Mashabiki wa Barcelona wamechukizwa na adhabu aliyopewa Sergio Ramos

Ryzen

JF-Expert Member
Dec 6, 2012
7,305
8,655
Jina la beki wa kati wa Real Madrid na nahodha wa timu hiyo Sergio Ramos bado linazidi kugonga headlines katika mitandao ya kijamii, Ramos bado amekuwa akijadiliwa na mashabiki wa soka kuhusiana na kadi yake nyekundu aliyooneshwa wakati wa mchezo wa El Clasico dhidi ya FC Barcelona.

Sergio Ramos alioneshwa kadi nyekundu dakika ya 77 ya mchezo baada ya kumchezea faulo Lionel Messi inayoaminika kuwa ni mbaya kwa mashabiki wa Barcelona, licha ya kuoneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja walitamani kuona Ramos akikosa mchezo zaidi ya mmoja kwa kosa hilo.
Beki huyo kwa sasa ataukosa mchezo mmoja wa Real Madrid wa siku ya Jumatano dhidi ya Deportivo utakaochezwa katika uwanja wa Municipal Riazor, kitendo ambacho hakijawafurahisha mashabiki wa Barcelona na kulaumu mitandaoni wakiamini Ramos anastahili kukosa mchezo zaidi mmoja kwa faulo aliyomchezea Lionel Messi
upload_2017-4-26_14-6-47.jpeg

upload_2017-4-26_14-4-59.jpeg
 
Mashabiki wa Madrid nao wanataka Neymar akose mechi ngapi? Kuwa balanced!
 
Mti wenye matunda Ndio unaopigwa mawe. LA Liga ni strong league than EPL, ndo maana wana timu 2 Kati ya 4 zilizotinga semi final ya UCL. Ambapo EPL Hawana timu hata moja
Kwa kigezo hicho French and Seria A ni ligi bora kuliko EPL. Kutwa mnashinda kwenye vibanda kuangalia EPL. Wewe angalia unachopenda usitake kuwaambia watu wachague nini au Dstv tu wanapunulia EPL.
 
Ligi ya hispania figisu nyingi sana....
Huo upande wa dikteta Franco una pendelewa kwa mengi sana.
 
Mti wenye matunda Ndio unaopigwa mawe. LA Liga ni strong league than EPL, ndo maana wana timu 2 Kati ya 4 zilizotinga semi final ya UCL. Ambapo EPL Hawana timu hata moja

Strong league kivipi?, miaka yote timu mbili tu ndio zinapokezana ubingwa
 
Back
Top Bottom