili ya utekeyezaji salama
 
Mkuu, wanapata hasara sana, hofu pekee ni hasara kubwa, usidhani kuwa na biashara au pesa ikuleteayo hofu ni faida...no kubwa
Kwenye hofu na kuishi tumbo joto nakuunga mkono.. Ila kwenye pesa ni lazima wanafaidika bro.. Kwa maana mimi naamin huwez ukafanya biashara ya hasara alaf uikazanie hiyo hiyo kila uchao..
 
Nimeona habari kupitia kituo cha ITV inahusiana na maswala ya uharibuji wa mashamba ya bangi huko Tarime lakini ghafla nikaona mtu mmoja ambae ameambatano na polisi akionyesha bendera ya CHADEMA wakiwa kwenye uteketezaji wa shamba hilo. Sijaelewa hebu waliiona habari nijuzeni.

==================



Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani Tarime mkoani Mara imeendesha oparesheni kali na kufanikiwa kukamata mashamba makubwa ya zao la bangi ikiwemo bangi kavu ambayo tayari imeandaliwa kwa ajili ya kusafirishwa kwenda nchi jirani kwa ajili ya kuuzwa.

Chanzo: ipp media
 
Mkuu sasa hapo tatizo nn? Kuoneshwa bendera ya chadema auuu kuna jingine? Au unataka nape apite nayo pia?
Atakua ni kiongoz wa chama.
 
Nimeona habari kupitia kituo cha ITV inahusiana na maswala ya uhalibuji wa mashamba ya mangi huko tarime lakini ghafla nikaona mtu mmoja ambae ameambatano na polisi akionyesha bendera ya chadema wakiwa kwenye uteketezaji wa shamba hilo sijaelewa hebu waliiona habari nijuzeni
Wewe pia si umeiona habari? Sasa walioiona habari si na wao wameona hicho hicho ulichoona?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom