jyfranca
JF-Expert Member
- Oct 3, 2010
- 297
- 8
- Ukurasa Mkuu
- Habari za Kitaifa
- Habari za Mataifa Mbalimbali
- Habari za Burudani na Michezo
- Makala
- Habari za Biashara
- Maoni na Barua
Home
JK aongoza kwa kura majimbo ya Mwanza
Monday, 01 November 2010 19:12 newsroom
Na Peter Katulanda, Mwanza
MGOMBEA urais wa CCM Rais Jakaya Kikwete ameongoza kwa kupata kura nyingi katika majimbo ya mkoa wa Mwanza, huku CHADEMA kikishinda viti vitatu vya ubunge vikiwemo vya majimbo ya mjini, Ilemela na Nyamagana jijini hapa. Kwa mujibu wa matokeo ya awali katika majimbo hayo, CCM kimepata majimbo sita, huku jimbo la Misungwi likongoza kwa kura nyingi za rais, mbunge na kuzoa kata zote.
Habari zilizopatikana hapa kutoka majimbo hayo, CHADEMA kimezoa madiwani katika kata 11 kwenye majimbo ya Ilemela na Nyamagana ambayo yanaunda Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa kuwa na kata 21. Jimbo lingine lililokwenda na Chadema ni la Ukerewe, huku CCM mbali na Misungwi ikishinda katika majimbo ya Kwimba na Magu. Mengine ni Sumve, Buchosa na jimbo la Busega.
Kata tano zilizochukuliwa na CHADEMA jimboni Nyamagana ni Isamilo, Mahina, Igoma, Pamba na Mbugani, huku jimbo la Ilemela zikiwa ni pamoja na Kirumba, Nyamanoro, Pasiansi, Ilemela, Nyakato na Kitangiri.